Nini Majukumu ya Mbunge kwa wapiga kura wake?

Mwanamayu

JF-Expert Member
May 7, 2010
11,347
6,471
Mara nyingi wabunge wanawahidi wananchi kuwa watawapelekea maendeleo, je hiyo ndio kazi ya mbunge? Kwenye katiba ya URT ibara ya 63 na 64, kazi ya mbunge ni kushiriki kwenye kutunga sheria na kusimamia na kushauri serikali. Sasa haya mambo ya nitajenga barabara, nitawachimbia kisima ni ya kweli? Na wanaofanya hivyo kwa pesa zao sio rushwa hiyo? Wananchi tusome katiba!

Au watuambie watatunga sheria nzuri kwa kiwango kipi ili kuboresha maisha yetu? Watasimamia serikali na kuishauri ili kuleta ubora wa maisha? Tusipowasikia bungeni, hakuna ajira! Wakishabikia sheria mbovu, wakiwashabikia mafisadi, hakuna ajira!!!


Swali No.2 Kutoka kwa Kijakazi

Nina swali ambalo limekuwa likinitatiza siku nyingi sana hapa nchini nalo ni kuhusu kazi ya Mbunge, hivi kazi ya Mbunge hasa nini (kikatiba) jimboni kwake?

Nauliza hivyo kwa maana mara nyingi nimekuwa nasikia wananchi wengi wanamlalamikia Mbunge wao kwamba hajafanya kitu jimboni kwao kwamba hajajenga Barabara, au hajaleta Maji au sijui hajajenga Daraja, sasa kitu ambacho sielewi Mbunge yeye ana mamlaka gani ya kufanya hayo mambo niliyoyataja?

Kama swala la Miundo mbinu mtoaji na muamuaji Barabara au Maji yawekwe wapi si Serikali, sasa yeye Mbunge ana uwezo gani au mamlaka gani ya kujenga Barabara au daraja jimboni kwake mpaka kustahili kupata lawama zote hizo? naomba mwenye uelewa na haya mambo aweze kunielezea kazi hasa ya Mbunge (Kikatiba ) ni ipi?

MAJIBU KUTOKA KWA WANAJF


Ndugu wanaJF,

Baada ya kusoma Katiba ya Jamahuri ya Muungano wa Tanzania kifungu cha 63 (hapo chini) chenye kuianisha madaraka ya wabunge nimekuwa nikijiuliza hii dhana ya watanzania kuwatarajia wabunge kuleta maendeleo katika jimbo moja moja k.m huduma za kijamii kama vile shule, zahanati, barabara, maji n.k chimbuko lake nini.


Ikiwa wananchi wataendelea kuwapima wabunge wao kwa viwango vya manedeleo katika majimbo binafsi badala ya uwezo wa kuisimamia na kuishauri serikali;
kwa kuwa Rais na Mawaziri ni sehemu ya Serikali ambayo wabunge wanatakiwa kuisimamia kwa mujibu wa katiba; na ili kupata maendeleo binafsi jimboni wabunge hulazimika kuwapigia magoti mawaziri ambao kwa mujibu wa katiba hii wanapaswa kuwasimamia.

Hatuoni kwamba katika kila chaguzi watanzania hupoteza fursa ya kuingiza bungeni idadi kubwa ya wabunge wenye uwezo wa kuisimamia serikali na badala yake kuwaingiza bungeni makuadi wa ufisadi ambao hawana ujasiri wa kuwasimamia mawaziri, makatibu wakuu n.k;

Na kibaya zaidi kuwatoa bungeni wale walionyesha uwezo wa kuisimamia serikali lakini wakashindwa kuwapigia magoti mawaziri (wanaopaswa kusimamiwa) ili kupatiwa migao binafsi ya maendeleo jimboni?

Ikiwa watanzania wataendelea na dhana ya kuwatarajia wabunge kuleta maendeleo katika majimbo binafsi kama vile chenge alivyofanya bariadi, lowassa alivyofanya monduli n.k kwa kutumia fungu dogo kati ya mabilioni ya fedha zinazoibiwa serikalini kila mwaka kutokana na usimamizi hafifu wa bunge.

Hatuoni kwamba hali ndio husababisha usimamizi wa serikali kupwaya na kupelekea rais na mawaziri kutumia fedha za rasirimali za Tanzania watakavyo. Matokeo yake Tanzania imeendelea kubaki katika lindi la umaskini licha ya kupata uhuru mika 49 iliyopita ikilinganishwa na kiwango cha rasirimali kilichopo?.

