Uchaguzi 2020 Je, wajua kuwa Mfumo wa Serikali ya Majimbo unatumika kwenye Nchi zenye kukosa Umoja wa Kitaifa?

Amani Msumari

JF-Expert Member
Aug 21, 2016
1,830
976
Waungwana,

Chunguzeni leo hii nchi zote ambazo ni kinara wa mfumo wa Serikali za majimbo (federal government) duniani ni nchi ambazo zilikuwa zinakabiliwa Sana na tatizo la kukosa umoja wa Kitaifa kutokana na Vita, udini au Kukosa lugha ya kuwaunganisha.

Marekani walikuwa mataifa huru 50. Kuwaunganisha ni lazima uwaachie baadhi ya madaraka yao, hivyo mfumo wa Serikali ya Majimbo ni sahihi kwao.

Canada wanashida ya lugha. Kuna majimbo hawajui au hawaongei kabisa kiingereza, wenyewe wanaongea kifaransa. Hawa ni muhimu kuwa na majimbo ili wawe huru kutumia lugha waipendayo.

Ujerumani walitawanyika na kuwa nchi mbili tofauti na ukuta ukajengwa Kati ya Ujerumani ya Mashariki na ile ya magharibi. Hawa ili kuwaunganisha mfumo wa Serikali ya Majimbo ulikuwa lazima ila maeneo hayo yabaki na sehemu ya utawala wake wa awali.

Nigeria imepitia mengi sana sana Kati ya waislamu wa kaskazini na wakristo wa kusini. Waafrika kusini vilevile wamepitia mengi Kuhusu ukoloni na ukaburu. Wazungu wengi walibaki Afrika Kusini baada ya Uhuru kamili mwaka 1994. Kwa misingi hiyo, unaweza kabisa kuona Nigeria na Afrika kusini walihitaji utawala wa majimbo.

Sisi Tanzania tunahitaji utawala wa majimbo ili iweje? Je, changamoto za kiuchumi, utamaduni na kisiasa zinatokana na mazingira hayo niliyoyataja hapo juu?

Wazungu hawana makabila na karibu wote wana dini au imani sawa. Kuwawekea utawala wa majimbo sio mbaya. Hapa kwetu tunajadili sio to dini Bali hata dhehebu. Kuna baadhi ya watu walisema katika uchaguzi wa 2015, Sasa ni zamu ya M-KKKT kuwa wa -RC wametawala Sana. Sasa kwenye nchi Kama hii uanze umajimbo, tunategemea nini kitokee?

Majimbo yatatutenga zaidi badala ya kutuleta pamoja. Mfumo wa Serikali za mitaa kwa Tanzania ni mzuri na toshelevu. Kama Kuna changamoto basi ni Kuboresha tuu.

Ninawashangaa Sana wapinzani, sijui wamekunywa wanzuki ya wapi. Tasilimali za kila eneo husaidia eneo hilo na maeneo mengine. Hii ni kwasababu watu wanaingiliana na wanaweza kuishi popote. Mtoto wa Kagera anapangiwa kazi Tanga na maisha yanaenda. Mtu wa Mtwara anahamia Mbeya anakuwa mnyaki maisha yanaenda.

Watanzania tuukumbatie umoja, amani na mshikamano wetu kwa kuchagua mafiga matatu hapo 28 Oktoba, 2020. Tuwaadhibu wapinzani wanaotaka kutugawa kwa kuwanyima kura.

Amani Msumari

Tanga (kwasasa Kigamboni kumtafutia Rais Magufuli kura za bonus).
 
Hayo mtaenda kufungua mashitaka baada ya Tundu Lisu kuapishwa kuwa Raisi 2020,ila kwa sasa tena msirukie huko na kutaka kupotosha. lengo ni kuiondoa CCM hatusikii hatuoni liwalo na liwe lakini CCM kwanza ikae pembeni.

Hata kura ya maoni inaweza kutaarishwa kwa hilo linalowakwaza.Ila sasa kwanza CCM wakae chonjo wapumzishwe.
 
..kama mikoa haijatutenga, basi majimbo nayo hayawezi kututenga.

..hata wakati Tanganyika ilipokuwa na majimbo wananchi hawakuwa wametengana.

..mfumo wa majimbo utarahisisha shughuli za utawala, na kupeleka maendeleo kwa wananchi kwa haraka zaidi.
 
Naona umeleta ushahidi hapa kuwa majimbo hayana uhusiano wowote na kuondoa umoja wa kitaifa kwa mifano uliyoitoa!
Ninachoshangaa ni kwamba kama mnaupenda sana umoja wa kitaifa kwaninj hamzungumzii uhuru na haki za raia wenu?Haya meneno mawaili mnayaona kama ukakasi midomoni kwenu!

Msingi wa umoja wa kitaifa na haki na uhuru!
 
Hayo mtaenda kufungua mashitaka baada ya Tundu Lisu kuapishwa kuwa Raisi 2020,ila kwa sasa tena msirukie huko na kutaka kupotosha.lengo ni kuiondoa CCM hatusikii hatuoni liwalo na liwe lakini CCM kwanza ikae pembeni.
Hata kura ya maoni inaweza kutaarishwa kwa hilo linalowakwaza.Ila sasa kwanza CCM wakae chonjo wapumzishwe.
Nchi haiendeshwi kwa ndoto ya mzee Mtei ambayo CHADEMA wote wanalazimika kuihubiri na kuitetea. Haifai kwani itatuletea shida kubwa Kama taifa. Tutawakataa na hata sasa tumewakataa
 
Waungwana,

Chunguzeni leo hii nchi zote ambazo ni kinara wa mfumo wa Serikali za majimbo (federal government) duniani ni nchi ambazo zilikuwa zinakabiliwa Sana na tatizo la kukosa umoja wa Kitaifa kutokana na Vita, udini au Kukosa lugha ya kuwaunganisha...
Kwanza wewe ni Muongo, Ujerumani sio Nchi mbili, Ujerumani ni Nchi 17 na kila Nchi ina Raisi wake, na wanatumia hio Dhana ya Majimbo ingawa wote wanazungumza kijerumani. Siri kuba ya mafanikio yao ni huo mgawano wa Majimbo, kua Kodi zinakuswanya kuanzia chini, kilichobaki ndio kinaenda serikali kuu.

