GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Ni maneno makali sana lakini hayana tafsiri ya kufariji mtu kwa kumwambia kwa lugha ya Kiingereza au Kiswahili
Mazuzu ni watu ambao hawawezi kusimamia misimamo yao binafsi, Mazuzu mara nyingi ni watu wanaoendeshwa na watu Wengine Katika misimamo yao. Mazuzu ni watu ambao wana hofu ya kupoteza vyeo, Mali na heshima
Mazuzu wapo tayari kufanya lolote lile kumfurahisha aliyewateua
Je wajua wanaoshabikia haya yafuatayo ni Mazuzu ndani ya vyama vyetu vya siasa
1. Wanaoshangilia kupita bila kupingwa kwenye uchaguzi huku wakitambua washindwa wao wamefichwa
2. Wanaoshinda uchaguzi kwa kuiba kura bila aibu wakisali na kushukuru ushindi
3. Wanaohama vyama vya siasa kwa kufuata shibe, Pesa na teuzi
4. Wanaopindisha sheria, kanuni na taratibu za nchi ili kumfurahisha aliyewateua
5. Wanaojifanya miungu watu wakiwa madarakani kwa kutoa maneno ya vitisho, dharau na kejeli kwa wananchi
6. Wanaoondolewa kwenye nafasi zao za uteuzi ndani ya chama na kuanza kupinga mambo ya chama walichohudumu Katika nafasi za uongozi
7. Wenye tabia za kubadili kauli kama vinyonga ili kumridhisha aliyewateua
8. Wanaojiona wameyamaliza maisha na kuyapatia maisha baada ya kupata uongozi, Hakuna mwenye maisha ya raha hapa duniani kama yeye
9. Wanaojificha kwa kutumia vivuli vya dini huku wakitajataja maneno ya vitabu vya dini kila wakati na kuhitaji maombi ya viongozi wa dini kila wakati kinyume na matendo yao
10. Wanaosifia na kupamba watawala hata kwenye mambo ya hovyo ili wasikose teuzi na shibe
Ni vyema tunapojadili mada hii tusiwataje wahusika kwa maneno kuwa ni Mazuzu bali tuonyeshe kauli yake na tukio alilofanya kwenye hayo mambo kumi yanayomfanya aitwe zuzu mbele ya jamii
Mazuzu ni watu ambao hawawezi kusimamia misimamo yao binafsi, Mazuzu mara nyingi ni watu wanaoendeshwa na watu Wengine Katika misimamo yao. Mazuzu ni watu ambao wana hofu ya kupoteza vyeo, Mali na heshima
Mazuzu wapo tayari kufanya lolote lile kumfurahisha aliyewateua
Je wajua wanaoshabikia haya yafuatayo ni Mazuzu ndani ya vyama vyetu vya siasa
1. Wanaoshangilia kupita bila kupingwa kwenye uchaguzi huku wakitambua washindwa wao wamefichwa
2. Wanaoshinda uchaguzi kwa kuiba kura bila aibu wakisali na kushukuru ushindi
3. Wanaohama vyama vya siasa kwa kufuata shibe, Pesa na teuzi
4. Wanaopindisha sheria, kanuni na taratibu za nchi ili kumfurahisha aliyewateua
5. Wanaojifanya miungu watu wakiwa madarakani kwa kutoa maneno ya vitisho, dharau na kejeli kwa wananchi
6. Wanaoondolewa kwenye nafasi zao za uteuzi ndani ya chama na kuanza kupinga mambo ya chama walichohudumu Katika nafasi za uongozi
7. Wenye tabia za kubadili kauli kama vinyonga ili kumridhisha aliyewateua
8. Wanaojiona wameyamaliza maisha na kuyapatia maisha baada ya kupata uongozi, Hakuna mwenye maisha ya raha hapa duniani kama yeye
9. Wanaojificha kwa kutumia vivuli vya dini huku wakitajataja maneno ya vitabu vya dini kila wakati na kuhitaji maombi ya viongozi wa dini kila wakati kinyume na matendo yao
10. Wanaosifia na kupamba watawala hata kwenye mambo ya hovyo ili wasikose teuzi na shibe
Ni vyema tunapojadili mada hii tusiwataje wahusika kwa maneno kuwa ni Mazuzu bali tuonyeshe kauli yake na tukio alilofanya kwenye hayo mambo kumi yanayomfanya aitwe zuzu mbele ya jamii