Je, wajua miti ni sumaku inayovuta nguvu za kiroho? Panda miti nyumbani kwako

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,339
51,884
Anaandika, Robert Heriel
Kuhani katika Hekalu Jeusi.

Andiko hili lamfaa kila mtu. Lugha iliyotumika ni laini. Sio Kali kama nilivyozoea Kwa mada zangu nyingi.

Kisayansi Miti ni moja ya viumbe hai muhimu katika Ecosystem (kutegemeana Kwa viumbe hai n mfu ili kufanya Maisha yaendelee katika uzuri).

Wengi tunajua faida za Miti iwe Kwa kusoma shuleni au Kwa utashi wetu. Tunafahamu Miti ni chanzo kizuri cha Hewa Safi ya Oksijeni pamoja na ku-regulate Jotoridi. Miti hutupatia Vivuli, hutupatia chakula, n.k.

Lakini leo Taikon atajikita zaidi katika mambo ya Kiroho, Miti ni sumaku inayovuta NGUVU za Kiroho. Hapa nitaomba utulivu wako. Nami Taikon nitajitahidi kadiri ya uwevyo niliojaliwa kuelezea ili uelewe.

Yapo mambo kadhaa Duniani yanayovuta Nguvu za Kiroho, mambo hayo ni kama ifuavyo;
1. Maji
2. Damu
3. Miti
4. Moto n.k.

Mambo hayo kwa kiasi kikubwa hushirikiana. Mfano, ndani ya damu kuna maji na Hewa. Ndani ya maji kuna Hewa. Ili Moto uwake lazima kuwe na hewa inayowaka na inayochochea Moto kuwaka.

Miti ni moja ya sehemu ya vyanzo vya hewa. Bado hujajua nazungumzia jambo gani? Hapa nazungumzia, roho kama nishati ya uhai na Roho kama Nafsi.

Mjadala wetu leo utajikita katika MITI kama Sumaku ya Kiroho.

Kila mti uuonao ni sumaku ya kuvuta Roho Fulani. Unaweza kuwa Roho NJEMA, ya bahati, ya baraka au neema, na pia unaweza kuwa ni SUMAKU ya kuvuta roho mbaya, ya mikosi, laana, na uharibifu.

Mungu alipoumba ulimwengu, moja ya viumbe walioachiwa Roho au Nguvu na uwezo wa kuvuta Roho ni Miti au mimea.

i) Ipo Miti imepewa uwezo wa kuvuta Roho ya uponyaji wa magonjwa ya Mwili, Akili, Roho na hisia.

ii) Ipo Miti imepewa uwezo wa kuvuta bahati.

iii) Ipo Miti imepewa uwezo wa kuvuta Roho ya burudani na ulevi.

iv) Ipo Miti imepewa uwezo wa kuvuta Shibe kuridhika, unaweza ukala ukashiba lakini usitosheke yaani bado ukahisi njaa.

v) Ipo miti imepewa uwezo wa kuvuta Mikosi, na majanga.

vi) Ipo Miti imepewa uwezo ivute Mauti, ukila majani au matunda, au mizizi au magome yake unakufa.

VIi) Ipo miti ambayo imepewa uwezo wa kuvuta Roho ya kuzaa Sana au Utasa.

Yaani ukila mti huo iwe ni majani au matunda, au mizizi au chochote kile katika mti huo basi Roho ya Utasa inakuvaa.

Zingatia kinachoua au kudhuru sio mti bali ile roho iliyowekwa kwenye mti au Roho itakayovutwa na huo Mti.

Ni muhimu kupanda miti katika nyumba yako kulingana na maisha unayoyahitaji. Watu wote wanaopanda miti wanajua kile wakifanyacho, ukienda kwenye mataifa yaliyoendelea au watu fulani wenye maisha mulani ya akili moja ya vitu ambavyo nitakuomba uchunguze ni pamoja na miti iliyopo katika eneo la nyumba zao.

Fuatilia ipo miti mingapi, ipo miti ya aina gani, pamoja na mimea kwa ujumla iwe ni maua au ukoka.

Moja ya makosa makubwa ambayo tunayafanya ni kukata miti maeneo ambayo tunaishi. Hilo ni kosa kubwa ambalo wengi hatulijui.

Unapopanda miti inamaanisha kuwa unaweka antenna au sumaku ya kukamata mawimbi ya Roho zinazoranda randa angani. Miti huvuta Roho zenye Uhai. Wajanja zaidi huweka mazingira yao kwa kuweka mabwawa ya maji ambayo yatazidisha usumaku wa kuvuta roho wanazozihitaji. Hii ni mada nyingine.

Watu waishio kwenye miti mingi ni rahisi kufanikiwa zaidi kuliko Watu waishio kwenye majangwa.

MTU yeyote mwenye akili afikapo eneo lenye ujangwa jambo la kwanza ni kupanda miti ili kulipa eneo lile Uhai. Kisha mengine yafuate.

Lakini MTU mjinga na mpumbavu akifika eneo lenye miti, badala aipangilie miti Ile ili ikae vizuri ndipo aanzishe makazi yake, yeye huikata Kwanza na bahati mbaya zaidi hapandi tena.

Biblia inasema,
Mwanzo 2:17
[17]walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.

Kwa kipindi kabla ya Adamu hajaasi, mti mmoja tuu ndio ulikuwa umepewa Code, antenna au usumaku wa kuvuta Mauti. Yaani utakapokula matunda yake basi umekivuta Kifo. Yaani ume-pair device kupitia mti kukivuta Kifo.

