Je, wakoloni wasingejikatia vitalu, Afrika ingekuwa ni taifa moja?

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,035
40,700
Inasemekana mataifa ya kikoloni kama Uingereza,Ujerumani, Ufaransa, Ubelgiji, Uitaliano na Ureno walijikatia vitalu katika Ardhi ya Afrika mithili ya watoto wakikatiana keki mnamo mwaka 1884 katika mkutano uliopewa jina la 'Berlin confrence' huko ujerumani. Kabala ya hapo hapakuwa na mipaka katika nchi za kusini mwa jangwa la Sahara, sana sana ilikuwa ni mipaka ya kufikirika baina ya 'chieftains' na 'kingdoms' mbali mbali. Je, bila kumegwa huko na wakoloni, leo hii tungekuwa taifa moja?, na je, tungekuwa ni 3rd world country? Na je, tungepewa kiti cha kudumu katika baraza la usalama la umoja wa mataifa? Je, tungekuwa taifa kubwa na lenye nguvu kama nchi zingine zenye eneo kubwa kijiografia,mfano Russia, China, India, USA?
 
Hizo kingdoms zilikuwa na mipaka na milki zake!!tena mipaka yao ilikuwa mizuri huwezi kukuta jamii moja imegawanywa kama ambavyo Leo kuna wamasai waliopo Kenya na Tanzania!!Kimsingi mipaka ni dhahania zaidi...sehemu chache duniani mipaka ni vitu halisi kama kuta na fensi
 
Ya kwamba ingekuwa taifa moja sidhani bali yangekuwa mataifa mengi madodo madogo zaidi labda ingejitokeza sababu nyingine ya kihistoria kabla wakoloni hawajajimegea mapande makubwa makubwa
 
Ukisoma pia historia athari mojawapo kuu ya ukoloni ni kuharibu ubunifu uliokuwa ukiendelea miongoni mwa jamii za kiafrika!!wakoloni wangechelewa miaka 200 plus wangekuta maendeleo makubwa tu yameshafikiwa!!Lakini athari kubwa zaidi ya ukoloni IPO ktk fikra!!Wametuathiri fikra zetu kwa kiasi kisichoweza kupona tena!!Matatizo mengi tuliyonalo Leo ni kwa sababu hatujajikomboa kifikra!!Sababu nyingine zozote ni visingizio!Tunahitaji kujikomboa kifikra
 
Ukisoma pia historia athari mojawapo kuu ya ukoloni ni kuharibu ubunifu uliokuwa ukiendelea miongoni mwa jamii za kiafrika!!wakoloni wangechelewa miaka 200 plus wangekuta maendeleo makubwa tu yameshafikiwa!!Lakini athari kubwa zaidi ya ukoloni IPO ktk fikra!!Wametuathiri fikra zetu kwa kiasi kisichoweza kupona tena!!Matatizo mengi tuliyonalo Leo ni kwa sababu hatujajikomboa kifikra!!Sababu nyingine zozote ni visingizio!Tunahitaji kujikomboa kifikra
Nakubaliana na wewe. Kuhusu mipaka.. na sisi tungepitia mfumo uleule waliopitia wao: vita na conquest.. kumbuka mpaka leo mipaka ya Ulaya haijawa fixed (rejea issue ya Crimea).. Ujerumani imefix mipaka yao 1990s.

In short walitunyang'anya haki yetu ya kufix mipaka kutokana na asili zetu na makabila.. ila pia wametuepusha na vita na disunity.. maana leo tusingekuwa na Tanzania inayoongea Kiswahili.
 
Back
Top Bottom