Je wajua kwamba - Serikali ya Muungano haisaidii ruzuku kwa SMS kujiendesha?

Teamo

JF-Expert Member
Jan 9, 2009
12,272
1,034
''..kwa mujibu wa hoja iliyotolewa kwenye bunge la baraza la wawakilishi leo na waziri husika,ni kwamba serikali ya muungano haitoi msaada wowote wa ruzuku ili kuisaidia SMZ kujiendesha...''ITAENDELEA!

wewe jiulize tu kama 'madai ya wazanzibari ' kuhusu marekebisho ya baadhi ya vipengele vya makubaliano ya muungano ni genuine?au inakuwaje?

................stay tuned!
Nitarudi
 
Huku hawataki Muungano, huku wanataka wasaidiwe ruzuku, hawaeleweki! Wanaleta hoja ya ruzuku ili kufunika suala la mafuta na gesi asilia ambalo wanajifariji kwamba wameliondoa kwenye orodha ya mambo ya Muungano bila kufuata taratibu!
 
Huku hawataki Muungano, huku wanataka wasaidiwe ruzuku, hawaeleweki! Wanaleta hoja ya ruzuku ili kufunika suala la mafuta na gesi asilia ambalo wanajifariji kwamba wameliondoa kwenye orodha ya mambo ya Muungano bila kufuata taratibu!
Unazungumza nini Mheshimiwa? Hivi Zanzibar lini wameomba ruzuku kutoka Serikali ya Muungano. Lakini uelewe Zanzibar hawaombi, wanadai kurejeshewa kile ambacho ni haki yao. TRA inakusanya kodi Zanzibar-kodi inapelekwa wapi? Ndiyo wanaomba vitu kama hivyo virejeshwe Zanzibar. Msaada unatolewa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania -unakwenda wapi? Wanaotoa wanasema Tanzania wakijua fika kuwa na Zanzibar imo . Jee mnawapa?
 
Unazungumza nini Mheshimiwa? Hivi Zanzibar lini wameomba ruzuku kutoka Serikali ya Muungano. Lakini uelewe Zanzibar hawaombi, wanadai kurejeshewa kile ambacho ni haki yao. TRA inakusanya kodi Zanzibar-kodi inapelekwa wapi? Ndiyo wanaomba vitu kama hivyo virejeshwe Zanzibar. Msaada unatolewa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania -unakwenda wapi? Wanaotoa wanasema Tanzania wakijua fika kuwa na Zanzibar imo . Jee mnawapa?


Kwa hiyo ule magao wa 4% wanayopata kutoka hazina ya Tanzania kila mwezi ya jumla ya mapato yote haiwatoshi tu?? Zanzibar kuna watu wangapi kati Mil.35 waliopo Tanzania !!!!!!!! Watu hawazidi 1.5Mil. wanapata 4% huoni ni nyingi sana hizo mnawadhulumu watu wa Shinyanga!!!
 
Kwa hiyo ule magao wa 4% wanayopata kutoka hazina ya Tanzania kila mwezi ya jumla ya mapato yote haiwatoshi tu?? Zanzibar kuna watu wangapi kati Mil.35 waliopo Tanzania !!!!!!!! Watu hawazidi 1.5Mil. wanapata 4% huoni ni nyingi sana hizo mnawadhulumu watu wa Shinyanga!!!
Wewe!!! sisi siyo Shinyanga . Sisi ni Nchi. Hujaelewa tu? Ukipambana na vichwa ngumu wanakwambia tuwachieni tunaweza kupata zaidi ya hiyo asilimia yenu 4.
 
Wewe!!! sisi siyo Shinyanga . Sisi ni Nchi. Hujaelewa tu? Ukipambana na vichwa ngumu wanakwambia tuwachieni tunaweza kupata zaidi ya hiyo asilimia yenu 4.

Hebu angalia kwenye ramani, au google hapo ulipo kama Duniani kuna nchi inaitwa Zanzibar!!!
 
