Katika kile kinachoonekana kuwepo kwa ombwe kubwa la uongozi hapa nchini, hivi karibuni chama tawala CCM imemua kufanya ziara mikoani ikambatana na mawaziri wanaongoza wizara mbali mbali kwa lengo la kutoa mrejesho kwa wananchi kuhusu utendaji wa Serikali yake. Ni ukweli usiopingika kwa elimu ni nyenzi muhimu sana ya kupambana na umaskini na karibu kila kaya hapa nchini ina watoto au wajukuu wanaosoma shule; hivyo elimu kuwa kipaumbele cha kwanza kwa mzazi au kaya yeyote.
Cha kusikitisha katika mrejesho huu wa CCM suala la elimu haligusiwi kabisa kwa maana ya Mawaziri wa Elimu hawakuhusishwa katika ziara hizi. Hii ni dharua kubwa kwa mamilioni ya watanzania wanaogaragazwa na CCM katika lindi la umaskini wao wenyewe, watoto wao na wajukuu.
Haya ni matusi kwa mamilioni ya watanzania kwa kuwa wote waliopanga, wanaofanikisha na wanaopanda majukwaani katika ziara hizi zisizogusa vipaumbele vya watanzania watoto wao hawasomi Shule za Msingi ambazo wanafunzi hukaa chini, Sekondari za Kata zisizo na waalimu, maabara wala hawatibiwi katika zahanati, vituo vya afya na hospitali za Serikali zisizokuwa na vifaa vya tiba vya kutosha, dawa n.k. Hivi sasa idadi kubwa ya watoto wa Kitanzania wanamaliza darasa la saba wakiwa hawajui kusoma na kuandika. Sababu ya hali hii ni CCM na Serikali yake kutoipa kipaumbele Sekta ya Elimu kwa kuitengea fedha kidogo katika bajeti. Wakati mwaka 2008/9 Serikali ilitenga kiasi Bilioni 344 kwa ajili ya sekta ya elimu, kiwango kimekuwa kikipungua kila mwaka. Mathalani, mwaka 2009/10 ilitenga Bilioni 302 tu, na 2010/11 imetenga Bilioni 238 tu.
Wakati hali ikiwa hivyo katika sekta ya elimu, CCM na Serikali yake waliojigamba hivi karibuni katika Mkutano Mkuu wa CCM wa 8 mjini Dodoma kuwa wanaweza kutoa elimu bure hadi ngazi ya Sekondari katika bajeti ya 2012/13 wametenga Bilioni 193.86 tu kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo katika sekta ya Elimu (sawa na 8.5% ya bajeti nzima Sekta ya Elimu) ikiwa ni pungufu kwa Bilioni 2.39 ya bajeti ya mwaka jana. Bajeti ya maendeleo ndio hutumika kujenga au kukarabati madarasa, kununua au kutengeneza madawati n.k.
Wakati CCM na Serikali yake ikitenga 8-9% ya bajeti ya Elimu kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo katika sekta ya Elimu, nchi jirani ya Uganda imekuwa ikitenga kati ya 20-24 ya bajeti ya Elimu kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo ya katika sekta ya Elimu. Huku Kenya ikitenga kati ya 14-15 ya bajeti ya Elimu kwa ajili ya miradi ya Maendelo katika sekta ya Elimu. (PER, 2011, Kenya), (Madina et al, 2011). Hivyo haishangazi kukuta watoto wa kitanzania katika nchi iliyosheheni raslimali lukuki wakijazana kati ya 65 -73 katika darasa moja, wakikaa chini kwa ukosefu wa madawati wengine wakisomea katika mabvu za mbwa, chini ya mti n.k. CCM na Serikali yake pia wametenga Bilioni 2089.14 kwa ajili ya matumizi ya kawaida (sawa na 91.5% ya bajeti nzima ya Sekta ya Elimu) ikwa ni ongezeko la Bilioni 240.39 ya bajeti ya mwaka jana. Fungu hili la Matumizi ya Kawaida pamoja na kutumika kulipa mishahara ya watumishi, kiasi kikubwa sana cha fedha zinzotengwa katika fungu hili hutumiwa vibaya katika matumizi mbali mbali ya ovyo yenye sura ya kifisadi kama vile kulipana posho za kukaa (Sitting Allowance).