Waamuzi 9:8 – 13. Biblia inasema hivi:-

“8. Siku moja miti ilitoka ili kuutia mmoja mafuta uwe mfalme juu yao; ikauambia mti mzeituni, Tawala wewe juu yetu. 9. Lakini huo mzeituni ukaiambia, Je! Niache mafuta yangu, ambayo kwangu mimi watu wamheshimu Mungu na wanadamu, ili niende nikayonge-yonge juu ya miti? 10. Kisha miti ikauambia mtini, Njoo wewe, utawale juu yetu. 11. Lakini huo mtini ukaiambia, Je! Niuache utamu wangu, na matunda yangu mazuri, niende nikayonge-yonge juu ya miti? 12. Kisha miti ikauambia mzabibu, Njoo wewe, utawale juu yetu. 13. Huo mzabibu nao ukaiambia, Je! Niiache divai yangu, ambayo humfurahisha Mungu na wanadamu, ili niende nikayonge-yonge juu ya miti?”
[14]Ndipo hiyo miti yote ikauambia mti wa miiba, Njoo wewe, utawale juu yetu.
[15]Huo mti wa miiba ukaiambia miti, Kwamba ninyi mwanitia mafuta niwe mfalme juu yenu kwelikweli, basi njoni mtumaini kivuli changu; na kwamba sivyo, na utoke moto katika mti wa miiba na kuiteketeza mierezi ya Lebanoni."


Aya hizi zinaeleza jinsi miti ilivyo na kazi muhimu Kwa Mungu na Kwa Binadamu. Ipo miti kazi yake ni kutoa Mafuta kwaajili ya kuvuta Roho ya ulaini, urembo, mvuto n.k kama unavyosikia Mzeituni akijieleza. Hakuna Shaka Mafuta ya Mzeituni yanafahamika kwa kazi zake.

Unamsikia Mzabibu naye akitamba kuwa yeye hatoweza mambo ya ufalme ila kazi yake ni kutoa burudani na kuvuta Roho ya furaha kupitia kilevi kitakachotoka kwake. Wanywaji wa pombe wanajua jinsi pombe ilivyo na jinsi wanavyojisikia.

Mtini unajieleza kuwa upo kwaajili ya kuvuta utamu na uzuri Kwa Binadamu. Wakati Mti wa miiba kazi yake ni kutoa kivuli tuu lakini unavuta Roho za kuchomwa, roho za maumivu, mateso n.k.

Nataka kusema nini,
Madaktari wote Duniani hutumia miti kutibu Watu, na miti hiyo ndio huvuta Roho za uponyaji.
Daktari Hana uwezo wa kumponyesha MTU lakini Dawa atakazokupa ambazo asilimia 90% zinatoka kwenye mimea ndio huvuta Roho za kukuponya zidi ya magonjwa uliyonayo.

Kupanda miti nyumbani kwako,
I) kutavuta Roho za Uponyaji
ii) kutavuta Roho za bahati
iii) kutavuta Roho za Mvuto sio ajabu ndege, wadudu kama vipepeo wakija nyumbani kwako, huo ni mvuto wa asili.

Wewe kama nyumba yako haitembelewi hata na ndege au wadudu unategemea upate wapi Mvuto?

Miti inaongeza uzuri wa hapo nyumbani na kufanya nyumba yako ivutie.

iv) Kuvuta Roho ya Utulivu. Miti inavuta Roho ya Amani na Utulivu. Akili inakuwa ime-relax na unakuwa mzuri katika kutafakari.

v) Unafukuza Roho ya Njaa na Mabalaa .Miti inakawaida ya kufukuza Roho chafu lakini miti hiyo Sharti iwekwe katika hali ya usafi na mpangilio.

Falme za Kiroho hutumia miti kama vituo vyao vya mapumziko, Pia hutumia kama sehemu ya kuvuta baraka kama Mvua n.k.

Utakapoenda Kwa Waganga wa kienyeji, kitu cha Kwanza watakachokifanya ni kuangalia tatizo lako limetokana na Miti gani, yaani umepata janga hilo kutokana na miti gani?
Alafu ndio watumie miti itakayokutibu au kuvuta Majini au viumbe wa Kiroho.
Zingatia Miti, maji na Damu ni SUMAKU muhimu ya kuvuta Roho.

Mungu mwenyeenzi anatutaka tuyatawala mazingira yetu, agizo NI lilelile, tulime na kutunza Bistani tulizopewa na Mungu. Na huwezi iita Bustani kama haina miti na mimea mingine. Falsafa hiyo ni muhimu na nyeti Sana.
Lazima tujue kipi tule na kipi tusile, mti upi upandwe nyumbani na upi usipandwe.
Lazima tujue ni Kwa nini kuna miti ya porini na miti ya nyumbani?

Nipumzike SASA.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Barikiwa sana..miti ni uhai.

Nyumba iliyozungukwa na miti huwa ina hewa safi pia hakuna joto(wakazi wa dsm hapa tunaelewana nadhani)jua na joto la manzese sio sawa na jua na joto la masaki.

#MaendeleoHayanaChama
 
Barikiwa sana..miti ni uhai.

Nyumba iliyozungukwa na miti huwa ina hewa safi pia hakuna joto(wakazi wa dsm hapa tunaelewana nadhani)jua na joto la manzese sio sawa na jua na joto la masaki.

#MaendeleoHayanaChama

Sisi huku Manzese chamoto tunakipata
 
Back
Top Bottom