Hii ndiyo hoja inayotakiwa Wazanzibar waizungumzie...Ni haki yao kukatiwa ruzuku toka pato la Taifa kama sehemu yao halali ya muungano wa nchi mbili..
Lakini pia wakumbuke ni lazima nao watoe mchango ktk mfuko wa Taifa sii mchezo ule wa changu Changu, chako Changu!
NMi muhimu yafanyike marekebisho makubwa ktk ukusanyaji wa kodi ili ifahamike fungu la serikali mbili hizi toka ktk mfuko wa Taifa..NI LAZIMA iundwe serikali ya Bara kuwezesha zoezi hili laa sivyo tutakuwa tunajenga juu ya Kichuguu..
 
Hilo la ruzuku lipo kwenye makubaliano ya awali ya Muungano au liliwekwa 'kinyemela' kama idaiwavyo kwenye suala la mafuta na gesi asilia?
 
Fanya marekebisho ya mada hii, pls! SMZ badala ya SMS! Usiwape nafasi watu kuanza kujadili title wakaacha hoja ya msingi!
 
Unazungumza nini Mheshimiwa? Hivi Zanzibar lini wameomba ruzuku kutoka Serikali ya Muungano. Lakini uelewe Zanzibar hawaombi, wanadai kurejeshewa kile ambacho ni haki yao. TRA inakusanya kodi Zanzibar-kodi inapelekwa wapi? Ndiyo wanaomba vitu kama hivyo virejeshwe Zanzibar. Msaada unatolewa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania -unakwenda wapi? Wanaotoa wanasema Tanzania wakijua fika kuwa na Zanzibar imo . Jee mnawapa?

Haki gani wanayodai Wazenj na kwa nani? Kila kukicha laja jipya. Ukiona hivyo kuna mawazo mufilisi.
 
Jamaa ana wake ng'ombe 99 na mimi nina ng'ombe 1 anasema tuchanganye tufanye biashara, wana JF naomba mawazo yenu.
 
..mtoa mada ana ripoti kuhusu habari niliyowawekea hapa toka Tanzania Daima.

..Zanzibar inapata misaada toka kwa Wafadhili, pamoja na gawio toka Hazina ya Muungano.

..Zanzibar ni sehemu ya Muungano. wanapotosha kwa kudai hawawakilishwi ktk mgawanyo wa mapato ya muungano.

..Zanzibar wamekuwa wakipewa umeme bure, au wakiuziwa kwa bei poa. pia serikali ya Tanganyika mara kwa mara imekuwa ikilipa mishahara ya watumishi wa SMZ. kwa mtizamo wangu hiyo ni RUZUKU.

Saleh Mohamed said:
Katika hatua nyingine, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, imesema haipokei msaada wa kibajeti kutoka kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa ajili ya utekelezaji wa mipango yake ya maendeleo.


Hayo yameelezwa jana na Waziri wa Nchi Afisi ya Rais (Fedha na Uchumi), Dk. Mwinyihaji Makame Mwadini wakati akijibu swali la Mwakilishi wa Jimbo la Mfenesini, Ali Abdallah Ali katika kikao cha Baraza la Wawakilishi.

Waziri Mwinyihaji alisema kwamba, fedha ambazo Zanzibar imekuwa ikipokea kama msaada wa kibajeti, ni zile zinazotolewa na wahisani kupitia Serikali ya Muungano na Zanzibar kupewa gawio lake kupitia mfumo wa asilimia 4.5.

"Mheshimiwa Spika, si kweli kwamba Serikali ya Muungano husaidia bajeti ya SMZ, isipokuwa husaidia katika upatikanaji wa fedha zinazotolewa na washirika wa maendeleo, kama misaada ya kibajeti," alisema Waziri Mwinyihaji.

Mapema, mwakilishi huyo alitaka kujua iwapo ni kweli Serikali ya Jamhuri ya Muungano huipatia Zanzibar misaada kwa ajili ya bajeti yake. Waziri Mwinyihaji alisema katika kipindi cha 2001 hadi 2009, jumla ya sh 2,530,889, zilitolewa na wahisani kusaidia bajeti, ambapo Zanzibar ilinufaika na sh milioni 115,599.

Hata hivyo, alisema tume ya pamoja, tayari imekwishapitia vyanzo mbalimbali vya mapato na kutayarisha ripoti yake itakayosaidia kuwepo mfumo bora wa mgawo baina ya pande mbili za Muungano, kwa vile kiwango inachopata Zanzibar ni cha muda mrefu.