Viongozi na watendaji wa juu wa Serikalini ambao kazi wanazolipiwa mishahara huhusisha kuhudhuria mikutano, akitoka ofisini kwake na kuhudhuria kikao ofisi ya pili hulipwa posho ya kati Shs 100,000/= hadi 1,000,000/= kulingana na cheo cha mtumishi, kwa mikutano ya masaa machache katika siku; na pengine huhudhuria vikao viwili na hata vitatu kwa siku na huko kote hujichotea posho na mwisho wa mwezi mshahara wake upo pale pale ukiambatana na posho zingine lukuki kama vile kulipiwa maji, umeme, nyumba n.k.
Matumizi mengine ya ovyo kabisa yenye sura za kifisadi ni safari zisizoisha na zisizo na tija ambazo hufanywa na mawaziri na viongozi wengine wa Serikali. Mathalani mawaziri wakitembelea majimbo yao hutumia magari ya Serikali na hulipwa posho wao wenyewe na madereva wao pamoja na magari kujazwa mafuta kwa gharama za Serikali ilihali waziri huyu kama Mbunge tayari keshalipwa posho ya gari na dereva kutoka kodi za wananchi huko bungeni, Je huko kwenye majimbo yao kuna kazi gani zinazohusisha majukumu ya kiwaziri? Kama wabunge wengine wote wanatumia usafiri binafisi kuzuru majimbo yao ni kwanini mawaziri watumia kodi zetu kuzuru majimbo yao kwa gharama za Serrikali? Haishangazi kuona kila wiki mawaziri waka barabarani badala ya kufanya kazi kupambana na umaskini wan chi na kutatua kero za wananchi.
Katika mlolongo huo wa matumizi ya kifisadi ya CCM na Serikali yake Maafisa waandamzi Serikalini huzua safari za mikoani na hata nje ya nchi kwa ajili kuhudhuria mikutano, semina, warsha, makongamano n.k na kujichotea mamilioni ya Dola na Shilingi za Kitanzania kwa njia ya posho, tiketi za ndege hulipiwa, magari ya Serikali yanayotumika hujazwa mafuta, madereva na wasaidizi kulazimika kulipwa posho na malipo mengine kwa safari hizi zisizo na tija. Matumizi yote haya yasiyo ya lazima ndio hupelekea Serikali kushindwa kuwapatia wananchi huduma za jamii za kiwango cha kuridhisha.
Katika bajeti ya 2012/13, Wizara ya Elimu inatazamiwa kutumia Bilioni 320.4 kwa ajili ya matumizi ya kawaida huku kiwango kikubwa kikienda katika matumizi ya kifisadi yaliyotajwa hapo juu. Kiwango hiki ni zaidi ya bajeti ya Maendeleo ya Sekta ya Elimu kwa Bilioni 120.4. Wakati matumizi yasiyo ya lazima yakitengewa fedha nyingi kiasi hiki CCM na Serikali yake wanashindwa kutekeleza kwa vitendo ahadi waliyojiwekea wenyewe toka mwaka 2002 ya kumpelekea kila mtoto aliyeko Shule ya Msingi Shs 10,000/= tu kwa mwaka kwa ajili ya Shule kununulia vitabu, vifaa vya kufundishia, kukarabati majengo na kununua madawati na kuchapa mitihani.
Tanzania inakadiriwa kuwa wanafunzi Milioni 10 katika Shule za Msingi. Kama kila mwanafunzi atatumiwa Shs 10,000/= tu (japo kiwango hiki ni cha 2002, ili mtoto aweze kusoma vizuri hakitoshi) zinahitaji Shs Bilioni 100 tu. Hii ni sawa na 31% tu ya Bilioni 320.4 zilizotengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya Wizara ya Elimu. Utafiti unaonyesha kuwa licha ya CCM na Serikali yake kutenga fedha nyinga kwa ajili ya posho, safari, mafuita na matumizi mengine yasiyo na tija, Shule za Msingi nyingi jijini Dar es Salaam mwaka 2010 zilitumiwa wastani wa Shs 4,000/= tu kwa kila mwanafunzi; huku kwa shule za mikoani kiwango hiki kikifikia pungufu ya Shs 1,000/= kwa kila mwanafunzi. Waalimu wamekuwa hawalipwi malimbikizo ya mishahara, malipo ya likizo, fedha za uhamisho posho mbali mbali wanozostahili kisheria.
