Je, wajua kuwa jongoo anao uwezo wa kudhuru afya yako,au hata kuua?

Na mwalimu Ngui au Mwangoka?
Usipime mkuu enzi za baba kadoda na mbabe mwaipaja, mwangoka alikuwa ananiavha hoi, hata kiwe na baridi vipi kuvaa sweta mwiko, yeye na uji uji wake, enzi za andazi la mama uswege na marehemu nelkon
 
Tandu anayo sumu na alichokisema kuhusu jongoo kipo ni kuhusu kujihami kwake unaweza kuwashwa nk lakini siyo SUMU,
SOURCE mbili tatu nilizopitia haraka haraka wamesema ni HARMLESS kwa binaadamu.

MACHO HANA NA BADO KUMSINGIZIA HAMUOGOPI WABONGO BANAAA.
Kipofu au scopion?
 
Hukuwa na haja ya kusema bavicha wala nini. Nawewe ungejibu kwa hoja. Wakati mwingine tunakua na hoja za msingi ila tunaonekana wapuuzi kwa kuingiza siasa kila kona
Huyu jamaa ni Mpuuzi anajifanya mjuaji hana lolote hakuna mahusiano yoyote ya mada yake na Bavicha!
 
Mkuu pinga kwa hoja, usiwe kama Bavicha, hebu mtafute jongoo kama Hugo kwenye picha dheni mchezee harafu mgusishe kwenye ngoZi yako ili urete mrejesho mzuri hapa
Hapo umechemka mkuu,kwa hiyo Uvccm huwa wanapinga kwa hoja,unaingiza siasa pasipo stahil siasa,kumbe na wewe ni wale wale,kwa hiyo usingetaja Bavicha usingeeleweka au ndiyo kitu unachokifikria muda wote maishani mwako
 
kweli umepona
hadi mood yakupost UZI unayo...

ASANTE KWA HII ELIMU ..daaah hill lilinipita kushoto kabisa ..sikuwahi kulijua hapo awali...
ila mimi binafsi jongoo nawapnda mnoo sababu kuu niule upole wao
 
Hiyo kwetu chakula!!! Tena tami zaidi akiwa mbichi... Unamvunja na kunyona ile juice yake
 
Tandu anayo sumu na alichokisema kuhusu jongoo kipo ni kuhusu kujihami kwake unaweza kuwashwa nk lakini siyo SUMU,
SOURCE mbili tatu nilizopitia haraka haraka wamesema ni HARMLESS kwa binaadamu.

MACHO HANA NA BADO KUMSINGIZIA HAMUOGOPI WABONGO BANAAA.
Nimecheka sana. Na bado nimejifunza kitu. Wanadamu tuna Chuki sana.
 
Hpn sio kweli hata siamini jogoo nimewachezea sana utotoni na mpaka huwa na wakamata kwa mikono au kupiga mateke sana kuwatupa nikiwakuta ndani au kwenye maharage
 
Jongoo wamegawanyika katika makundi makuu mawili...
...
Lakini kwa asilimia kubwa sana jongoo ana sumu tena mbaya sana inayojulikana kama Hydrogen Cyanide Gas ambayo iko kama kimiminika fulani hivi, na mara nyingi hukitoa kwaajili ya kujilinda na adui wake pale anapoguswa utaona anajikunja na kumwaga maji haya (unaweza ukadhani anakunya) lakini ndio self defence yake huyu mdudu. Sumu hii ina madhara makubwa sana kwa mwanadamu pale anapoigusa kama vile maumivu ya mbaaaaali au makali sana au hata kuwashwa na pia kubabua ngozi kama MTU aliyeunguzwa maji moto ..
...
Rejea utafiti wako au pale uliposoma. Jongoo hutoa majimaji yenye harufu kali kujikinga na adui. Majimaji haya huitwa hydrochloric acid ambayo yaweza kuchubua ngozi.

Kama yataingia mdomoni, kama zilivyo acid zote, ukiimeza hiyo itakuchubua mdomoni na kooni na ukapata naumivu makali sehemu hizo na tumboni. Matibabu ya haraka yatakurejesha kwenye hali ya afya ya kawaida.
 
Jongoo wamegawanyika katika makundi makuu mawili ambayo ni wenye sumu na wasiokuwa na sumu,

Lakini kwa asilimia kubwa sana jongoo ana sumu tena mbaya sana inayojulikana kama Hydrogen Cyanide Gas ambayo iko kama kimiminika fulani hivi, na mara nyingi hukitoa kwaajili ya kujilinda na adui wake pale anapoguswa utaona anajikunja na kumwaga maji haya (unaweza ukadhani anakunya) lakini ndio self defence yake huyu mdudu. Sumu hii ina madhara makubwa sana kwa mwanadamu pale anapoigusa kama vile maumivu ya mbaaaaali au makali sana au hata kuwashwa na pia kubabua ngozi kama MTU aliyeunguzwa maji moto

Lakini sumu hii huwa hatari sana ikiwa itaingia tumboni mwa binadamu kwani inaweza kuua kwa muda mchache sana

Jongoo huwa hatari zaidi kwa watoto wanaotambaa kwani kwani wao huwachezea pasina kujua, hivyo wazazi tuwe makini katika kipindi hiki cha mvua kwani jongoo huongezeka sana.

Mara nyingi jongoo wa aina hii ndo hatari sana, hawapaswi kubughudhiwa hata kidogo>>>>>>
a81892d83e1785c0cdba6bcf62f3d50d.jpg
>>>>
64bce0b3da62ac1a68a47a96c19428b4.jpg
<<<<<<<

Asanteni na Mungu awabariki sana
Huyo ni jongoo (millipede):
"millipedes are not poisonous, but many species have glands capable of producing irritating fluids that may cause allergic reaction in some individuals. The defensive sprays of some millipedes contain hydrochloric acid that can chemically burn the skin and cause long-term skin dislocation."
 
Huyu jamaa ni Mpuuzi anajifanya mjuaji hana lolote hakuna mahusiano yoyote ya mada yake na Bavicha!
Ujuaji wangu uko wapi Mkuu!? Unagombana na MTU usiyemjua? By the way nimekuomba msamaha kama nimekuudhi! Nisamehe, sina ujuaji wala upuuzi unaousema
 
Back
Top Bottom