kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,839
- 17,437
Unajua mimi huwa sipendi kuzungumzia mambo ya dini dini kabisa nilishakataa kabisaTafiti zimeonyesha binadamu meenye matatizoya figo anaweza kupona kwa kupandikiziwa figo ya nguruwe,View attachment 1983581
Kuna dhehebu linaitwa mashahidi wa yehova, hili dhehebu linazuia mtu wa dini hiyo kuongezewa damu,
Je waislam mtakubali kupamdikiziwa figo ya nguruwe?
Kama unakula kitimoto kula kwa raha zako, hakuna wa kukuzuiya, kama huli usile,
Wewe unayekula usimchukie asiyekula,na wewe usiyekula usimchukie anayekula, mwisho ni kila mtu na hesabu zake mbele ya mungu
Sasa niende moja kwa moja kwenye topic husika, hivi unajua ni upuuzi kuwahusisha waislam na mada zenu za kipuuzipuuzi za nguruwe
Nasema hivyo kwasababu sio dini ya kiislam pekee inakataza nguruwe bali hata dini ya kiikristo inakataza ulaji wa kitimoto
Soma kumbukumbu la torati mlango wa 14
MLANGO 14
Ninyi mmekuwa wana wa Bwana, Mungu wenu; msijitoje miili yenu, wala msifanye upaa katikati ya macho yenu kwa ajili ya aliyekufa.
2 Kwa kuwa u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako, na Bwana amekuchagua kuwa watu wake hasa, kuliko mataifa yote yaliyo juu ya uso wa nchi.
3 Usile kitu cho chote kichukizacho.
4 Wanyama mtakaokula ni hawa ng'ombe, na kondoo, na mbuzi,
5 kulungu, na paa, na kongoni, na mbuzi wa mwitu, na paa mweupe, na pofu, na mbuzi wa mlima;
6 na kila mnyama aliyepasuliwa ukwato, ukapasuka ukwato wake zikawa mbili, naye ni mnyama mwenye kucheua akatafuna tena, katika wanyama wote, ndiye mnyama mtakayemla.
7 Lakini, hawa msile katika wale wenye kucheua, na hao waliopasuliwa ukwato; ngamia, na sungura, na kwang'a, kwa kuwa hucheua, lakini hawakupasuliwa kwato, ni najisi kwenu;
8 na nguruwe, kwa kuwa amepasuliwa ukwato lakini hacheui, huyu ni najisi kwenu msile nyama zao, wala mizoga yao msiiguse.
9 Mtakula hawa katika wote walio majini; kila kilicho na mapezi na magamba mtakula;
10 na kila kisichokuwa na mapezi na magamba msile; ni najisi kwenu.
Sasa nauliza mnachowashwawashwa na waislam kuwataja ninini kwani bible haikatazi kula?Kwani msinyooshane ninyi kwa ninyi vidole kwakua vitabu vyenu vinakataza?
Kuna mmoja atakuambia hilo ni agano la kale.....Sasa kama ni agano la kale kwanini msilipige marufuku kutumika?Ukikataa agano la kale unatakiwa ukatae kila kila kitu kuanzia Amri kumi za mungu, uwakatae manabii wote wa vitabu vya agano la kale, ukatae kila kitu sio unasema ni agano la kale hilo, huku ukimtambua adam, eva,musa,yakobo, amri za mungu 10 nk....Wakati mwingine tuwe na akili ya kujua zuri na baya,,,mambo mengine ni kujiongeza tu.....Kuna mambo mengine ni kama taasisi za biashara tu...Some religion is all about money even spirit
Mimi ninaomba kabisa wanaJF iwe ni mwanzo na mwisho kuutaja uislam kwenye hayo mavitimoto yenu....kwamba waislam dini yao inawakataza kula....sasa kwani hiyo bible inayokataza kula kitimoto hilo agano la kale ni la waislam au wakristo....Kitabu chenu kiwakataze kula kitimoto ....Hafafu kula na kukiuka mle nyie... lawama mtutupie sisi.. ..huo ni ukorofi.Hebu tujaribu kuwa na akili tu kidogo tusiishi kwa kusukumwa tu na tamaa za kimwili tu na ulafi na anasa
Kila mtu apambane na dini lake, biashara za kusingiziana au kuleteana "scapegoatism" haikubaliani.....Nguruwe mle nyie...Utamu muusikie nyie.....Halafu lawama mtutupie sisi....STOP THAT NONSENSE
Mimi sipendagi kujadili masuala ya madini dini humu ila huu ujinga hauvumiliki hata kidogo.....TUHESHIMIANE.......