Wakati huo huo, Dk. Mwinyihaji alisema kuwa, Zanzibar imekuwa haipati gawio la kodi kutoka kwa mabenki yanayotoa huduma zake Zanzibar, kwa vile kodi hizo hulipwa makao makuu ya benki hizo Tanzania Bara.

Aliyasema hayo wakati akijibu swali la Mwakilishi, Ali Abdallah Ali wa Jimbo la Mfenesini katika kikao cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea mjini Zanzibar.
Alisema kwamba benki nyingi zinazotoa huduma Zanzibar ni matawi ukiondoa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) ambayo makao makuu yake yapo Zanzibar.

Aliyataja matawi ya benki yanayotoa huduma Zanzibar kuwa ni NBC, NMB, CRDB, Barclays, TPB, PBZ, KBC, Exim, FBME na Diamond Trust Bank, ambapo hulipa kodi serikalini pale zinapopata faida katika uendeshaji wake.

Hata hivyo, alisema ni vigumu kuweza kufahamu takwimu sahihi za viwango vya kodi vinavyolipwa na benki zinazofanya shughuli zake Zanzibar kwa vile zinaendeshwa kama matawi.

Waziri Mwinyihaji alisema mbali na Zanzibar kupoteza mapato, vile vile inakosa mapato yatokanayo na faida ya uwekezaji ambayo hupaswa kulipa mwekezaji kwa wateja wao na kodi ya ushuru wa dhamana kwa wafanyabiashara wanaoingiza bidhaa kutoka nje.
Aidha, alisema Zanzibar hupoteza kodi itokanayo na kipato cha mishahara ambayo hukata wafanyakazi wa mabenki yaliyopo Zanzibar kwa vile kodi hiyo huingizwa katika Hazina ya Muungano.
Awali, Mwakilishi Ali Abdallah Ali, alitaka kujua Zanzibar inanufaika na kiasi gani cha fedha kufuatia uwekezaji wa mabenki yanayotoa huduma zake Zanzibar.
 
Kwa hiyo ule magao wa 4% wanayopata kutoka hazina ya Tanzania kila mwezi ya jumla ya mapato yote haiwatoshi tu?? Zanzibar kuna watu wangapi kati Mil.35 waliopo Tanzania !!!!!!!! Watu hawazidi 1.5Mil. wanapata 4% huoni ni nyingi sana hizo mnawadhulumu watu wa Shinyanga!!!
Sina hakika kama unaelewa unaachokiongea, hiyo 4.5% unayosema ni kasma ya magawanyo ya misaada ya kibajeti iliyoshauriwa na wafadhili, mpaka muda huu formula ya kugawana mapato katika vyanzo vya Muungano ambayo zanzibar inachangia hakuna, tume ya pamoja ya fedha iliyoundwa imesha wasilisha ripoti yake juu ya tatizo hili, ambapo mpaka sasa katika kugawana mapato ya muungano tunatumia formula hiyohiyo ya inayotumika katikia misaada ya wafadhili kwa muda tu, mpka hapo serikali zitakapo tolea tamko ripoti ya tume ya pamoja ya fedha.
Na kuhusu hiyo habari hapo juu alichosema waziri wa fedha na uchumi zanzibar Dr. Mwinyihaji, ni kuwa SMT haitowi fungu lolote kuchangia bajeti ya zanzibar kutoka bajeti yake, sasa kuna tatizo gani wakati huo ndo ukweli? Na si kuwa wanalalamika la hasha! alipokuwa najibu swali hilo alitaka kumuhakikishia muulizaji kuwa zanzibar inaandaa bajeti yake bila ya kutegemea msaada wa Tanganyika ambao wao wenyewe hawajijuwi hawajitambui kama sisi. Bakuli mkononi kila kukicha! Ila wao ni wezi sana tu!

Hebu angalia kwenye ramani, au google hapo ulipo kama Duniani kuna nchi inaitwa Zanzibar!!!
Naona kazi pevu aliyokuwa nayo mwalimu wako wa jiografia na historia ulipokuwa shule!