Ni kwanini Watanzania wasiwaachie wabunge kazi ya kuisimamia serikali na wakasubiri maendeleo kwa mujibu wa mipango ya serikali kwa wananchi wote kwa uwiano sawa kwa majimbo yote badala ya utaratibu wa sasa ambapo baadhi ya mawaziri na watendaji wa serikali wanaruhusu kiasi kikubwa cha fedha na rasalimali za taifa kupotea ili waweze kupata kidogo cha kupeleka majimboni mwao kuwapoza wananchi wanaowachagu na kujilimbikizia ziada?

Je, katika hali hii vita dhidi ya ufisadi itafanikiwa kweli?

63.-(1) Rais kama sehemu moja ya Bunge atatekelezamadaraka yote aliyokabidhiwa na Katiba hii kwa ajili hiyo.

(2) Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu chaJamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwaniaba ya wananchi, kuisimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii.

(3) Kwa madhumuni ya utekelezaji wa madaraka yake Bunge laweza-
(a) kumuuliza Waziri yeyoyote swali lo lote kuhusu mambo ya umma katika Jamhuri ya Muungano ambayo yako katika wajibu wake;

(b) kujadili utekelezaji wa kila Wizara wakati wa Mkutano wa Bunge wa kila mwaka wa bajeti;

(c) kujadili na kuidhinisha mpango wowote wa muda mrefu au wa muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa katika Jamhuri ya Muungano, na kutunga sheria ya kusimamia utekelezaji wa mpango huo;

(d) kutunga sheria pale ambapo utekelezaji unahitaji kuwapo sheria;

(e) kujadili na kuridhia mikataba yote inayohusu Jamhuri ya Muungano na ambayo kwa masharti yake inahitaji kuridhiwa.

======
Wana jamvi naomba tuwekane sawa Nitapokuwa nimekosea nisahisheni juu ya h baadhi ya duku duku, maswali na maoni yangu.


  1. Kwanza napenda nieleweshwe kazi hasa ya mbunge ni nini.?Je kazi za Mbunge wa magu zinatofautiana na zile za mbunge wa Sengerema.?Wajibu wa diwani unaanzia wapi na wajibu wa mbunge unaishia wapi.Je hakuna duplication ya vyeo. Ni katika level gani inakuwa ni kero ya kufanyiw akazi na diwani na katika level gani inakuwa ni kero ya kufanyiwa kazi na mbunge?
Baadhi ya majibu ni kuwakilisha/ kutatua matazizo ya wananchi. Jibu hili lina zaa swali lingine

2. Je matatizo ya msingi ya wanachi wa jimbo la bunda yanatofautiana na matatizo ya msingi ya wanachi wa jimbo la Tarime?


Binafsi naamini Tanzania tofauti na nchi zilizoendelea matatizo yetu ya msingi kwa sasa ni common. hatuhitaji wabunge wengi sababu matatiz ni yetu ni yale yale ELIMU, AFYA, MAJI, NISHATI, etc.Nadhani USA UK wanahitaji wabunge wengi sababu naamini matatizi ya msingi walishayatatua wamebaki kutatu area specific problem ndio maana kilo cha mbunge wa jimbo fulani la labda london inaweza isiwe tatio kwa mbunge wa jimbo fulani la Birmingham .

Nadhani kila wilaya ingekuwa na mbunge 1ja ingetosha na hizo na hizo hela ambazo wanalipwa wabunge zingeenda kwenye kutatua true poblem in local areas.

Naamini hii kasumba ya kuongeza majimbo ni ya kupumbaza wanachi wajione serikali imesogea karibu yao wakati huduma na mahitaji yya msingi ya wanachi bado inakuwa kero.

3. Je Ni halali kwa mbunge kusema akichaguliwa ataleta barabara ya rami au atajenga shule au ataleta umeme au visima vya maji? je ni kazi ya wabunge kufanya hivi? Najiuliza mbunge anakuwa ana maanisha nini kusema yeye ataleta barabara ina maana washindani wake hawawezi kuleta barabara?Ina maana atatumia Hela zake mfukoni?

Hapa napata wasi wasi kuwa kuna aina ya watu wakiwa wabunge( eg profesors, Dk, friends to president family, etc) labda serikali inakuwa wepesi kutekeleza maombi yao na kuna aina ya watu wakiwa wabunge hata wakiongea kitu gani cha maana serikali inaziba masikio.

KAZI ZA WABUNGE HASA NI NINI?

4.Je wastani wa gharama za uchaguzi kwa kila jimbo ni shilingi ngapi? Kwani mbunge
akifariki. akitimuliwa chama kabla ya mhuhula kuisha nafasi isichukuliwe na yule aliekuwa
wa pili ?