Laiti kama CCM na Serikali yake wangekuwa na mapenzi ya dhati kwa maskini wa nchi hii upo uwezekano wa kupunguza matumizi yasio ya lazima kama vile posho za kukaa, safari zisizo na tija, matuimizi ya mafuta, vitafunwa n.k na hivyo kuokoa 20% ya kiasi kilichotengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida katika Wizara ya Elimu, hivyo kiasi cha Bilioni 64 kinaweza kuokolewa. Kiasi hiki kinaweza kujenga maabara 1,280 kwa ajili ya Shule zetu za sekondari kwa gharama ya Shs Milioni 50 kila moja.
Kama katika bajeti ya Sekta ya Elimu waalimu nao wangekuwa wanatengewa posho hizi hali ingekuwaje katika ari ya ufundishaji? Kuna mtoto wa Mtanzania angemaliza darasa la saba bila ya kujua kusoma na kuandika? Kama kweli CCM inawapenda watanzania ni kwanini iendelee kuwarundikia mishahara minono na posho lukuki kundi dogo la viongozi wa serikali badala ya fedha hizo kutumika kupandisha mishahara ya waalimu ili waongeze ari ya kufundisha watoto wa kitanzania maskini?
Matokeo yake CCM na Serikali yake wanawaacha wazazi kurundikiwa michango lukuki kama vile kulipa mlinzi, madawati, ukarabati wa madarasa, kuchapa mitihani n.k na shule zetu za msingi zikiwa hazina madarasa ya kutosha, hazina madawati, hakuna vitabu na vifa vya kufundishia, hakuna vyoo, hakuna maji mashuleni, waalimu wankaa chni ya miti kusahihisha mazoezi ya wanafunzi kwa ukosefu wa ofisi na samani, wanafunzi wanrundikwa kati ya 65-73 kwa darasa moja, watoto wa kitanznia wankaa chini, mwalimu mmoja kwa wanafunzi 55 na mapungufu mengine lukuki. Hii ni aibu katika nchi iliyosheheni raslimali kibao ikiwemo madini, ardhi, mito, bahari, mbuga za wanyama n.k
Cha kusikitisha katika mrejesho huu wa CCM suala la elimu haligusiwi kabisa kwa maana ya Mawaziri wa Elimu hawakuhusishwa katika ziara hizi. Hii ni dharua kubwa kwa mamilioni ya watanzania wanaogaragazwa na CCM katika lindi la umaskini wao wenyewe, watoto wao na wajukuu.
Haya ni matusi kwa mamilioni ya watanzania kwa kuwa wote waliopanga, wanaofanikisha na wanaopanda majukwaani katika ziara hizi zisizogusa vipaumbele vya watanzania watoto wao hawasomi Shule za Msingi ambazo wanafunzi hukaa chini, Sekondari za Kata zisizo na waalimu, maabara wala hawatibiwi katika zahanati, vituo vya afya na hospitali za Serikali zisizokuwa na vifaa vya tiba vya kutosha, dawa n.k. Hivi sasa idadi kubwa ya watoto wa Kitanzania wanamaliza darasa la saba wakiwa hawajui kusoma na kuandika. Sababu ya hali hii ni CCM na Serikali yake kutoipa kipaumbele Sekta ya Elimu kwa kuitengea fedha kidogo katika bajeti. Wakati mwaka 2008/9 Serikali ilitenga kiasi Bilioni 344 kwa ajili ya sekta ya elimu, kiwango kimekuwa kikipungua kila mwaka. Mathalani, mwaka 2009/10 ilitenga Bilioni 302 tu, na 2010/11 imetenga Bilioni 238 tu.