Huo uchokozi .....
No si uchokozi anaonyesha kiwango chake cha uwelewa wa historia ya taifa lake na jiografia, usishangae ikawa ndo miongoni mwa hao wanapita mitihani ya shule kwa kughushi majibu kwa kununuwa mitihani. Taifa hili linafisidika kwa mengi ati mpaka thinkings za raia zake kama hawa zinapinda pinda.
 
..kulingana na kauli ya Maalim Seif waZenj wanakatiwa fungu toka serikali ya Muungano.

..tatizo ni kwamba hawakubaliani na kiwango cha mgao huo. wanataka wapewe asilimia 10% ingawa kwa idadi yao na ukubwa wa uchumi wao hawastahiki kiwango hicho.

..pia inaelekea hawachangii chochote hawa kama anavyoelekeza Maalim Seif. kama wangekuwa wanachangia hawa asingelala mtu kwa kelele zao.

..pia wakiulizwa kwanini hawatoi fungu lolote kusaidia matumizi ya taasisi za Muungano wanaanza kuleta maneno na kucheza na lugha.

..anauliza mchango wa Tanganyika uko wapi !! sasa askari, ofisi za ubalozi etc wanalipwa na nani kama siyo Tanganyika wanaotoa fedha hizo.

..tumewadekeza hawa.

..WABUNGE WA TANGANYIKA VUNJENI MUUNGANO.

Seif Sharrif Hamad said:
"Je, mtu anaposema Zanzibar haichangii gharama za uendeshaji wa vyombo na taasisi za Muungano kwa sababu tu Serikali ya Zanzibar haitoi fungu la fedha na kuliingiza katika Serikali ya Muungano, Tanganyika ambayo hata Serikali haina inachangia vipi na kiasi gani? Ikiwa mchango wake unatolewa na Serikali ya Muungano, kwani hii siyo serikali ya shirika ambapo Zanzibar ni mbia? Vipi basi Zanzibar itakiwe ichangie mara mbili kwa kutumia hadhi mbili tofauti? Na ikichangia (iwapo itachangia), ina uhakika upi kwamba itakachotoa hakitatumiwa na Serikali ya Muungano kwa shughuli za Tanganyika zisizo za Muungano ikitumia mamlaka yake kwa madhumuni hayo?

Vivyo hivyo kwa mapato yatokanayo na vyombo na taasisi za Muungano, tunajua Zanzibar inapata mgao wake na kiasi chake kimewekwa wazi (ingawa hakikubaliki kwa Wazanzibari).

Masuala yanakuja: Yale mapato yanayobaki katika Serikali ya Muungano, kuna kipi cha kuonyesha mpaka wa matumizi yake kwa Muungano na kwa shughuli za Tanganyika zisizo za Muungano? Uadilifu na uwajibikaji wa matumizi yatokanayo na mgao huu wa mapato utaonekana vipi?"
 
Sina hakika kama unaelewa unaachokiongea, hiyo 4.5% unayosema ni kasma ya magawanyo ya misaada ya kibajeti iliyoshauriwa na wafadhili, mpaka muda huu formula ya kugawana mapato katika vyanzo vya Muungano ambayo zanzibar inachangia hakuna, tume ya pamoja ya fedha iliyoundwa imesha wasilisha ripoti yake juu ya tatizo hili, ambapo mpaka sasa katika kugawana mapato ya muungano tunatumia formula hiyohiyo ya inayotumika katikia misaada ya wafadhili kwa muda tu, mpka hapo serikali zitakapo tolea tamko ripoti ya tume ya pamoja ya fedha.
Na kuhusu hiyo habari hapo juu alichosema waziri wa fedha na uchumi zanzibar Dr. Mwinyihaji, ni kuwa SMT haitowi fungu lolote kuchangia bajeti ya zanzibar kutoka bajeti yake, sasa kuna tatizo gani wakati huo ndo ukweli? Na si kuwa wanalalamika la hasha! alipokuwa najibu swali hilo alitaka kumuhakikishia muulizaji kuwa zanzibar inaandaa bajeti yake bila ya kutegemea msaada wa Tanganyika ambao wao wenyewe hawajijuwi hawajitambui kama sisi. Bakuli mkononi kila kukicha! Ila wao ni wezi sana tu!