Hoja yangu ni kuwa badala serikali kofocus na kutumia a mapensa mengi kwenye dhana ya demokrasia ya uteuzi na si ku focus zaidi kwenye dhana utekelezaji wa sera zake.
 
Last edited by a moderator:
Mwanamayu

Ni kweli wanachofanya si majukumu yao. Kila siku wanapaswa kuulizwa kama wametekeleza majukumu yao. Wananchi nao wanapaswa kukumbushwa kuwauliza wabunge kama wametekeleza majukumu yao badala ya kuwauliza mambo mengine.

Remote
Kuna tatizo la kujua majukumu ya Mbunge. Nina uhakika hata wao hawajui majukumu yao. Kwa ufupi Mbunge ni mwakilishi wa wananchi katika ngazi mbali mbali kuanzia jimbo, wilaya au mkoa. Kwa upande mwingine ni mwakilishi wa wananchi katika ngazi ya taifa ambayo ni Bunge.


Mbunge si mtendaji kikazi. Kazi yake ni coordination ya haja za wananchi na maamuzi yatakayoathiri wananchi wa eneo lake. Ni mfuatiliaji wa maamuzi yanayohusu wananchi wake katika ngazi za jimbo hadi taifa.


Si kazi ya mbunge kutoa pesa za shughuli za maendeleo kwasababu hana fungu.

Mbunge anapaswa kuangalia mafungu yaliyopo au kujenga hoja za kutafutwa fungu kwa haja ya kutimiza malengo mengine yenye ulazima na umuhimu.


Fungu la pesa za mbunge linalotolewa sasa hivi ni hongo tu halina maana yoyote.

Ni njia ya kumuongezea mbunge kipato. Fungu hilo halina audit na anayepaswa kuamua nani apate nini ni mbunge, kinyume na utawala bora.


Kujenga shule n.k kwa pesa zao ni hongo tu, hilo si jukumu lao.

Jukumu lao ni pamoja na kuangalia usalama na ustawi wa jamii zao.


Jiulize kuna sababu gani za kujenga shule wakati wafugaji na wakulima wanapigana. Mbunge amefanya nini kuhakikisha usalama wao.


Concern ya mbunge siku zote ni kuhakikisha kunakuwepo na mawasiliano ya uhakika na vyombo vingine akiwa kama ‘go between' na si kumwaga pesa.


Kwa nchi za wenzetu imefika mahali ofisi ya mbunge inasikiliza matatizo ya mtu mmoja mmoja ambayo ynahitaji msaada mkubwa (siyo kugawa pesa za chakula )
.

Mfano, mbunge anafuatilia kwanini mpiga kura wake amenyimwa haki ABCD au hakutendewa EFG na kwamba hilo ni tatizo la mfumo, watu au kitaifa.


Kama ni kitaifa mbunge atalifikisha bungeni kujadiliwa. Endapo ni mfumo wahusika watawajibika n.k.

Endapo kuna anayedhani kazi ya mbunge ni kutoa mipesa au misaada, sasa wale wa kuteuliwa na vyama au Rais wana kazi gani. Watatoa misaada wapi.

Kazi ya mbunge ni uwakilishi kwa ukubwa na upana wake, ngazi ya jimbo hadi taifa

 
Katika mwaka huu mzima wewe ndio umeanzisha topic yenye tija kwa taifa hili katika forum hii, lakini8 kwa bahati mbaya sana ni wananchi wachache wanaelewa unataka kumaanisha nini hata wana forum wenzetu wengi hawaelewi umuhimu wa discussion uliyotaka kuanzisha ndio maana wameshindwa kuchangia topic hii.

Kimsingi Tume ya Jaji Nyalali ilipanga rataiba ya kutolewa kwa elimu ya uraia kwa miezi 18 ndipo tuingie kwenye mfumo wa vyama vingi. Lakini wakubwa wetu wakakataa kwa kuwa walitambua kuwa wajinga wataamshwa katika usingizi wa pono waliolala wa kutaka wabunge wawaletee maji safi, barabara, shule n.k. Ili mbunge aweze kupata vitu hivi kwa jimbo lake ni lazima ampigie magoti waziri wa serikali mwenye mafungu ya fedha za maendeleo.

Ni kutokana na sisi wananchi kuwafanya wabunge wetu wawapigie magoti mawaziri wa serikali ambayo walipaswa kuisimamia na kuishauri ndio maana Serikali ya Tanzania inakosa mwelekeo kwa kukosa usimamizi wa wananchi ambao ulipaswa kutoka kwa wabunge. Siku watanzania watakapotambua kuwa maji safi, barabara, shule n.k. hupatikana kwa utaratibu wa kawaida wa utendaji wa serikali na sio uhodari wa mbunge wa jimbo fulani hapoi tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana ya kimaendeleo na Mawaziri na watendaji katika Serikali ya Tanzania wataanza kuwajibika kwa kuwa hakuna wabunge watakaokuwa wakiwapigia magoti kuwaomba maendeleo kwa joimbo fulani na badala yake wabunge watakuwa wakikagua matumizi ya fedha katika bajeti nzima.

Kutokana na sisi wananchi kuwahukumu wabunge wetu kutokana na vitu kama maji safi, barabara, shule, hospitaki, zahanati n.k katika majimbo yetu, masuala makubwa ya kitaifa kama vile kukuza uchumi, usafiri wa reli, foleni za magari barabarani, elimu duni n.k vimekuwa vuikikosa wabunge wa kuvisemea na kuifanya Tanzania kuendelea kubaki nyuma kimaendeleo.

Athari kubwa ya utaratibu huu wa wananchi kendekeza maslahi binafsi ya kijimbo badala ya maslahi ya taifa ni kufanya raslimali za Tanzania kukosa walinzi, kwani ilitazamiwa kuwa wabunge watakuwa walinzi wa raslimali za taifa wakati wakitimiza wajibu wao wa kuisimamia serikali.

Ili kurekebisha hali hii inatakiwa vijana wa Tanzania wajielimisha kuhusu topic hii na kuielewa vyema ndiipo waelimishe jamii kwa kuwa CCM hawataki wananchi kujua ukweli huu.
 
Wana jamvi naomba tuwekane sawa Nitapokuwa nimekosea nisahisheni juu ya h baadhi ya duku duku, maswali na maoni yangu.


  1. Kwanza napenda nieleweshwe kazi hasa ya mbunge ni nini.?Je kazi za Mbunge wa magu zinatofautiana na zile za mbunge wa Sengerema.?Wajibu wa diwani unaanzia wapi na wajibu wa mbunge unaishia wapi.Je hakuna duplication ya vyeo. Ni katika level gani inakuwa ni kero ya kufanyiw akazi na diwani na katika level gani inakuwa ni kero ya kufanyiwa kazi na mbunge?
Baadhi ya majibu ni kuwakilisha/ kutatua matazizo ya wananchi. Jibu hili lina zaa swali lingine

2. Je matatizo ya msingi ya wanachi wa jimbo la bunda yanatofautiana na matatizo ya msingi ya wanachi wa jimbo la Tarime?


Binafsi naamini Tanzania tofauti na nchi zilizoendelea matatizo yetu ya msingi kwa sasa ni common. hatuhitaji wabunge wengi sababu matatiz ni yetu ni yale yale ELIMU, AFYA, MAJI, NISHATI, etc.Nadhani USA UK wanahitaji wabunge wengi sababu naamini matatizi ya msingi walishayatatua wamebaki kutatu area specific problem ndio maana kilo cha mbunge wa jimbo fulani la labda london inaweza isiwe tatio kwa mbunge wa jimbo fulani la Birmingham .

Nadhani kila wilaya ingekuwa na mbunge 1ja ingetosha na hizo na hizo hela ambazo wanalipwa wabunge zingeenda kwenye kutatua true poblem in local areas.

Naamini hii kasumba ya kuongeza majimbo ni ya kupumbaza wanachi wajione serikali imesogea karibu yao wakati huduma na mahitaji yya msingi ya wanachi bado inakuwa kero.

3. Je Ni halali kwa mbunge kusema akichaguliwa ataleta barabara ya rami au atajenga shule au ataleta umeme au visima vya maji? je ni kazi ya wabunge kufanya hivi? Najiuliza mbunge anakuwa ana maanisha nini kusema yeye ataleta barabara ina maana washindani wake hawawezi kuleta barabara?Ina maana atatumia Hela zake mfukoni?

Hapa napata wasi wasi kuwa kuna aina ya watu wakiwa wabunge( eg profesors, Dk, friends to president family, etc) labda serikali inakuwa wepesi kutekeleza maombi yao na kuna aina ya watu wakiwa wabunge hata wakiongea kitu gani cha maana serikali inaziba masikio.

KAZI ZA WABUNGE HASA NI NINI?

4.Je wastani wa gharama za uchaguzi kwa kila jimbo ni shilingi ngapi? Kwani mbunge
akifariki. akitimuliwa chama kabla ya mhuhula kuisha nafasi isichukuliwe na yule aliekuwa
wa pili ?