Baadae Serikali kuu inaangalia jimbo lopi ni Tajiri Zaidi na lipi ni Maskini inachangia kuweka usawa baina ya Majimbo. Hata Baada ya Ujerumani ya mashariki na Magharibi , Magharibi walikuwa Matajiri ukilinganisha na Mashariki, kwa hiyo Wafanyakazi wa Magharibi walikuwa wanalipia kodi iliyokuwa ikiitwa Solidarity Tax (Kuonesha umoja) mpaka mwaka huu ndio kodi hio iimeondolewa
 
Hata Marekani na Canada mwanafunzi au mfanyakazi anaweza kupangiwa kazi au shule na maisha yanakwenda fuleshi kabisa.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
Huko hakuna wewe ni kabila flani au dini flani. Halafu nchi yao imeshaendelea na wanapata mahitaji yote. Hapa kwetu aki tutashikana uchawi. Kwani Nigeria au Somalia ni mbali kaka? Mifano ipo hai
 
Marekani haikuwahi kuwa na Mataifa 51 huru ilikuwa ni majimbo 13 yaliyokuwa makoloni chini ya utawala mmoja wa ufalme wa Uingereza.
Waungwana,

Chunguzeni leo hii nchi zote ambazo ni kinara wa mfumo wa Serikali za majimbo (federal government) duniani ni nchi ambazo zilikuwa zinakabiliwa Sana na tatizo la kukosa umoja wa Kitaifa kutokana na Vita, udini au Kukosa lugha ya kuwaunganisha..
 
Kwanza wewe ni Muongo, Ujerumani sio Nchi mbili, Ujerumani ni Nchi 17 na kila Nchi ina Raisi wake, na wanatumia hio Dhana ya Majimbo ingawa wote wanazungumza kijerumani...
Sasa unajipinga mwenyewe? Nimesema nchi mbili za Ujerumani magharibi na Mashariki hapo kabla ya kuungana. Wewe vipi?
 
Majimbo yatatutenga zaidi badala ya kutuleta pamoja. Mfumo wa Serikali za mitaa kwa Tanzania ni mzuri na toshelevu. Kama Kuna changamoto basi ni Kuboresha tuu.
Yaani huu mfumo wa kumsubiri Rais aje kwenye Kampeni ndiyo aseme peleka pesa kujenga barabara ya 10 km Itigi .... Seriously!!

Mfumo unaopendekezwa hautatofautiani sana na huu wa sasa kimuundo. Tofauti itakuwa ni kuwa nguvu inarudishwa kwa wananchi. Siyo lazima tufanye kama US au RSA .... haiwezekani kwenye nchi kubwa kama hii pesa ya barabara ya mtaani kwangu, choo cha sokoni au mabati ya shule iwe issue ya Rais wa nchi ....!!
 
Yaani huu mfumo wa kumsubiri Rais aje kwenye Kampeni ndiyo aseme peleka pesa kujenga barabara ya 10 km Itigi .... Seriously!!

Mfumo unaopendekezwa hautatofautiani sana na huu wa sasa kimuundo. Tofauti itakuwa ni kuwa nguvu inarudishwa kwa wananchi. Siyo lazima tufanye kama US au RSA .... haiwezekani kwenye nchi kubwa kama hii pesa ya barabara ya mtaani kwangu, choo cha sokoni au mabati ya shule iwe issue ya Rais wa nchi ....!!
Sio ishu ya Rais, n ishu ya bunge. Bajeti huandaliwa kutoka ngazi ya chini kabisa ili kuleta uwakilishi
 
Ondokana na mawazo ya kijima ya kufikiria kazi lazima itoke serikalini,maendeleo yakiwepo ya kutosha hata huko kusubiri kupangiwa kazi kutokana na ajira za serikali kutaondoka.

Marekani watu wengi zaidi wanatoka jimbo moja kwenda lingine kufanya biashara kuliko kusubiri kupangiwa kazi za serikali kuu kwa sababu mfumo wao umewezesha watu binafsi kuzifikia fursa binafsi za biashara na kazi zaidi kuliko ajira za serikali.
Huko hakuna wewe ni kabila flani au dini flani. Halafu nchi yao imeshaendelea na wanapata mahitaji yote. Hapa kwetu aki tutashikana uchawi. Kwani Nigeria au Somalia ni mbali kaka? Mifano ipo hai?
 
Waungwana,

Chunguzeni leo hii nchi zote ambazo ni kinara wa mfumo wa Serikali za majimbo (federal government) duniani ni nchi ambazo zilikuwa zinakabiliwa Sana na tatizo la kukosa umoja wa Kitaifa kutokana na Vita, udini au Kukosa lugha ya kuwaunganisha...
Kwahiyo ata Serikali za mitaa zitafutwa?
Maana Federal System ndiyo imezaa Decentralization by Devolution.
D by D
 
Ni majimbo yanayojiongeza sio yaliyokuwa yanajiongeza kwa sababu hayakuanza yote pamoja,yalianza majimbo 13 na yakazidi kuongezeka kwa njia mbalimbali mpaka kufika 50 sio hata 51.
Sawa. 51 states ni majimbo yaliyokuwa yanajiongoza
 
Back
Top Bottom