Wakati hali ikiwa hivyo katika sekta ya elimu, CCM na Serikali yake waliojigamba hivi karibuni katika Mkutano Mkuu wa CCM wa 8 mjini Dodoma kuwa wanaweza kutoa elimu bure hadi ngazi ya Sekondari katika bajeti ya 2012/13 wametenga Bilioni 193.86 tu kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo katika sekta ya Elimu (sawa na 8.5% ya bajeti nzima Sekta ya Elimu) ikiwa ni pungufu kwa Bilioni 2.39 ya bajeti ya mwaka jana. Bajeti ya maendeleo ndio hutumika kujenga au kukarabati madarasa, kununua au kutengeneza madawati n.k.
Wakati CCM na Serikali yake ikitenga 8-9% ya bajeti ya Elimu kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo katika sekta ya Elimu, nchi jirani ya Uganda imekuwa ikitenga kati ya 20-24 ya bajeti ya Elimu kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo ya katika sekta ya Elimu. Huku Kenya ikitenga kati ya 14-15 ya bajeti ya Elimu kwa ajili ya miradi ya Maendelo katika sekta ya Elimu. (PER, 2011, Kenya), (Madina et al, 2011). Hivyo haishangazi kukuta watoto wa kitanzania katika nchi iliyosheheni raslimali lukuki wakijazana kati ya 65 -73 katika darasa moja, wakikaa chini kwa ukosefu wa madawati wengine wakisomea katika mabvu za mbwa, chini ya mti n.k. CCM na Serikali yake pia wametenga Bilioni 2089.14 kwa ajili ya matumizi ya kawaida (sawa na 91.5% ya bajeti nzima ya Sekta ya Elimu) ikwa ni ongezeko la Bilioni 240.39 ya bajeti ya mwaka jana. Fungu hili la Matumizi ya Kawaida pamoja na kutumika kulipa mishahara ya watumishi, kiasi kikubwa sana cha fedha zinzotengwa katika fungu hili hutumiwa vibaya katika matumizi mbali mbali ya ovyo yenye sura ya kifisadi kama vile kulipana posho za kukaa (Sitting Allowance).
Viongozi na watendaji wa juu wa Serikalini ambao kazi wanazolipiwa mishahara huhusisha kuhudhuria mikutano, akitoka ofisini kwake na kuhudhuria kikao ofisi ya pili hulipwa posho ya kati Shs 100,000/= hadi 1,000,000/= kulingana na cheo cha mtumishi, kwa mikutano ya masaa machache katika siku; na pengine huhudhuria vikao viwili na hata vitatu kwa siku na huko kote hujichotea posho na mwisho wa mwezi mshahara wake upo pale pale ukiambatana na posho zingine lukuki kama vile kulipiwa maji, umeme, nyumba n.k.
Matumizi mengine ya ovyo kabisa yenye sura za kifisadi ni safari zisizoisha na zisizo na tija ambazo hufanywa na mawaziri na viongozi wengine wa Serikali. Mathalani mawaziri wakitembelea majimbo yao hutumia magari ya Serikali na hulipwa posho wao wenyewe na madereva wao pamoja na magari kujazwa mafuta kwa gharama za Serikali ilihali waziri huyu kama Mbunge tayari keshalipwa posho ya gari na dereva kutoka kodi za wananchi huko bungeni, Je huko kwenye majimbo yao kuna kazi gani zinazohusisha majukumu ya kiwaziri? Kama wabunge wengine wote wanatumia usafiri binafisi kuzuru majimbo yao ni kwanini mawaziri watumia kodi zetu kuzuru majimbo yao kwa gharama za Serrikali? Haishangazi kuona kila wiki mawaziri waka barabarani badala ya kufanya kazi kupambana na umaskini wan chi na kutatua kero za wananchi.
Katika mlolongo huo wa matumizi ya kifisadi ya CCM na Serikali yake Maafisa waandamzi Serikalini huzua safari za mikoani na hata nje ya nchi kwa ajili kuhudhuria mikutano, semina, warsha, makongamano n.k na kujichotea mamilioni ya Dola na Shilingi za Kitanzania kwa njia ya posho, tiketi za ndege hulipiwa, magari ya Serikali yanayotumika hujazwa mafuta, madereva na wasaidizi kulazimika kulipwa posho na malipo mengine kwa safari hizi zisizo na tija. Matumizi yote haya yasiyo ya lazima ndio hupelekea Serikali kushindwa kuwapatia wananchi huduma za jamii za kiwango cha kuridhisha.