Hoja yangu ni kuwa badala serikali kofocus na kutumia a mapensa mengi kwenye dhana ya demokrasia ya uteuzi na si ku focus zaidi kwenye dhana utekelezaji wa sera zake.
 
kwa jinsi ilivyo sasa naona mbunge kama anachukuliwa vibaya na wapiga kura .kama vile mbunge anatakiwa kuwa mtu mwenye fedha na uwezo binafsi wa mali ,anayeweza kujitolea mali hizo kwa wengine.

Wakati mwingine mbunge naona kama vile haijalishi hata asipokuwa mkazi wa eneo analogombea ili mradi ameonyesha nia au ameamua kugombea sehemu fulani ili mradi iwe ndani ya Tanzania na yeye ni mtanzania.

Kuna wakati nildhani kuwa kiongozi ni mtu wa watu fulani,anayechaguliwa katika kundi hilo la watu ,ili awaongoze/awawakilishe watu hao katika maisha yao ya kila siku.Nilidhani mtu huyo anatakiwa aishi na hao watu ili apate muda wa kushauriana nao ili kwa pamoja watatue changamoto au awakiilishe panapohusika na akiweza(hili sio lazima) ajitolee.je mbunge kazi yake nini ?wana jf naomba msaada.
 
Primarily, she / he has to join others Members of the Parliament:-

  • To pass laws for the good governance.
  • To provide, by giving legislative sanction to taxation and acquisition
    of means to carrying out the work of the government.
  • To scrutinize government policy and administration, including
    proposal for expenditure; and to debate major issues of the day

Kazi zao ni za muhimu sana. Pengine kichwa cha mada yako kingekuwa je tunahitaji Bunge kubwa la kiasi cha sasa kuleta ufanisi?
 
Mtazamaji usiwaangalie wabunge katika eneo moja la kuwakilisha wananchi, pia wanaisimamia Serikali itekeleze wajibu wake na kutunga Sheria! Kwa upande wa kuahidi kujenga barabara, visima, etc nadhani sio kazi yao ya msingi! Wabunge wamewaaminisha wananchi kwamba wanaweza kufanya vitu hivyo na inawagharimu sana!
 
Mimi nafikiri mbunge yeyote yule anapoteuliwa anakuwa haendi bungeni kwa minajili ya kusaidia kila tatizo ambalo lipo jimboni mwake. kwa mfano mbunge hayupo bungeni kutatua tatizo ambalo linaweza kutatuliwa na diwani ambae nae itabidi aishirikishe manispaa ya eneo husika.

Mbunge anafanya kazi kupitia serikali kuu kwa kutoa mchango wa mawazo yake bungeni na kupitisha mipango na maamuzi yote yanayopendekezwa na serikali kuu (miswaada) baada ya majadiliano na mifano ipo na mingi tu.

Umesema kwamba wabunge wengi wa Tanzania wanawakilisha matatizo ambayo yanafanana. Sidhani kama hilo linasumbua ila ni kasi gani mbunge ameishawishi serikali kuu kupitia bungeni labda kujenga barabara ya lami au daraja au kuweka kivuko sehemu au kujenga zahanati au hata hospitali, nafikiri hapa ndio iwe focal point ya swali.

Mbunge anaposema ataleta barabara mimi naelewa anamaanisha kwamba ata-raise jambo hilo bungeni kwa wizara husika au atafanya kampeni (Lobbying) na wananchi wa jimbo lake, jambo ambalo ni mara chache wabunge wanafanya ili barabara ya lami iwekwe mahali husika.

Ila ndani ya jimbo lake mbunge hana mamlaka makubwa kwani shughuli zote za maendeleo kama kuzoa taka, kukarabati barabara, kujenga recreation centres au bustani kwa kiswahili kwa mipango itakayosimamiwa na baraza la madiwani na serikali za mitaa husika.

Kwa mfano halmashauri ya manispaa fulani inaweza kusema kwamba itakarabati barabara fulani kwa kuweka upya lami kwa kutumia fwedha iliyotoka kwenye fungu la kodi za maendeleo na sio kujenga barabara mpya mbayo fwedha zake zitatoka serikali kuu kwa kuidhinishwa na wabunge.

Hata hivyo wabunge wengi waendao bungeni hawana nia ya kufanya mazuri kwenye majimbo yao kwani wengine tayari ni matajiri wakubwa na wapo pale kwa manufaa yao (kwenye masuala ya kodi, na ku-facilitate ufisadi mwingine mwingi tu) na matokeo yake kuanzia mwaka huu tutakuwa na bunge dhaifu (kiutendaji) kuliko mabunge yote yaliyowahi kuwepo Tanzania.

