Je, wajua Japan watu huajiriwa ili kuwasukuma watu kwenye treni?

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,000
9,862
Kazi hii inapatikana nchini Japan kutokana umati unaokwenda kazini nyakati za asubuhi kwa kutumia usafiri wa treni. Japan ni taifa linalochapa kazi, na huhakikisha kila mtu anafika kazini kwa wakati unaotakiwa.

Kutokana na wingi wa watu, Japan imewaajiri watu wenye taaluma ya kuwasukuma watu ndani ya treni wakati kuna msongamano ili pasiwe na mtu hata mmoja wa kuchelewa kazini.

Wasukumaji hawa wakati mwingine hulazimika kuwasukuma ndani ya treni wasafiri ambao huchelewa kupanda treni au wakati wanapositasita kupanda kwa madai kwamba treni imejaa.

Wanaotaka kazi hii wanatakiwa kuvaa sare nyeupe na glovu nyeupe na watatakiwa kufanya kazi hiyo kati ya saa moja na saa tatu asubuhi, kisha saa moja jioni hadi saa tatu usiku.

Kazi hiyo huchukuliwa kama kama kazi ya ziada na mara nyingi hufanywa na wanafunzi na mshahara haufahamiki.

Bongo tunaweza kuajiri watu kusukuma watu daladala za Mbagala, Gongolamboto na Kimara

 
Mmmmhhh Japan kweli hawafuati taratibu za Safety?

Labda miaka ya zamani na labda pia pakiwa na crisis. Sio kirahisi hivyo. Ila bado siamini.
 
Kazi hii inapatikana nchini Japan kutokana umati unaokwenda kazini nyakati za asubuhi kwa kutumia usafiri wa treni. Japan ni taifa linalochapa kazi, na huhakikisha kila mtu anafika kazini kwa wakati unaotakiwa.

Kutokana na wingi wa watu, Japan imewaajiri watu wenye taaluma ya kuwasukuma watu ndani ya treni wakati kuna msongamano ili pasiwe na mtu hata mmoja wa kuchelewa kazini.

Wasukumaji hawa wakati mwingine hulazimika kuwasukuma ndani ya treni wasafiri ambao huchelewa kupanda treni au wakati wanapositasita kupanda kwa madai kwamba treni imejaa.

Wanaotaka kazi hii wanatakiwa kuvaa sare nyeupe na glovu nyeupe na watatakiwa kufanya kazi hiyo kati ya saa moja na saa tatu asubuhi, kisha saa moja jioni hadi saa tatu usiku .

Kazi hiyo huchukuliwa kama kama kazi ya ziada na mara nyingi hufanywa na wanafunzi na mshahara haufahamiki.

Bongo tunaweza kuajiri watu kusukuma watu daladala za Mbagala, Gongolamboto na Kimara

View attachment 1871770
Kunaitwa kushindilia
 
Wahuni wa kijep walikuwa wakitumia kujaa sana kwa treni zao kufanya uhuni wa kuwashika matiti KE na sehemu zao nyeti ikiwemo makalio. Na walikuwa wajanja sana kugundulika ni nani aliyefanya huo uhuni. Malalamiko ya KE yalipozidi Serikali ikaamua kuwe na treni za gender tofauti ili kumaliza uhuni huo.
 
Back
Top Bottom