Je wajua unaweza kuambukizwa VVU/UKIMWI hata kama uliyefanya naye ngono zembe umempima na majibu yamekuja Negative?

Justdr

Member
Jun 1, 2021
51
89
Habari za muda huu?
Najua mko wazima kabisa! Wale mnaoumwa Mungu awajalie mrudi kwenye hali zenu za kawaida.

Kumekuwa na hii imani kuhusu Virusi Vya UKIMWI watu wanatumia isivyo vipimo vya VVU(HIV SD BIOLINE au OraQuick HIV test) kama namna moja ya kijikinga ya haya maradhi. Watu wamekuwa wakipima mtu wakikuta yuko negative basi wanaona ni salama kufanya ngono bila kinga kwa maana kipomo kinasoma negative.

Ukweli ni kwamba kipimo kusoma negative haimaanishi kwamba hauwezi kuambukizwa VVU/HIV.

Ukiwa na uelewa wa vitu hivi viwili hautarudia kufanya tena hii mistake, Kitaalam kuna kitu kinaitwa WINDOW PERIOD na INCUBATION PERIOD. Tutaongelea zaidi window period maana ndo inahusika zaidi hapa.

WINDOW PERIOD ni Kipindi toka mtu ambukizwe hadi kutengenezwa kwa kingamwili dhidi ya VVU kwa kawaida huwa chini ya mwezi 1 lakini inaweza kuwa hadi miezi 3.

Hizi kingamwili(antibodies) ndo uwa zinapimwa na hivi vipimo Tajwa hapo juu mtu akiwa nazo ndo kipimo kinasoma positive yani ameathirika (Ndo maana ukienda vituo vya kutolea huduma za afya kupima afya yako unaambiwa upo okay but rudi baada ya miezi mitatu)

INCUBATION PERIOD hiki ni kipindi toka mtu apate maambukizi ya VVU hadi hatakapoanza kuonesha dalili ambayo kwa kawaida ni kuanzia mwezi mmoja mpaka zaidi ya miaka kumi (binadamu tunatofautiana)

Kwahiyo ikitokea umefanya mapenzi/ngono zembe na mtu ambaye umempima yuko negative ila yupo Window period unakuwa uko hatarini zaidi kupata HIV /VVU kwasababu huu ndo muda virusi vinakuwa vinajizalisha zaidi kwenye mwili na kingamwili bado inakuwa haijatengenezwa kupambana na hivi virusi. Let's be care!

Points to Note.
  • Kutumia vipimo vya HIV siyo namna sahihi ya kujikinga na haya maradhi.
  • Kuna uwezekano mkubwa wa kupata HIV hata kama mwenzi wako umempima na ukakuta yuko Negative
  • Matumizi ya kondomu yatabaki kuwa kinara wa kujikinga na HIV pamoja na magonjwa mengine ya zinaa.
UKIMWI UPO NA UNAUA TUJIKINGE
Kama una swali karibu.
 
Mkuu na vipi kuhusu hawa Carrier ambaye anaweza kaa zaidi ya miaka hata 7 na wakimpima haoneshi kama ana HIV..!?
Hawa hawaitwi carrier bali ni wagonjwa wa HIV kama walivyo wengine sema wao wanakuwa wametumia ARVs na kufata mashariti vizuri kiasi kwamba wakifanya kipimo kinaonesha hawana HIV zinakuwa undetectable)
Sema hawa uwezo wao wa kuambukiza wengine Unakuwa mdogo sana.
 
Hawa hawaitwi carrier bali ni wagonjwa wa HIV kama walivyo wengine sema wao wanakuwa wametumia ARVs na kufata mashariti vizuri kiasi kwamba wakifanya kipimo kinaonesha hawana HIV zinakuwa undetectable)
Sema hawa uwezo wao wa kuambukiza wengine Unakuwa mdogo sana.
Huyu ninae mjua ye hatumii hata ARVs
 
Kuna mmoja tupo nae mtaa mkewe alishafariki na waya lakini yeye anadunda tu na inavyosemekana ni yeye alimpa mke wake lakini yeye akipima hakuna.
Yah kibongo bongo wanaweza kuwepo ila ni adim sana mimi nmebahatika ni resistant na malaria (siwezi kushikwa na malaria)
 
Habari za muda huu?
Najua mko wazima kabisa! Wale mnaoumwa Mungu awajalie mrudi kwenye hali zenu za kawaida.