Nafikiri nimejaribu kueleza kidogo.
 
Kibunago,
Mkuu unajua Watanzania wengi hufikiria kwamba Mbunge jukumu la kazi yake ni kutoa vitu serikalini au mfukoni mwake na kuwapelekea Wananchi majimboni, badala ya kuwa Mbunge kazi yake ni kuwawakilisha hawa Wananchi huko bungeni ktk maswala mazito kama ulivuyoorodhesha yaani toka utungaji wa sheria, Utawala bora, kodi, bajeti na kadhalika, lakini maajabu ya Mussa wabunge wengi huulizwa katuletea nini swali ambalo lilitakiwa kukifuata CHAMA TAWALA ambacho sera zake ndizo zilitoa ahadi ya kutimiza mahitaji ya Wananchi.

Nijuavyo mimi in a way, Mbunge ni oneway Traffic ya kuwakilisha mahitaji ya wananchi huko Bungeni na njia inayorudi ni Chama kilichoshinda ktk mfumo huu wa winner takes all ndicho chenye jukumu la kurudisha yale matakwa ya wananchi kwao..

Sio jukumu la Mbunge kuwaletea wananchi maendeleo hata kidogo, isipokuwa ni serikali iliyopo madarakani na kibaya zaidi kwa nchi kama Tanzania ambayo winner takes all, fikra hizi zinaharibu kabisa nguvu ya Upinzani kwa sababu serikali inaweza kutopeleka maendeleo Karatu kwa Dr. Slaa wakijua lawama zitakwenda kwake, hivyo inambidi Dr. na uongozi wa Chadema kutafuta mbinu za kuwasaidia wananchi kwani kila mwananchi anategemea mbunge ndiye anayetakiwa kupeleka maendeleo kwao na sii chama kilichounda serikali..
 
Last edited by a moderator:
Wanajamvi
Tunakaribia kuwachagua.Tunasikia wanahaidi wataleta barabara,watajenga mashule,watajenga mahospitali na ahadi kibao.

Sasa swali ni hivi wananchi, wapiga kura tunajua wajibu wa wabunge. ?

Sometime huwa nashangaa na kuchanganyikiwa kusikia wabunge fulani wanapata sifa wamefanya kitu fulani jimbni kwao na wengine wanakejeliwa hawajapeleka mradi wowote.

  • Wajibu hasa wa mbunge ni nini?
  • Kipimo cha mbunge bora ni nini?( Maswali bungeni, kuibua kashfa,kutoa Msaada jimboni aukuwezeha miradi kwenda jimboni kwake)
Nawasilisha kwa mjadala
 
kazi ni kutunga sheria
siasa darasa la tano [enzi zetu]

siku hizi kazi ya bunge ni kulamba ulaji
 
kazi ni kutunga sheria
siasa darasa la tano [enzi zetu]

siku hizi kazi ya bunge ni kulamba ulaji
OK hiyo ya kutunga sheria ni kazi kuu sawa na wanaifanya wakiwa mjengoni. sasa je hawana majukumu au wajibu mwingine kisheria wakiwa majimboni mwao ?
 
Kwa Tanzania tu ikiwa chini ya CCM:

Kazi ya Mbunge wa Kike hasa wale wa kuchaguliwa ni Kuwahudumia Wazee wanapokuwa mbali na Wake zao.

1. Chifupa Amina (RIP).

2. Anna Abdallah.

3. Sofia Simba.

4. ###### *******

5. Tatu Ntimizi.

Kwa wanaume:

Wengi huwa pale ili kushangilia na kuongeza kura kwenye habari zozote zinaunga mkono Ufisadi.

Inatakiwa iwe kama walivyoelezea Waungana wengine juu ila huwa sivyo.
 
Ndugu wanaJF,

Baada ya kusoma Katiba ya Jamahuri ya Muungano wa Tanzania kifungu cha 63 (hapo chini) chenye kuianisha madaraka ya wabunge nimekuwa nikijiuliza hii dhana ya watanzania kuwatarajia wabunge kuleta maendeleo katika jimbo moja moja k.m huduma za kijamii kama vile shule, zahanati, barabara, maji n.k chimbuko lake nini.


Ikiwa wananchi wataendelea kuwapima wabunge wao kwa viwango vya manedeleo katika majimbo binafsi badala ya uwezo wa kuisimamia na kuishauri serikali;
kwa kuwa Rais na Mawaziri ni sehemu ya Serikali ambayo wabunge wanatakiwa kuisimamia kwa mujibu wa katiba; na ili kupata maendeleo binafsi jimboni wabunge hulazimika kuwapigia magoti mawaziri ambao kwa mujibu wa katiba hii wanapaswa kuwasimamia.

