Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,348
- 6,472
Mama Salma amesema anampigia debe mumewe kwa sababu ndiye msaidizi wake wa karibu kwenye masuala ya maendeleo ya jamii nchini kwa sababu anamiliki WAMA Foundation(Majira 23/09/2010). Hivi HakiElimu sio msaidizi wa JK kwenye masuala ya elimu? TGNP kwenye jinsia? LHRC kwenye haki za binadamu? Je, hawa nao wampigie kampeni JK? Au wabaki bila kuegemea upande wowote na kumtaka yoyote atakayeimarisha hayo wanayoshughulikia?
Hii inaonesha kuwa Urais kwa JK ni suala la kifamilia! Je, wanawake wote Tanzania ni UWT? WAMA Foundation ni UWT? Hivi baada ya miaka mitano kama JK atashinda, atafanyaje? Je, WAMA Foundation itakufa? Je, JK akishindwa mwaka huu kama polls zinavyo onyesha, WAMA Foundation itakufa? Je, kwa sasa WAMA Foundation inafuata sheria? Kilefu cha WAMA ni Wanafamilia na Marafiki Foundation na sio Wanawake na Maendeleo!!!!!!!
Hii inaonesha kuwa Urais kwa JK ni suala la kifamilia! Je, wanawake wote Tanzania ni UWT? WAMA Foundation ni UWT? Hivi baada ya miaka mitano kama JK atashinda, atafanyaje? Je, WAMA Foundation itakufa? Je, JK akishindwa mwaka huu kama polls zinavyo onyesha, WAMA Foundation itakufa? Je, kwa sasa WAMA Foundation inafuata sheria? Kilefu cha WAMA ni Wanafamilia na Marafiki Foundation na sio Wanawake na Maendeleo!!!!!!!