Je, wachezaji wote wa Tanzania waliosajiliwa timu za nje wanastahili kuitwa katika kikosi cha Taifa Star?

Mzalendo_Mkweli

JF-Expert Member
Jan 30, 2012
1,988
1,175
Leo nilijaribu kujipa kazi ya kufuatilia maendeleo ya timu za Afrika ambazo wachezaji wetu wa kulipwa wanazichezea huko. Wachezaji ambao nimefuatia timu zao ni Himid mao Mkami (Petrojet-Misiri), Thomas Ulimwengu (JS Saoura-Algeria), Simon Msuva (Difaa el jadida- Morocco) na Abdi Banda (Baroka fc- Afrika Kusini). Katika Tathmini yangu nimegundua kwamba mchezaji pekee ambaye timu yake itashiriki mashindano ya vikombe vya Afrika mwakani ni Thomas Ulimwengu wa JS Saoura ya Algeria ambayo katika Ligi ya huko inashika/Itashika nafasi ya nne.

Nilipojaribu kufuatilia mchango wa wachezaji (wanavyopangwa) wa Tanzania katika timu zao, nimekutana na changamoto kidogo ya kupata taarifa sahihi sana hasa kwa timu za mataita ya kiarabu (Morocco, Algeria na Misri) ambao mifumo ya kutoa hali za michezo katika mitandao (Status) hawatoi Line-up (wachezaji waliopangwa) ila nimeona Substitutions tu (wachezaji wa akiba) hivyo kushindwa kupata hitimisho kama wachezaji Thomas Ulimwengu, Himid mao Mkami, Simon Msuva wanapangwa mara kwa mara katika vilabu vyao au la. Nilipojeukia kwa Abdi Banda ambaye anachezea huko afrika ya kusini huko nimepata taarifa zote za wachezaji yaani vikosi vya kwanza na wachezaji wa akiba kwa kila mechi. Nilipofuatilia takwini za kiuchezaji za Abdi Banda nimegundua kwamba ni zaidi ya miezi mitatu/minne Abdi Banda hajawepo katika Kikosi cha kwanza au cha akiba cha Baroka fc. Natambua kwamba Baroka fc katika miezi kama sita iliyopita wamekuwa katika vita kubwa ya kuepuka kushuka daraja katika ligi yao, lakini Je mchezaji ambaye hakuweza kumvutia kocha hata mara moja kuwa katika kikosi cha akiba kwa zaidi ya miezi minne atakuwa na "Fitness" ya kutosha kuichezea timu yetu ya taifa Taifa? Je mchezaji akishasajiliwa tu timu ya nje ya Tanzania kunampa ticket ya moja kwa moja ya kuitwa timu ya Taifa.

Nimetoa mawazo yangu kama mfuatiliaji tu wa mambo ya mpira wa miguu na sio mtaalamu wa mpira wa miguu.

Wataalamu na wafuatiliaji wenzangu wa mpira wa miguu mnakaribishwa kutoa maoni yenu.

Nawakilisha
 
Wa nkana anacheza ni kweri kwa banda acheni Kabsa miez Miwili iliyopita nilikuwa Limpopo South Africa na ndio team ya banda inatoka jamaa achezi
 
ni msuva na kessy pekee wanao pata angalau muda kidogo wa kucheza wengine wote ni uongo awapat muda wa kucheza ,
 
Nadhani kuna utofauti wa kusugua benchi Cardiff City iliyoshuka daraja England na kuanza first eleven Simba iliyochukua ubingwa wa TPL.
 
Nadhani kuna utofauti wa kusugua benchi Cardiff City iliyoshuka daraja England na kuanza first eleven Simba iliyochukua ubingwa wa TPL.
Punguza majungu mkuu, ungeweza kuchangia tu bila kuwahusisha mabingwa wa nchi na ungeeleweka bila matatizo yoyote yale.
 
Kabla ya Majeruhi Banda alikuwa anacheza sana tu.Msuva anaanza wakati mwingine haanzi kama sammata tu naye sio kila Mechi anaanza.pia Kessy anaanza na wakati mwingine haanzi.kwa hiyo sio kwamba kila mchezaji kwa kuwa ni mzuri lazima aanze.kuna rotation ya timu.Sammata pamoja na magori mengi alofunga kuna mechi zaidi ya 7 ameanzia nje.pia msuva mara kadhaa nimemwona akifunga mara 2 kwenye mechi zao.Ko bado tupo kwenye right track.Tumwombe Mungu ajibu apate namba huko Mazembe ili tuzidi mwakani kuwa bora.Mfano kundi letu la Afcon msimu huu lilikuwa jepes sana,sio hadi mechi ya mwisho iamue kama sasa
 
Rudi tena kufuatilia hata taarifa zao sio kuishia kuangalia list ya vikosi.
Mfano miezi hiyo unaitaja Banda alikua majeruhi ndo mana hata kwenye mechi ya Stars na Uganda hakuitwa
 
Rudi tena kufuatilia hata taarifa zao sio kuishia kuangalia list ya vikosi.
Mfano miezi hiyo unaitaja Banda alikua majeruhi ndo mana hata kwenye mechi ya Stars na Uganda hakuitwa
Mimi nimefungua mdahalo /majadiliano hivyo basi kama wewe una taarifa kinzani unaweza kuzitoa. Yote kwa yote nilichokisema kuhusu ukosefu wa "Match Fitness" kwa baadhi ya wachezaji wanaocheza nje ya nchi ni jambo linalohitaji kujadiliwa bila kumwonea mtu.
 
Mimi nimefungua mdahalo /majadiliano hivyo basi kama wewe una taarifa kinzani unaweza kuzitoa. Yote kwa yote nilichokisema kuhusu ukosefu wa "Match Fitness" kwa baadhi ya wachezaji wanaocheza nje ya nchi ni jambo linalohitaji kujadiliwa bila kumwonea mtu.
Mkuu naona huna taarifa sahihi
 
Kuna mwaka Maximo alijifanya eti kuita ma pro wanaocheza nje bwana wee akaleta rasta mmoja eti foward anaitwa Michael Chuma na kipa anaitwa muharami lahaulaa yaani timu ikawa ikawa haifungi na golini ni kama kulikua na shati tu .. ilikua kituko.. tukawa tunagongwa tu mara moja mara mbili mara tatu.. tena kipindi hicho Kaseja yuko moto kweli golini na mgosi alikua balaa lkn hawapangwi sababu ya ma pro koko.. na utashangaa hapa akapangwa Himidi anayecheza mechi moja kwa mwaka akaachwa mkude ambaye mwaka mzima alikua bize kupambana na Sevila, Vita club, Mazenbe, Nkana, Ahly nk..
 
Back
Top Bottom