Hatuoni kwamba katika kila chaguzi watanzania hupoteza fursa ya kuingiza bungeni idadi kubwa ya wabunge wenye uwezo wa kuisimamia serikali na badala yake kuwaingiza bungeni makuadi wa ufisadi ambao hawana ujasiri wa kuwasimamia mawaziri, makatibu wakuu n.k;

Na kibaya zaidi kuwatoa bungeni wale walionyesha uwezo wa kuisimamia serikali lakini wakashindwa kuwapigia magoti mawaziri (wanaopaswa kusimamiwa) ili kupatiwa migao binafsi ya maendeleo jimboni?

Ikiwa watanzania wataendelea na dhana ya kuwatarajia wabunge kuleta maendeleo katika majimbo binafsi kama vile chenge alivyofanya bariadi, lowassa alivyofanya monduli n.k kwa kutumia fungu dogo kati ya mabilioni ya fedha zinazoibiwa serikalini kila mwaka kutokana na usimamizi hafifu wa bunge.

Hatuoni kwamba hali ndio husababisha usimamizi wa serikali kupwaya na kupelekea rais na mawaziri kutumia fedha za rasirimali za Tanzania watakavyo. Matokeo yake Tanzania imeendelea kubaki katika lindi la umaskini licha ya kupata uhuru mika 49 iliyopita ikilinganishwa na kiwango cha rasirimali kilichopo?.

Ni kwanini Watanzania wasiwaachie wabunge kazi ya kuisimamia serikali na wakasubiri maendeleo kwa mujibu wa mipango ya serikali kwa wananchi wote kwa uwiano sawa kwa majimbo yote badala ya utaratibu wa sasa ambapo baadhi ya mawaziri na watendaji wa serikali wanaruhusu kiasi kikubwa cha fedha na rasalimali za taifa kupotea ili waweze kupata kidogo cha kupeleka majimboni mwao kuwapoza wananchi wanaowachagu na kujilimbikizia ziada?

Je, katika hali hii vita dhidi ya ufisadi itafanikiwa kweli?

63.-(1) Rais kama sehemu moja ya Bunge atatekeleza madaraka yote aliyokabidhiwa na Katiba hii kwa ajili hiyo.

(2) Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwa niaba ya wananchi, kuisimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii.

(3) Kwa madhumuni ya utekelezaji wa madaraka yake Bunge laweza-
(a) kumuuliza Waziri yeyoyote swali lo lote kuhusu mambo ya umma katika Jamhuri ya Muungano ambayo yako katika wajibu wake;

(b) kujadili utekelezaji wa kila Wizara wakati wa Mkutano wa Bunge wa kila mwaka wa bajeti;

(c) kujadili na kuidhinisha mpango wowote wa muda mrefu au wa muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa katika Jamhuri ya Muungano, na kutunga sheria ya kusimamia utekelezaji wa mpango huo;

(d) kutunga sheria pale ambapo utekelezaji unahitaji kuwapo sheria;

(e) kujadili na kuridhia mikataba yote inayohusu Jamhuri ya Muungano na ambayo kwa masharti yake inahitaji kuridhiwa.
 
Jatropha

Ndio maana tunachagua wafadhili majimboni baadala ya Wabunge , watu kama Mkono , RA ,MO dewji ni wafadhili majimboni mwao
 
Last edited by a moderator:
Kwa muundo wa Tanzania mchango wa mbunge katika maendeleo ya sehemu husika ni mdogo sana .

Afadhali hata diwani anaweza kukaa na wananchi wake wakaamua kufanya mambo kadha wa kadha lakini sio mbunge.

Ushauri wa buree kwa ma great thinkers waanze kuangalia madiwani zaidi kuliko wabunge.:smile-big:
 
TanzActive

Na hilo ndio kosa linalofanyika kila mara. Wananchi wakishafadhiiwa na mbunge tajiri basi hata kama ni fisadi ataingia tu bungeni hata kama hatapiga kampeni.

Ni jukumu letu kuwaelimisha watanzania wenzetu kuwa si jukumu la mbunge kufadhili miradi ya maendeleo jimboni, japo mfuko upo-unaweza kutoa vijisenti kidogo!!

Kazi ya mbunge ni kuleta maendeleo jimboni kupitia bajeti ya serikali kwa kuainisha mahitaji ya msingi na kujenga hoja kwa nini jimbo lake lifikiriwe na kutekelezewa huduma husika.

Pili, kwa kuikosoa vilivyo na kuibana kila wakati kunapokuwepo na matumizi mabaya ya raslimali za taifa kwani ndizo hutumika kuleta maendeleo jimboni.

