Je, wabunge kupingana kuhusu hoja ya Katiba mpya ina maana gani?

Kasomi

JF-Expert Member
Sep 3, 2014
11,037
20,333
Machi 30 mwaka 2021 Bunge la Jamhuri ya Muungano lilishuhudia dalili za kurudi mchakatoni kutokana na hoja za wabunge wawili waliokinzana wakati wa vikao.

Mbunge wa Viti Maalumu kutoka chama cha upinzani Chadema, Sophia Mwakagenda alisema Rais Samia Suluhu anapaswa kutibu majeraha yaliyotokana na uchaguzi uliopita kwa kuwaachilia huru wafungwa wote wa kisiasa na kuendelea na mchakato wa Rasimu ya Katiba mpya ya Jaji Warioba.

Hoja ya Mbunge Mwakagenda ilipingwa na Mbunge wa Viti Maalumu wa chama tawala CCM, Munde Tambwe ambaye alieleza bungeni hapo kuwa hayati rais John Magufuli na rais wa sasa Samia Suluhu kwenye mikutano ya kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2020 walinadi maendeleo na kusisitiza kuwa viongozi hao hawakutoa ahadi ya Katiba mpya.

Aidha, kwa nafasi aliyonayo sasa yenye mamlaka makubwa kwa nchi hiyo na alikotoka kisiasa ni dhahiri Rais Samia ni kiongozi 'anayenukia' mchakato wa Katiba mpya.

Yeye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba akiwa chini ya Uenyekiti wa hayati Samwel Sitta, Mbunge wa zamani wa Urambo mkoani Tabora na Spika wa zamani wa Taifa hilo (2005-2010).

Mchakato huo ulikoma mwaka 2014 kwa mgawanyiko wa wapinzani wakiunga mkono Rasimu ya Katiba ya Jaji Warioba huku chama tawala CCM kiliunga mkono Katiba Pendekezwa ya Kamati ya Andrew Chenge.
Muundo wa Bunge la Katiba kipindi hicho ulitaka viongozi wa juu watoke katika pande mbili za muungano na kwa vile Mwenyekiti alikuwa ni hayati Samuel Sitta kutoka Tanzania Bara, hivyo nafasi ya Makamu Mwenyekiti iliangukia kwa Mzanzibari Samia Suluhu Hassan.

Usuli unaonesha kuwa Rais Samia akiwa mgombea mwenza wa tiketi ya chama cha CCM alishiriki kikamilifu kunadi na kuahidi kuendelezwa mchakato wa Katiba mpya kupitia mikutano ya kampeni ya uchaguzi mkuu akitumia ilani ya chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita (2015-2020).

Vilevile katika hotuba ya hayati John Magufuli wakati akifungua Bunge la 11 alisisitiza kuendelezwa kwa mchakato wa katiba mpya katika kipindi chake cha kwanza cha miaka mitano (2015-2020).

Hata hivyo hadi kukumilika kwa ngwe ya kwanza ya uongozi wao suala hilo hawakuendeleza mchakato wa Katiba mpya.

Aidha, wakati wa kunadi sera za CCM kwenye uchaguzi mkuu uliopita ilishuhudiwa chama hicho kiupiga teke mchakato huo baada ya kuondolewa kuwa miongoni mwa vipaumbele ndani ya Ilani ya uchaguzi kwa kipindi cha mwaka 2020-2025.

Kwenye mikutano ya kampeni ya urais,ubunge na udiwani si John Magufuli wala Samia Suluhu hawakujihusisha na ahadi za kuendelezwa mchakato wa Katiba mpya.

Si wagombea wa ubunge wala udiwani au timu ya kampeni za uchaguzi mkuu a CCM ambazo zilitamka lolote kuhusu kuendelezwa mchakato wa katiba mpya. Mchakato ni kama ulipigwa teke.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom