Je, wajua kufanya "Back up" ni njia moja ya ulinzi wa data katika kifaa chako?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
1582721533031.png

Back up ni hatua muhimu ya #UlinziWaData kwani humsaidia mhusika kutunza taarifa zake muhimu ili hata akipoteza kifaa chake au kikiharibika aweze kuzipata tena

Kuna majukwaa mengi yanayotoa huduma ya Backup kwa uchache ni Google Drive, One Drive, Team Drive, iCloud, SugarSync, MyPCBackup n.k

Aidha ya data ambazo zinaweza kuwekwa au kufanyiwa Backup: Nyaraka laini, picha, video, na sauti. Unaweza kufanya backup kwa kutumia simu yako au kompyuta yako

Hata hivyo umakini unahitajika sana wakati wa kuchagua sehemu ya kuhifadhi taarifa zako, hakikisha mtoa huduma hiyo anazingatia ufaragha wa taarifa zako

#UlinziWaData

JINSI YA KUFANYA BACK UP KWENYE GOOGLE DRIVE KWA WATUMIAJI WA SIMU ZA ANDROID​

Kwa watumiaji wa simu za mfumo wa Android wengi wao wanatumia Email na huduma za Google hivyo wao wanaweza kuhifadhi data zao katika Google Drive

Unaweza kufanya back up ya taarifa zako kwa kufuata hatua zifuatazo: Kama simu yako haina Application ya Google Drive basi unapaswa kuipakua (Download) kwanza

Kama tayari una application hiyo ifungue kisha nenda sehemu yenye alama ya kujumlisha au tafuta sehemu imendikwa Pakia Faili au Upload File bofya sehemu hiyo

Simu yako itakutaka uchague faili, data au nyaraka unayotaka kuifanyia back up, chagua taarifa husika kama ni picha, video, namba za simu au nyaraka

Baada ya kufuata hatua hizo simu yako itaanza kuhifadhi taarifa hizo kwenye Google Drive kwa ajili ya kutunzwa

KUMBUKA: Kazi hii huitaji simu yako iwe ina kifurushi cha Internet au iwe imeunganishwa na huduma ya Internet kwa njia nyingine kama vile Wi-Fi

Aidha, unaweza kuchagua na kuiruhusu simu yake iwe inafanya backup kila inapounganishwa na huduma ya Wi-Fi

 
Hili ni somo zuri. Kwanza nadhani hakuna sababu ya yeyote kutohifadhi data zake mahala pa uhakika kwani mchakato wenyewe haukugharimu kama ambavyo ungegharamika ukipoteza mambo yako muhimu. Imagine kuwa na sehemu salama (tena ya bure tu) ya kuhifadhi nyaraka zako ambazo huwezi kuzi-replace!
 
Kuhifadhi data ni kitu muhimu sana, ukizingatia vifaa tutumiavyo sio imara sana vingi vinaharibika kirahisi au wakati mwingine vinaweza kupotea.

Hivyo kama utakuwa umehifadhi data zako kwenye sehemu ambayo unaweza kufanya buck up na ukazipata unakuwa salama wakati wote na itakupunguzia hatari ya kupoteza taarifa au nyaraka muhumu.
 
Hivi kufanya backup kama una sensitive information si ndo unazidi kuzitapanya zipatwe na hackers huko?

Bora zibaki sehemu moja.
 
Ni muhimu. Na kuna njia zaidi ya moja ya kufanya hivi. Hata unapopoteza kifaa chako, bado unakuwa na access ya files ulizotunza
 
Kwa kuzingatia kufanya backup inakuepusha na athari za kupoteza picha na nyaraka mbalimbali za muhimu ambazo utahitaji kuzitumia hapo baadaye.

Muda na pesa unazozitumia kwenye usalama wa taarifa zako mtandaoni ni uwekezaji unaofaa.
 
naomba kujua kama kuna namna naweza kuweka password kwenye google drive...yani ninapoingia iwe inani guide kuweka password
 
Kuna tofauti kati ya Ulinzi wa Data na Uhifadhi wa Data.

Ulinzi wa data ni zile njia za kuzihifadhi data katika usalama ili zisiweze kuathirika kwa namna yoyote.

Kilichoelezwa hapa ni uhifadhi wa data nje ya kifaa bebeshi kwa njia ya mtandao. Lengo ni kuweza kuzipata tena data husika endapo kifaa hicho kitapotea au kuharibika.

Kwa ufupi, sio kila kilichohifadhiwa kimelindwa au kipo salama.
 
naomba kujua kama kuna namna naweza kuweka password kwenye google drive...yani ninapoingia iwe inani guide kuweka password

Chakufanya mkuu, download app lock ,itakayo kufaa kwa matumizi yako Kisha , Google drive na app zingine unaziunganisha kwa applock
 
Chakufanya mkuu, download app lock ,itakayo kufaa kwa matumizi yako Kisha , Google drive na app zingine unaziunganisha kwa applock
Nikipoteza kifaa changu au kubadili nikiweka email zangu ina maana nikipakua tena app lock nitapata data zangu kule kama ambavyo nazikuta kwenye google drive?

Sivutiwi na Google drive sababu haina password
 
Hivi kufanya backup kama una sensitive information si ndo unazidi kuzitapanya zipatwe na hackers huko?

Bora zibaki sehemu moja.
Kama nahitaji kufanya back up kwa njia hizo ila nikiwa na laptop, inakuwaje? Sitaki kuweka katika storage disc kama external disc
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom