Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Nimeisikiliza Kwa makini Sana hotuba ya Rais Samia Suluhu Hassan, aliyoitoa Leo, huko Ikulu, wakati anaongea na viongozi wa vyama vya siasa nchini.
Kwa kweli Sina budi kumpongeza Rais wetu Samia Suluhu Hassan, Kwa msimamo wake Kwa kueleza kuwa kama Taifa, inabidi tujenge mshikamano, umoja na utulivu na vyama vyote vya kisiasa, kwani ndiyo nguzo kuu ya kutuletea maendeleo endelevu ya kudumu.
Alieleza zaidi kuwa hatuwezi kuujenga umoja huo kama tutaendelea kutowafanyia haki Kwa kutowatendea haki vyama vya upinzani, Kwa kuendelea kuwanyima haki yao ya kikatiba ya kuitisha mikutano ya hadhara ya kisiasa.
Jambo moja ninalojiuliza, ni Kwa vipi mtangulizi wake Hayati Magufuli, aliamua kuzivunja Sheria za nchi, ambazo zinaruhusu mikutano hiyo ya hadhara kwenye nchi hii ya mfumo wa vyama vingi vya kisiasa?😎
Alieleza kuwa wajibu wa Jeshi la Polisi ni kuilinda mikutano hiyo Ili ifanyike Kwa amani na wala siyo kuipiga marufuku isifanyike.
Rais aliendelea kueleza kuwa wao kama watawala, wangependa Sana kukosolewa, kwani ni Kwa njia hito inayoweza kuwafanya wajirekebishe na kuwatendea mambo mazuri watanzania, Kwa lengo la kuwapatia maendeleo.
Lakini ingawa uamuzi huo ameutoa kama Rais na wakati huo huo kama Mwenyekiti wa chama chake Cha CCM, ninaamini kabisa kuwa ndani ya chama chake Kuna wahafidhina wachache ambao Bado wanaunga mkono maamuzi ya Hayati Magufuli ya kuipiga marufuku mikutano hiyo hawatapenda maamuzi hayo na wangependa kuendeleza malumbano na kutotenda haki dhidi ya vyama vya upinzani
Kwani wahafidhina hao wanaamini kuwa Kwa kuruhusu mikutano hiyo ya hadhara Kwa vyama vya siasa, maovu yao yatawekwa hadharani na hivyo kuzifanya nafasi zao za kiutendaji Serikalini ziwe katika hati hati😃
Kwa kweli Sina budi kumpongeza Rais wetu Samia Suluhu Hassan, Kwa msimamo wake Kwa kueleza kuwa kama Taifa, inabidi tujenge mshikamano, umoja na utulivu na vyama vyote vya kisiasa, kwani ndiyo nguzo kuu ya kutuletea maendeleo endelevu ya kudumu.
Alieleza zaidi kuwa hatuwezi kuujenga umoja huo kama tutaendelea kutowafanyia haki Kwa kutowatendea haki vyama vya upinzani, Kwa kuendelea kuwanyima haki yao ya kikatiba ya kuitisha mikutano ya hadhara ya kisiasa.
Jambo moja ninalojiuliza, ni Kwa vipi mtangulizi wake Hayati Magufuli, aliamua kuzivunja Sheria za nchi, ambazo zinaruhusu mikutano hiyo ya hadhara kwenye nchi hii ya mfumo wa vyama vingi vya kisiasa?😎
Alieleza kuwa wajibu wa Jeshi la Polisi ni kuilinda mikutano hiyo Ili ifanyike Kwa amani na wala siyo kuipiga marufuku isifanyike.
Rais aliendelea kueleza kuwa wao kama watawala, wangependa Sana kukosolewa, kwani ni Kwa njia hito inayoweza kuwafanya wajirekebishe na kuwatendea mambo mazuri watanzania, Kwa lengo la kuwapatia maendeleo.
Lakini ingawa uamuzi huo ameutoa kama Rais na wakati huo huo kama Mwenyekiti wa chama chake Cha CCM, ninaamini kabisa kuwa ndani ya chama chake Kuna wahafidhina wachache ambao Bado wanaunga mkono maamuzi ya Hayati Magufuli ya kuipiga marufuku mikutano hiyo hawatapenda maamuzi hayo na wangependa kuendeleza malumbano na kutotenda haki dhidi ya vyama vya upinzani
Kwani wahafidhina hao wanaamini kuwa Kwa kuruhusu mikutano hiyo ya hadhara Kwa vyama vya siasa, maovu yao yatawekwa hadharani na hivyo kuzifanya nafasi zao za kiutendaji Serikalini ziwe katika hati hati😃