Naona kazi pevu aliyokuwa nayo mwalimu wako wa jiografia na historia ulipokuwa shule!


No si uchokozi anaonyesha kiwango chake cha uwelewa wa historia ya taifa lake na jiografia, usishangae ikawa ndo miongoni mwa hao wanapita mitihani ya shule kwa kughushi majibu kwa kununuwa mitihani. Taifa hili linafisidika kwa mengi ati mpaka thinkings za raia zake kama hawa zinapinda pinda.

Naona una matatizo ya kuelewa wakati unasoma, Unachopinga na unachokubali ni nini sasa!!! Mara unasema hawapati chochote toka hazina zaidi ya fedha za wafadhili, mara unakubali tunagawana fedha za hazina kwa kutumia formula ya fedha za wafadhili!!!

Inaonesha ulivyona na kichwa kigumu kama kambale!, sometimes kama umeishiwa cha kuandika unaweza ukapita kwa kusoma tu bila kuchangia wala siyo kosa na hakuna atakayekuuliza, kuliko kubisha kitu na kukubali tena mwenyewe. Watu watakuona kama mwenda wazimu. Kama kweli umesoma ungekuwa umeshajigundua kosa lako!!

Nawasiwasi na elimu yako, kwani mara nyingi mtu asiyesoma hupenda kujisifu kuwa yeye ndiye, na wenyewe wenye elimu zao hata siku moja hawajitangazii.
 
ni kwamba serikali ya muungano haitoi suzuku ya SMZ KUJIENDESHA!narudia,RUZUKU KWA AJILI YA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR KUJIENDESHA!
 
ni kwamba serikali ya muungano haitoi suzuku ya SMZ KUJIENDESHA!narudia,RUZUKU KWA AJILI YA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR KUJIENDESHA!
Hili suala ni pana kabisa. SMZ ina jukumu la kuwahudumia Wazanzibari katika mambo yale ya kijamii (elimu, afya, makaazi, kilimo, uvuvi, na kadhalika). Mambo hayo niliyoyaorodhesha hapo wa-Tanzania bara (Wa-tanganyika) wanahudumiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania(ambayo ni yetu sote hata sisi kule Zenj) sasa kwa nini Serikali hiyo ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania inafumbia jicho kuwahudumia Wazanzibari katika mambo hayo -sawia na wenzao wa bara. Hapo ndio maana tunasema Bajeti ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lazima iwe na kasma ya kuhudumia Watanzania(Wazanzibari) katika hayo mambo ya elimu, afya, na mengineyo- Hiyo kasma iite kwa jina la ruzuku kama unapenda.
 
Kwa hiyo ule magao wa 4% wanayopata kutoka hazina ya Tanzania kila mwezi ya jumla ya mapato yote haiwatoshi tu?? Zanzibar kuna watu wangapi kati Mil.35 waliopo Tanzania !!!!!!!! Watu hawazidi 1.5Mil. wanapata 4% huoni ni nyingi sana hizo mnawadhulumu watu wa Shinyanga!!!

Duuu!! hizo mbona ni mgao mkubwa!! Yaani wanataka mafuta wachukue wao, ruzuku wachue 4% na TRA wasikusanye kodi. Sasa hiyo 4% itoke wapi kama mafuta ni yao, TRA hakusanyi kodi, tunalipa mshahara majeshi ya Tanzania ambayo yanalinda Zanzibar, tunalipa wabunge wao wanaowawakilisha bunge la Muungano, tunasomesha watoto wao elimu ya juu. Halafu wanachukua 4% kwa idadi ya watu sawa na Wilaya moja ya Bara. Sasa tugawe sawa mgao kulingana na idadi ya watu huone kama hakuna upendeleo kwa Wazanzibar na khali hakuna uchumi walio nao uko visiwani. Kumbuka hiyo 4% inatoka kwenye madini yetu, pamba, kahawa, korosho utalii wa mbuga zetu, uvuvi toka maziwa yetu. Mimi naona waondoke na wabaki na mafuta yao na sisi tuna gesi na mafuta hivi karibuni tutapata
 
Back
Top Bottom