Joash Sospeter
Member
- Dec 1, 2018
- 11
- 11
Ukatae ukubali lakini ukweli utabaki kuwa Ulaya ipo mbele yetu kwa zaidi ya miaka elfu moja yaani zaidi ya karne.Nasema hivi kwasababu vitu tunavyoviona kama ujanja kwetu kwao vilikuwa vya kipumbavu karne moja iliyopita.
Mwaka 1844 mwandishi wa Norway aitwaye Henrick Ibsen aliandika kitabu kiitwacho AN ENEMY OF THE PEOPLE akimtumia Dr.Stockman kama muhusika mkuu na mtu aliyeitwa adui na watawala na wakapandikiza wananchi hivyo nao wananchi kwa upumbavu wao wakaamini hivyo ilhali Dr.Stockman alikuwa akipambana kwa kila hali aliyokuwa nayo kuwatetea wananchi ikiwa ni pamoja na kujitolea kama kafara bila kujali nafasi aliyokuwa nayo akitumia muda wake mwingi kuwaambia wananchi ukweli ambao kwa watawala ilikuwa ni uadui mkubwa na uhaini.Leo tupo karne ya 21 karne mbili baada ya kuandikwa kwa hichi kitabu lakini huku kwetu yaliyozungumzwa kwenye kitabu ndo yanatokea.
Watu wanaojitoa maisha yao kusema ukweli ambao haupingwi kwa hoja bali kwa bunduki na kuwekwa rumande wanaitwa maadui wa taifa na wananchi wanapandikizwa uongo huo nao bila kutumia macho yao na kama ikishindikana basi pua zao kunusa ukweli nao wanaamini hivyo.
Naweza nikasema kuwa kwa wakati wetu kwa sasa Tundu Lissu namfananisha kama Dr.Stockman maana historia yake tangu kabla ya kuwa mbunge na baada amekuwa ni mtu anayepambana bula woga kuwaambia wananchi ukweli na kuhakikisha haki inatendeka katika taifa.
Namfananisha na Dr.Stockman tena yeye ni zaidi maana Dr. Stockman alipigwa mawe kwa anili ya ukweli lakini yeye akapigwa risasi,Dr.Stockman alifutwa kazi lakini yeye hata kabla ya kufutwa ubunge washafuta mishahara yake wakati yupo wodini akiugulia operesheni ya 23 theatre.
Kila akipata nafasi ya kusema anatoa hoja nzito ambazo zinajibiwa na maneni ya kishenzi kama ombaomba,mzururaji,wakala wa mabeberu na hata kugika kiwango kikubwa cha kumuita haini.Cha kushangaza ni kuwa wananchi hawaoni wala hawapimi hoja ili kujua uongo na ukweli uko wapi ili kusimama upande wa ukweli bali wao wamekuwa washangiliaji tu wa viongizi wa vyama vyao wakijidanganya kuwa huo ndiyo uzalendo.
Ni kweli watazidi kumbeza sana kumtukana na kumyanyasa wanavyoweza maana Dr.Stocjman naye alifanyiwa hivyo lakini wachache wenye mwanga na upeo wa kuona tutasimama naye maana siyo kwamba hata wa huko upande wa pili hawaoni wanaona sana ila uoga umewatawala maana kuna kipindi mwaka 2016 kati ya wabunge ninaowaheshimu kwa utashi wao mkubwa wa kuelewa mambo,Mh.Hussein Bashe alisema kuwa amekuwa akifatilia nyaraka za Tundu Lissu kuhusu upoteaji wa rasilimali za taifa hata kabla hajawa mbunge na akasema kuwa ni nzuri lakini anabezwa kwa kuwa ni mpinzani.
Nimalizie kwa kusema kuwa Ulaya ipo mbele yetu kwa karne zaidi ya moja maana rafiki wa wananchi leo anaitwa adui wa wananchi ila ninukuu neno la mwisho la Dr.Stockman alilosema kuwa *the strongest man in the world is the one who stands alone* kwahiyo Lissu asihofu atajiona yupo mwwnyewe lakini na sisi wapenda haki tupo nae tutasimama naye hadi mwisho na hata wengine wanaoteswa magerezani hadi kunyimwa dhamana tupo nao maana tunatambua kuwa the guilty are afraid na kwa kuwa hawana namna tena ya kuongoza kwa haki watatumia vitisho vyote maana jeshi wanalo lakini sisi tuna haki na daima Mungu yupo na wenye haki hivyo atasimama nasi.Viva Lissu the enemy of the rulers but a friend to the oppressed.
