Maneno "a" pamoja na "the" ni kifungu cha mameno ambayo huwa yanatumika kama utambulisho wa nomino katika lugha ya kiingereza .utofauti wa haya maneno mawili ni:-
"A" hutumika kutambulisha nomino ambayo haina umbo maalum.kwa mfano:- tuchukue nomino ambayo haina umbo maalum kama "maji" basi sentensi itakuwa, "this is a water from indian ocean".hatuwezi kusema "this is the water from indian acean.
"THE" ni kinyume cha "A" ambapo hutumika kwa ajili ya utambulisho wa nomino ambayo ina umbo maalum hapa tutumie kitabu sentensi yetu itakuwa ni, "this is the book".hatuwezi kusema "this is a book
nafikiri nitakuwa kidogo nimetoa darasa kwa ambao walikuwa wakichanganyikiwa juu ya maneno haya mawili.
🙏👊👊👊Ulichoandika kina mashiko japo ungeweka ktk lugha yetu kwa faida ya wengine kwa sbb hapa naona kama bado unaweka chumvi kwenye kidonda boss.
Okay,huwa naangali series na zile za Philippines huwa naangalia zenye subtitles basi
Okay,
Kwa kuanza download movies na subtitles. Halafu usijiweke tuu kwenye kusoma subtitles wasikilize pia. Itakusaidia kujua namna wanavyotamka maneno.
Mpaka movie iishe unajaribu kuirudia bila subtitles utaona mabadiliko.
Jaribu movies kutoka nchi mbali mbali maana kila nchi ina accents zake. Wengine ni rahisi kusikika wengine ni ngumu.
This is a water? Hapana kamanda !!!
1. A - kama kiambishi hutumika kwa nomino zinazohesabika na kamwe haiwezi kutumika katika nomino zinazoelezea vitu visivyohesabika kama maji.
This is a water
This is water
2. A - kama kiambishi hutumika kwa nomino ili kutoa taarifa za jumla tu.
This is a book (Hiki ni kitabu)
2. The - kama kiambishi hutumika katika nomino zinazorejelewa au zinajulikana tayari. Zinaweza kuwa zinahesabika ama la!
This is the water that I drank (Haya ni maji niliyokunywa)
This is the book (Hiki ni kitabu ila kitabu hiki kinajulikana na kinakuwa kimezungumziwa au kutajwa kabla)
3. The pia hutumiwa kwenye nomino peke (mf. Jua, mwezi n.k)
The sun is extremely hot today
The clouds are covering the moon
Angalau tuanzie hapa
Hapa ndipo nilipokuwa nimesimama mwanzoLakini pia "the" huwekwa ktk nomino/jina ambalo Mimi mtamkaji na wewe msikilizaji tulifahamu au tunafahamu vizuri hicho kitu au jina lililotamkwa.Hii "a" Ni pale ambapo jina au nomino sio maalum au daaah...sijui nisemeje hapa ,kufundisha nako kazi sana Yan.
Hukuwahi kusomea Bongo mpendwa?Ila kiswahili nacho ni kigumu sana.
Zinazorejelewa, za jumla, kiambishi. ew!!!
Nimesoma, lakini wewe hauoni hivo vitu ni vigumu? Namaanisha sio kiswahili cha kawaida kinachoongelewa na kila mtu.Hukuwahi kusomea Bongo mpendwa?
Na hapo bado hatujaanza mambo ya viambishi yambwa, mofimu changamano, viambishi tamati yakinishi, ukanushi rejeshiNimesoma, lakini wewe hauoni hivo vitu ni vigumu? Namaanisha sio kiswahili cha kawaida kinachoongelewa na kila mtu.
Lala usiku umekuwa mkubwa"give me a water"
Napambana nilale .Lala usiku umekuwa mkubwa
Na hapo bado hatujaanza mambo ya viambishi yambwa, mofimu changamano, viambishi tamati yakinishi, ukanushi rejeshi
Ni sawa tu na kwenye sarufi ya Kiingereza. Mambo ya relative clauses, object markers, null traces, propositional phrases....
Kila taaluma ina kilugha chake tofauti na lugha ya kawaida ya kuzungumza mtaani. Madaktari na mainjinia wakianza lugha yao ndo kabisaaa mtu huelewi cho chote...Wanasheria hali kadhalika...
Ungekuwa na mtu wa "kupambana naye" hapo ungekuwa umechoka ushalala tayariNapambana nilale .
"Give me some water", will sound gud."give me a water"
😂😂😂😂Ungekuwa na mtu wa "kupambana naye" hapo ungekuwa umechoka ushalala tayari