Je, Wajua Senegal ilishapoteza Fainali 2 za AFCON kabla ya kuibuka kidedea dhidi ya Watoto wa Farao?

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275
Timu ya taifa ya Senegal ndio mabingwa wa mwaka huu wa mashindano ya mataifa ya Afrika (AFCON) baada ya kuilaza Misri katika mechi ya fainali iliyoandaliwa katika uwanja wa Olembe katika jiji kuu la Cameroon, Yaounde.

Misri sasa imeshiriki mashindano ya AFCON mara 25 hii ikiwa ni rekodi ya bara Afrika na kuingia fainali mara 10.

Kati ya hizo kumi, watoto wa Farao, wameshinda saba kati yazo, miongoni mwazo tatu mfululizo; mwaka 2006, 2008 na 2010.

Senegal imefuzu kwa mashindano ya AFCON mara 15 na kuingia fainali mara tatu, ikipoteza za kwanza mbili; mwaka 2002 na 2019.

Hili ndilo taji la kwanza kwa Senegal, ambalo wachezaji wa timu hiyo walitaka sana kulishinda wakisema kuwa litampunguzia shinikizo kocha wao Aliou Cisse.

Kwa mujibu wa Mane, Cisse ndiye kocha anayekashifiwa zaidi katika soka duniani licha ya kujitoa mhanga kwa nchi yake.

Cisse alikuwa nahodha wa kikosi cha Senegal kilichpoteza fainali ya 2002 dhidi ya Cameroon na alikuwa mmoja wa wachezaji waliopoteza penalti katika fainali hiyo na 2019 alikuwa kocha wa kikosi hicho kikipigwa na Algeria jijini Cairo nchini Misri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom