Sekibuju
JF-Expert Member
- Jul 23, 2012
- 314
- 130
Kwani ni waislam pekee ndio wanaosema nguruwe haramu? Hujui nchi hii km kuna baadhi ya Wakristo pia.Tafiti zimeonyesha binadamu meenye matatizoya figo anaweza kupona kwa kupandikiziwa figo ya nguruwe,
Kuna dhehebu linaitwa mashahidi wa yehova, hili dhehebu linazuia mtu wa dini hiyo kuongezewa damu,
Je waislam mtakubali kupamdikiziwa figo ya nguruwe?
=====
Figo ya nguruwe iliyopandikizwa kwa binadamu mgonjwa yafanya kazi
Washington, Marekani (AFP). Nguruwe ni mnyama ambaye nyama yake inaliwa na baadhi ya jamii, huku nyingine zikiiepuka kutokana na sababu za kiimani, na sasa timu ya madaktari nchini Marekani imeongeza changamoto katika suala hilo baada ya figo ya mnyama huyo iliyopandikizwa kwa binadamu kuonekana inafanya kazi.
Mafanikio ya majaribio hayo yamesifiwa na madaktari waliofanya upasuaji huo kuwa ni "uwezekano wa miujiza".
Upasuaji huo uliofanyika Septemba 25, ulihusisha mnyama huyo mtoaji figo aliyefanyiwa marekebisho, na mgonjwa ambaye ubongo wake ulishakufa na ambaye alikuwa katika mashine ya kupumulia.
Familia ya mgonjwa huyo iliruhusu kufanyika kwa upasuaji huo wa siku mbili, kwa lengo la kuendeleza sayansi.
"Ilifanya kile ilichotakiwa kufanya, ambacho ni kuondoa uchafu na kutengeneza mkojo," Robert Montgomery, mkurugenzi wa taasisi ya upandikizaji katika Chuo Kikuu cha New York (NYU) Langone, aliiambia AFP katika mahojiano.
Kiungo hicho cha nguruwe kiliweza kupunguza kiwango cha molecule creatinine, uchafu unaochujwa kutoka kwenye damu na kutolewa nje ya mwili kwa njia ya mkojo, kitu ambacho ni ishara muhimu ya afya ya figo kwa mgonjwa.
Advertisement
Montgomery alifanya upasuaji huo na wenzake kadhaa katika muda wa karibu saa mbili.
Waliunganisha figo hiyo ya nguruwe na mishipa ya damu juu ya miguu ya mgonjwa, ili kuwawezesha kuifuatilia na kuchukua sampuli.
Mgonjwa huyo alikuwa ametaka kuwa mtoaji wa kiungo na awali familia yake ilifadhaishwa ilipoambiwa kuwa kiungo cha mpendwa wao hakikuwa kinafaa, alisema Montgomery.
Lakini "walijisikia ahueni fulani kwamba hili (la kujaribisha figo ya nguruwe kwa mgonjwa wao) ni fursa nyingine ya kutoa msaada," alisema.
Mgonjwa aliondolewa katika mashine ya kupumulia na akafariki baada ya saa 54 zilizofuata za kupima.
Utafiti wa awali ulionyesha kuwa figo za nguruwe zinafaa kutumika kwa viumbe ambavyo si binadamu kwa hadi mwaka mmoja, lakini hii ilikuwa ni mara ya kwanza zimejaribishwa kwa binadamu.
Nguruwe aliyetolewa figo ni miongoni mwa mifugo iliyopitia mchakato wa marekebisho ya kuondoa jini ambazo huzalisha sukari ambayo ingeweza kusababisha kingamwili za binadamu kuhamaki na kukikataa kiungo hicho.
Chanzo: Mwananchi
Kwann uzi wako umeegemea kwa Waislamu tu.
Ikumbukwe kuwa kula nguruwe mtu wa dini yeyote kubwa katika hizi dini kuu, ni ulafi wake tu, kwakuwa vitabu vimeweka wazi kabisa kuwa nguruwe hafai kuliwa.
Isaya 65:4
[4]waketio kati ya makaburi, na kulala katika mahali pao pa siri; walao nyama ya nguruwe, na mchuzi wa vitu vinichukizavyo u katika vyombo vyao;
Kumbukumbu la Torati 14:8
[8]na nguruwe, kwa kuwa amepasuliwa ukwato lakini hacheui, huyu ni najisi kwenu msile nyama zao, wala mizoga yao msiiguse.
Kutumia kwa kuokoa uhai katika hali ngumu hii haina tatizo.
Maamuzi ni yako.