Je, wajua njia bora ya ufundishaji hesabu kwa hapa bongo?

victor lenard

Member
May 14, 2017
10
3
2e39d45641d3d6dd3674d7c0f27ba535.jpg
somo la hesabu limekua chukizo Kwa wanafunzi wengi dunia nzima, hali hii huwapa ugumu walimu WA somo hili kwakua wanafunzi hulichukia sana. Mwalimu Mmoja huko afrika ya kusini ameamua kutumia njia mbadala kuwafundisha wanafunzi wake somo hili. Mwalimu huyu ameamua kuandika formulae za hesabu kwa mfumo WA nyimbo za hiphop na nyimbo hizo huchukua sekunde 60 hivyo yeye huchukua nyimbo hizo na kuziweka kwenye laptop yake na pindi afikapo darasani huanza kuwaimbia wanafunzi wake. aliongeza kuwa hua anaruhusu kucheza pia ili kuongeza umakini darasani. Anasema Mwalimu Kurt kwamba juhudi zake zimeonesha matokeo chanya sana maana wanafunzi asilimia 100 Wanafaulu na wote hufika darasani tofauti na hapo awali
9dfc7e37cf7d704469fe39e5439b771a.jpg
njia hii inaweza kutumika hata hapa kwetu Tanzania kutokana na wanafunzi wengi kuwa wapenz WA muziki na kushika sana mistari ya sanaa hii ambayo pia ni burudani kwao
 
He he hee hongera zake uyo mwalimu kwa kuwa na kipaji na kuwa tayari kukitumia kwenye kaz yake.Swali je wasio na vipaji hivyo wafanyeje? Na vipi kuhusu maadili ya taaluma husika?
 
Eeeh hongera zake kama wameonyesha kuelewa..... Sisi mwalimu wetu alituruhusu tuingie mpaka na vibomu na bado ikashindikana
 
Back
Top Bottom