Kumekuwa na hii imani kuhusu Virusi Vya UKIMWI watu wanatumia isivyo vipimo vya VVU(HIV SD BIOLINE au OraQuick HIV test) kama namna moja ya kijikinga ya haya maradhi. Watu wamekuwa wakipima mtu wakikuta yuko negative basi wanaona ni salama kufanya ngono bila kinga kwa maana kipomo kinasoma negative.

Ukweli ni kwamba kipimo kusoma negative haimaanishi kwamba hauwezi kuambukizwa VVU/HIV.

Ukiwa na uelewa wa vitu hivi viwili hautarudia kufanya tena hii mistake, Kitaalam kuna kitu kinaitwa WINDOW PERIOD na INCUBATION PERIOD. Tutaongelea zaidi window period maana ndo inahusika zaidi hapa.

WINDOW PERIOD ni Kipindi toka mtu ambukizwe hadi kutengenezwa kwa kingamwili dhidi ya VVU kwa kawaida huwa chini ya mwezi 1 lakini inaweza kuwa hadi miezi 3.

Hizi kingamwili(antibodies) ndo uwa zinapimwa na hivi vipimo Tajwa hapo juu mtu akiwa nazo ndo kipimo kinasoma positive yani ameathirika (Ndo maana ukienda vituo vya kutolea huduma za afya kupima afya yako unaambiwa upo okay but rudi baada ya miezi mitatu)

INCUBATION PERIOD hiki ni kipindi toka mtu apate maambukizi ya VVU hadi hatakapoanza kuonesha dalili ambayo kwa kawaida ni kuanzia mwezi mmoja mpaka zaidi ya miaka kumi (binadamu tunatofautiana)

Kwahiyo ikitokea umefanya mapenzi/ngono zembe na mtu ambaye umempima yuko negative ila yupo Window period unakuwa uko hatarini zaidi kupata HIV /VVU kwasababu huu ndo muda virusi vinakuwa vinajizalisha zaidi kwenye mwili na kingamwili bado inakuwa haijatengenezwa kupambana na hivi virusi. Let's be care!

Points to Note.
  • Kutumia vipimo vya HIV siyo namna sahihi ya kujikinga na haya maradhi.
  • Kuna uwezekano mkubwa wa kupata HIV hata kama mwenzi wako umempima na ukakuta yuko Negative
  • Matumizi ya kondomu yatabaki kuwa kinara wa kujikinga na HIV pamoja na magonjwa mengine ya zinaa.
UKIMWI UPO NA UNAUA TUJIKINGE
Kama una swali karibu.
Asante Sana Mkuu. Na ELISA test nayo vipi katika kutambua nirusi kabla ya dalili au window period? Maana mtaani ndiko wanasema kiko effective zaidi. Elimu hapa mkuu.
 
Asante Sana Mkuu. Na ELISA test nayo vipi katika kutambua nirusi kabla ya dalili au window period? Maana mtaani ndiko wanasema kiko effective zaidi.
Yes ,ELISA inauwezo wa kumtambua hata kama yuko window period.
But this is not routinely done na hospital zinazofanya hicho kipimo Tanzania zinaweza zisifike Kumi.
 
S
Yes ,ELISA inauwezo wa kumtambua hata kama yuko window period.
But this is not routinely done na hospital zinazofanya hicho kipimo Tanzania zinaweza zisifike Kumi.
Shukrani Sana mkuu. Nafikiri ELISA test Kwa watu ambao Wana Nia ya kuanza serious relationship ni vyema waifanye hii maana itafika mahali condom wataweka pembeni. Wale walabuaji hovyohovyo ndiyo hizo temporary tests ambazo hazionesh waathirika window period na pia test hizi lazima ndom ichukue nafasi yake.
 
Mkuu na vipi kuhusu hawa Carrier ambaye anaweza kaa zaidi ya miaka hata 7 na wakimpima haoneshi kama ana HIV..!?
Anakua na virus lakin azalish antibody za ukimwi ndio maana vikipimwa havionekan kinachopimwa na vipimo sio ukimw bali ni antibdoy ambazo huzalishwa na kuonekana baada ya week mbili mpaka sita
 
Back
Top Bottom