Suala la mbunge kupiga kampeni na kusema nimejenga madarasa mawili kwa pesa zangu mwenyewe ni la kupuuzwa. Mtu huyu ashukuriwe kwa utu wema na kujitolea kwake, jambo ambalo angeweza kulifanya hata bila kuwa mbunge kama ana roho ya kutoa, na uwezo pia!!
 
Last edited by a moderator:
Wakati mwingine huwa tunajisahau sana kwa maslahi yetu wenyewe ndio hicho kinatukwamisha as a whole. Hizi tabia zilianzishwa na wabinafsi na wakabila kama akina 'Msuya' huko Same na kuonekana mashujaa huko kwao kwa kuwakilisha. Leo hii ni trend kwa viongozi wote waliokuwa influential katika uongozi wa juu wanaona bora ni kujipendelea na kuonekana mashujaa kwa mfumo huu na kurudi bungeni despite depriving our national development and imroving our national economic strategies.

Kweli ina make sense mtu akaweke umeme Same juu, wakati chini hakuna na hapo ndipo kwenye economic activities. Hawa jamaa wameshauwa the meaning of representative na kuigeuza into local government. Along the way the constituencies have come expect their reps to bring the necessary changes regardless. Hii dhana ndio inauwa uchumi wa Taifa na serikali kutokuwa na priorities wala development strategies na wala kutotaka tambua umuhimu wa kuwa nazo kitaifa.

Na unakuta sasa ndio tuna agizia mpaka samaki, wakati mbunge badala ya kwenda bungeni na kusema sera kadhaa ina umiza jimbo langu kwa kuwa tunaagizia kitu ambacho kwangu kipo tele na uagiziaji una haribu maendeleo fulani. Hilo ni hapana kwa siasa zetu tunachojua ni kutafuta namna ya kuwapelekea maendeleo ya muda mfupi au yasiyo na faida katika jammii mfano kupoteza hela kujenga barabara sehemu ambazo hazina traffic ya hivyo wala national economic movement occur. Badala ya kuwasaidia kupigania sera za watu wajiendeleze wenyewe kwa kuhakikisha kilichopo ndio kina faidisha tanzania na watu wa huko jimboni zaidi.

But then how many policies pass in the house unscrutinised that affect the nation, hii inaonyesha ni jinsi gani baadhi ya wabunge kuwa na uwezo mdogo wa kuchambua mambo huko bungeni, na wala kutojua shughuli zao halisi na wala effects of the policies za serikali ndio wafugaji wanajikuta sasa wanashindana na watu wa njee kwa product ambazo tunazo. Wao waagizaji wanalipa ushuru na kupeleka bidhaa sehemu ambapo wafugaji hawazifikisha na kuweka bei zao hili kupata faida as a result tunapata national inflation. Badala ya sisi wenyewe kuja na sera za ku increase productivity na vitu ambavyo tunaweza fanya wenywe.

Ukweli ni kwamba huu mfumo wa sasa na fikra zetu za kazi ya mmbunge nao unachangia sana katika kuuwa the meaning of representative democracy kwa kuwa tumeuza sauti zetu na kumwachia mmbunge fate ya maendeleo yetu. Si ajabu ukute wabunge zetu wala hawapati tafrani na malalamiko ya mibarua kutoka kwa wananchi kudai kitu fulani kina tuathiri tunaomba utufikishie ujumbe wetu na matokeo yake watu kubaki kulalamikiana wenyewe kwa wenyewe tu. Wananchi sasa wanategemea mmbunge ajue matatizo yao huko ndio kupoteza demokrasia yenyewe na kuongeza uzembe wa jitihada binafsi. Ndio maana mijitu kama RA na Lowassa inapendwa kwao kwa sababu inasiadia sana na kuchota sana katika mfuko wa taifa.
 
:sad::sad:Hivi karibuni kumekuwepo na wimbi la wabunge kuchangia hela zao binafsi ili kuwasaidia wananchi/wapiga kura wao. Kwa mfano leo nimesikia kutoka vyombo vya habari kuwa Dr. Kigwa ametoa million 100 kuwalipia watoto wenye shida ada ya sekondari. Na wabunge wengi wamekuwa wakifanya hivyo huku wakiwaacha wananchi wao wakishindwa kupata masoko ya mazao yao na rasilimali zinazowazunguka zikichukuliwa na wageni.
Naomba kujua, je, kazi ya mbunge ni kuwa mfadhili au kuwapa wananchi uwezo wa kujitegemea?:sad:
 
Back
Top Bottom