Katika bajeti ya 2012/13, Wizara ya Elimu inatazamiwa kutumia Bilioni 320.4 kwa ajili ya matumizi ya kawaida huku kiwango kikubwa kikienda katika matumizi ya kifisadi yaliyotajwa hapo juu. Kiwango hiki ni zaidi ya bajeti ya Maendeleo ya Sekta ya Elimu kwa Bilioni 120.4. Wakati matumizi yasiyo ya lazima yakitengewa fedha nyingi kiasi hiki CCM na Serikali yake wanashindwa kutekeleza kwa vitendo ahadi waliyojiwekea wenyewe toka mwaka 2002 ya kumpelekea kila mtoto aliyeko Shule ya Msingi Shs 10,000/= tu kwa mwaka kwa ajili ya Shule kununulia vitabu, vifaa vya kufundishia, kukarabati majengo na kununua madawati na kuchapa mitihani.
Tanzania inakadiriwa kuwa wanafunzi Milioni 10 katika Shule za Msingi. Kama kila mwanafunzi atatumiwa Shs 10,000/= tu (japo kiwango hiki ni cha 2002, ili mtoto aweze kusoma vizuri hakitoshi) zinahitaji Shs Bilioni 100 tu. Hii ni sawa na 31% tu ya Bilioni 320.4 zilizotengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya Wizara ya Elimu. Utafiti unaonyesha kuwa licha ya CCM na Serikali yake kutenga fedha nyinga kwa ajili ya posho, safari, mafuita na matumizi mengine yasiyo na tija, Shule za Msingi nyingi jijini Dar es Salaam mwaka 2010 zilitumiwa wastani wa Shs 4,000/= tu kwa kila mwanafunzi; huku kwa shule za mikoani kiwango hiki kikifikia pungufu ya Shs 1,000/= kwa kila mwanafunzi. Waalimu wamekuwa hawalipwi malimbikizo ya mishahara, malipo ya likizo, fedha za uhamisho posho mbali mbali wanozostahili kisheria.
Laiti kama CCM na Serikali yake wangekuwa na mapenzi ya dhati kwa maskini wa nchi hii upo uwezekano wa kupunguza matumizi yasio ya lazima kama vile posho za kukaa, safari zisizo na tija, matuimizi ya mafuta, vitafunwa n.k na hivyo kuokoa 20% ya kiasi kilichotengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida katika Wizara ya Elimu, hivyo kiasi cha Bilioni 64 kinaweza kuokolewa. Kiasi hiki kinaweza kujenga maabara 1,280 kwa ajili ya Shule zetu za sekondari kwa gharama ya Shs Milioni 50 kila moja.
Kama katika bajeti ya Sekta ya Elimu waalimu nao wangekuwa wanatengewa posho hizi hali ingekuwaje katika ari ya ufundishaji? Kuna mtoto wa Mtanzania angemaliza darasa la saba bila ya kujua kusoma na kuandika? Kama kweli CCM inawapenda watanzania ni kwanini iendelee kuwarundikia mishahara minono na posho lukuki kundi dogo la viongozi wa serikali badala ya fedha hizo kutumika kupandisha mishahara ya waalimu ili waongeze ari ya kufundisha watoto wa kitanzania maskini?
Matokeo yake CCM na Serikali yake wanawaacha wazazi kurundikiwa michango lukuki kama vile kulipa mlinzi, madawati, ukarabati wa madarasa, kuchapa mitihani n.k na shule zetu za msingi zikiwa hazina madarasa ya kutosha, hazina madawati, hakuna vitabu na vifa vya kufundishia, hakuna vyoo, hakuna maji mashuleni, waalimu wankaa chni ya miti kusahihisha mazoezi ya wanafunzi kwa ukosefu wa ofisi na samani, wanafunzi wanrundikwa kati ya 65-73 kwa darasa moja, watoto wa kitanznia wankaa chini, mwalimu mmoja kwa wanafunzi 55 na mapungufu mengine lukuki. Hii ni aibu katika nchi iliyosheheni raslimali kibao ikiwemo madini, ardhi, mito, bahari, mbuga za wanyama n.k