Mwaka 1844 mwandishi wa Norway aitwaye Henrick Ibsen aliandika kitabu kiitwacho AN ENEMY OF THE PEOPLE akimtumia Dr.Stockman kama muhusika mkuu na mtu aliyeitwa adui na watawala na wakapandikiza wananchi hivyo nao wananchi kwa upumbavu wao wakaamini hivyo ilhali Dr.Stockman alikuwa akipambana kwa kila hali aliyokuwa nayo kuwatetea wananchi ikiwa ni pamoja na kujitolea kama kafara bila kujali nafasi aliyokuwa nayo akitumia muda wake mwingi kuwaambia wananchi ukweli ambao kwa watawala ilikuwa ni uadui mkubwa na uhaini.Leo tupo karne ya 21 karne mbili baada ya kuandikwa kwa hichi kitabu lakini huku kwetu yaliyozungumzwa kwenye kitabu ndo yanatokea.
Watu wanaojitoa maisha yao kusema ukweli ambao haupingwi kwa hoja bali kwa bunduki na kuwekwa rumande wanaitwa maadui wa taifa na wananchi wanapandikizwa uongo huo nao bila kutumia macho yao na kama ikishindikana basi pua zao kunusa ukweli nao wanaamini hivyo.
Naweza nikasema kuwa kwa wakati wetu kwa sasa Tundu Lissu namfananisha kama Dr.Stockman maana historia yake tangu kabla ya kuwa mbunge na baada amekuwa ni mtu anayepambana bula woga kuwaambia wananchi ukweli na kuhakikisha haki inatendeka katika taifa.
Namfananisha na Dr.Stockman tena yeye ni zaidi maana Dr. Stockman alipigwa mawe kwa anili ya ukweli lakini yeye akapigwa risasi,Dr.Stockman alifutwa kazi lakini yeye hata kabla ya kufutwa ubunge washafuta mishahara yake wakati yupo wodini akiugulia operesheni ya 23 theatre.
Kila akipata nafasi ya kusema anatoa hoja nzito ambazo zinajibiwa na maneni ya kishenzi kama ombaomba,mzururaji,wakala wa mabeberu na hata kugika kiwango kikubwa cha kumuita haini.Cha kushangaza ni kuwa wananchi hawaoni wala hawapimi hoja ili kujua uongo na ukweli uko wapi ili kusimama upande wa ukweli bali wao wamekuwa washangiliaji tu wa viongizi wa vyama vyao wakijidanganya kuwa huo ndiyo uzalendo.
Ni kweli watazidi kumbeza sana kumtukana na kumyanyasa wanavyoweza maana Dr.Stocjman naye alifanyiwa hivyo lakini wachache wenye mwanga na upeo wa kuona tutasimama naye maana siyo kwamba hata wa huko upande wa pili hawaoni wanaona sana ila uoga umewatawala maana kuna kipindi mwaka 2016 kati ya wabunge ninaowaheshimu kwa utashi wao mkubwa wa kuelewa mambo,Mh.Hussein Bashe alisema kuwa amekuwa akifatilia nyaraka za Tundu Lissu kuhusu upoteaji wa rasilimali za taifa hata kabla hajawa mbunge na akasema kuwa ni nzuri lakini anabezwa kwa kuwa ni mpinzani.
Nimalizie kwa kusema kuwa Ulaya ipo mbele yetu kwa karne zaidi ya moja maana rafiki wa wananchi leo anaitwa adui wa wananchi ila ninukuu neno la mwisho la Dr.Stockman alilosema kuwa *the strongest man in the world is the one who stands alone* kwahiyo Lissu asihofu atajiona yupo mwwnyewe lakini na sisi wapenda haki tupo nae tutasimama naye hadi mwisho na hata wengine wanaoteswa magerezani hadi kunyimwa dhamana tupo nao maana tunatambua kuwa the guilty are afraid na kwa kuwa hawana namna tena ya kuongoza kwa haki watatumia vitisho vyote maana jeshi wanalo lakini sisi tuna haki na daima Mungu yupo na wenye haki hivyo atasimama nasi.Viva Lissu the enemy of the rulers but a friend to the oppressed.