Fred Mpendazoe
Member
- Aug 21, 2016
- 33
- 504
Ninaona maandiko mengi yakieleza kwamba hatua nyingi zinazochukuliwa na Serikali ya CCM chini ya uongozi mahiri wa JPM, yalisemwa na Chadema kupitia Tundu Lissu au Mnyika au Mbowe. Hii siyo hoja imara.
Hapa duniani wapo watu ambao wanaweza kusema jambo ukadhani wanasema jambo hilo kwa dhati kumbe wanaamini tofauti kabisa. Mfano Chadema walimsema sana Lowassa kama fisadi kwa zaidi ya miaka 10, lakini hawakuyaamini waliyoyahubiri. Ndiyo maana mwaka 2015 wakampokea Lowassa kuwa mgombea urais. Watanzania wakaihukumu Chadema kwenye uchaguzi Mkuu.
Wabunge wa Chadema wamehubiri sana demokrasia na kufanya maandamano kudai demokrasia pana. Wabunge hao walifunga midomo kuonyesha hisia hizo wakiwa bungeni. Lakini uteuzi wa wagombea ubunge wa bunge la Afrika Mashariki ikadhihirisha kwamba wanachokisema si kile wanachokiamini. Ndani ya Chadema demokrasia ni kwa masilahi mapana ya kikundi cha watu.
Kwahiyo madai ya Chadema na viongozi wa Chadema kudai kwamba yanayotekelezwa kwa sasa wao waliyasema siku nyingi ni hoja isiyo na mashiko.
Jambo lililo mhimu na la msingi ni mwenendo chanya wa viongozi na wanachama wa chama cha siasa kwa jamii. Pili chama cha siasa kinatakiwa kusimamia kinachokiamini. Siyo kuhubiri tu.
Kingine, lugha zinazotumika na baadhi ya viongozi wa Chadema mara nyingi huonyesha upungufu wa maadili na inawafanya watanzania wajiulize, je watu hawa wakipewa madaraka watakuwaje ? Ukosoaji wa Chadema umekuwa wa matusi. Na ukiwa mtukanaji wa Serikali utapewa sifa nyingi sana na hata kuitwa jiniasi- genius. Ni ujinga. Hitler alikuwa genius lakini alikuwa mharibifu pia. Unaweza ukawa genius na unajua sana sheria lakini bila moyo wa uzalendo hautakuwa na faida kwa jamii.
Rais JPM anafanya kazi njema, watanzania tumuunge mkono.
Hapa duniani wapo watu ambao wanaweza kusema jambo ukadhani wanasema jambo hilo kwa dhati kumbe wanaamini tofauti kabisa. Mfano Chadema walimsema sana Lowassa kama fisadi kwa zaidi ya miaka 10, lakini hawakuyaamini waliyoyahubiri. Ndiyo maana mwaka 2015 wakampokea Lowassa kuwa mgombea urais. Watanzania wakaihukumu Chadema kwenye uchaguzi Mkuu.
Wabunge wa Chadema wamehubiri sana demokrasia na kufanya maandamano kudai demokrasia pana. Wabunge hao walifunga midomo kuonyesha hisia hizo wakiwa bungeni. Lakini uteuzi wa wagombea ubunge wa bunge la Afrika Mashariki ikadhihirisha kwamba wanachokisema si kile wanachokiamini. Ndani ya Chadema demokrasia ni kwa masilahi mapana ya kikundi cha watu.
Kwahiyo madai ya Chadema na viongozi wa Chadema kudai kwamba yanayotekelezwa kwa sasa wao waliyasema siku nyingi ni hoja isiyo na mashiko.
Jambo lililo mhimu na la msingi ni mwenendo chanya wa viongozi na wanachama wa chama cha siasa kwa jamii. Pili chama cha siasa kinatakiwa kusimamia kinachokiamini. Siyo kuhubiri tu.
Kingine, lugha zinazotumika na baadhi ya viongozi wa Chadema mara nyingi huonyesha upungufu wa maadili na inawafanya watanzania wajiulize, je watu hawa wakipewa madaraka watakuwaje ? Ukosoaji wa Chadema umekuwa wa matusi. Na ukiwa mtukanaji wa Serikali utapewa sifa nyingi sana na hata kuitwa jiniasi- genius. Ni ujinga. Hitler alikuwa genius lakini alikuwa mharibifu pia. Unaweza ukawa genius na unajua sana sheria lakini bila moyo wa uzalendo hautakuwa na faida kwa jamii.
Rais JPM anafanya kazi njema, watanzania tumuunge mkono.