Uchaguzi 2020 Je, Vyombo vya Habari hapa nchini vimeripoti "press conference" aliyoifanya mgombea Urais kupitia Chadema, Tundu Lissu?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,477
30,130
Mgombea Urais kupitia CHADEMA jana Jumatano alifanya "Press conference" na Vyombo vya Habari hapa nchini, akilalamikia kutomfanyia "coverage" yeye akiwa ni mgombea Urais toka chama kikuu cha upinzani hapa nchini, kwa alichokiita ni Hofu, Hofu, Hofu iliyowajaa waandishi wa habari, pamoja na wamiliki wa vyombo hivyo.

Jambo la kushangaza ni kuona kuwa hata chombo cha habari cha Umma, Televisheni ya TBC, ambayo gharama za uendeshaji wake tunaibeba walipa kodi wa nchi hii, bila kujali itikadi zetu za kisiasa, nacho hakitaki kumripoti mgombea huyo wa kiti cha Urais!

Kwa namna ya jinsi inavyotoa ripoti, na kuzifanya habari za Rais John Magufuli, kuwa ni "lazima" zipewe kipaumbele, zinafanya chombo hicho cha habari nchini cha TBC, kuwa kama ni chombo cha propaganda za CCM!

Kinachotakiwa na vyombo vya habari hapa nchini ni kuondoa hofu ambayo imetanda miongoni mwao, katika kuripoti matukio ya kampeni ya mgombea huyo wa Urais wa chama kikuu cha upinzani nchini cha CHADEMA na kufanya kuwa fair kwa kutoa nafasi iliyo sawa kwa vyama vikuu hapa nchini vya CCM na CHADEMA.

Swali kubwa ninalojiuliza, je baada ya Tundu Lissu kufanya hiyo "press conference" vyombo vya habari hapa nchini vimeanza kubadilika na kuona hakuna "consequences" za kuanza kumripoti huyo mgombea Urais wa chama kikuu cha upinzani nchini cha CHADEMA?
 
Kama magazeti yameendelea kumfanyia "blackout" mgombea huyo wa Urais, basi tutajua kuwa ile Tundu Lissu, aliyoiita Hofu, Hofu, Hofu, iliyowajaa hao waandishi wa habari, kwa hawa watawala "dhalimu" imeendelea kuwatesa waandishi wa habari hao, pamoja na wamiliki wa vyombo vyao vya habari, wakihofia "consequences" zitakazowapata wakiripoti hiyo press conference
 
Hana issue za kuripotiwa , hakuna MTU wa kuripoti matusi na kejeri za muungano . Yeye akazane kuita wenzake , Wajinga, wapuuzi, washamba, Dictator, atukane majina yote lakini hakuna media yeyote itaripoti maneno hayo tena.
komamgo
Hebu nitajie angalau tusi moja, alilolitoa Tundu Lissu katika "Press conference" aliyoifanya hiyo Jana?

Kama usipotaja, ndipo tutaamini maneno aliyotoa Tundu Lissu, kuwa waandishi wa habari na wamiliki wao, wanawaogopa sana akina Dkt Abbas, kuhofia "consequences" zitakazowapata, iwapo tu vyombo vyao vya habari vitampa "coverage" kubwa huyo mgombea Urais toka chama cha Chadema
 
JokaKuu
Imekuwa vyema kama vyombo vya habari vitakuwa vimeanza kubadilika na kuanza kumfanyia "coverage" mgombea huyo wa Urais Tundu Lissu, ambapo hapo awali walikuwa wanaogopa kuripoti habari zake

Tukiamini sasa kuwa SAA YA UKOMBOZI ishawadia!

..opening statement ni about 30 minutes.

..Q&A session ni zaidi ya masaa mawili.
 
Wewe umesikia tusi?
Kama hukusikia jua walinyofoa (edit)
Hakuna speech asiyotoa bila kuwaita wenzake majina ya ajabu .
Yaani yeye anajua kila kitu, anaweza kila kitu, wenzake wote ni zero, wenzake hawajui chochote. Yaani hata watanzania nao hawajui kabisa , yeye peke yake anajua na anaweza na anaomba mchango kwa lazima.
Mpuuzi huyo achana naye, anahofia BUKU SABA YAKE iko mbioni kutoweka.
 
Madikteta wOte Duniani, hakuna hata mmoja, anayependa au kuruhusu uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa maoni.

Wakati wa Mabuto huko DRC, ole chombo cha habari kitangaze habari za mtu yeyote anayemkosoa yeye au Serikali. Ilikuwa hivyo kwa Amin, Bokasa, Nguema, Gadafi, Sadam, n.k.

'...... vyombo vya habari hampo huru kiasi hicho'

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mgombea Urais kupitia Chadema jana Jumatano alifanya "Press conference" na vyombo vya habari hapa nchini, akilalamikia kutomfanyia "coverage" yeye akiwa ni mgombea Urais toka chama kikuu cha upinzani hapa nchini, kwa alichokiita ni Hofu, Hofu, Hofu iliyowajaa waandishi wa habari, pamoja na wamiliki wa vyombo hivyo.

Jambo la kushangaza ni kuona kuwa hata chombo cha habari cha Umma, Televisheni ya TBC, ambayo gharama za uendeshaji wake tunaibeba walipa kodi wa nchi hii, bila kujali itikadi zetu za kisiasa, nacho hakitaki kumripoti mgombea huyo wa kiti cha Urais!

Kwa namna ya jinsi inavyotoa ripoti, na kuzifanya habari za Rais John Magufuli, kuwa ni "lazima" zipewe kipaumbele, zinafanya chombo hicho cha habari nchini cha TBC, kuwa kama ni chombo cha propaganda za CCM!

Kinachotakiwa na vyombo vya habari hapa nchini ni kuondoa hofu ambayo imetanda miongoni mwao, katika kuripoti matukio ya kampeni ya mgombea huyo wa Urais wa chama kikuu cha upinzani nchini cha CHADEMA na kufanya kuwa fair kwa kutoa nafasi iliyo sawa kwa vyama vikuu hapa nchini vya CCM na CHADEMA.

Swali kubwa ninalojiuliza, je baada ya Tundu Lissu kufanya hiyo "press conference" vyombo vya habari hapa nchini vimeanza kubadilika na kuona hakuna "consequences" za kuanza kumripoti huyo mgombea Urais wa chama kikuu cha upinzani nchini cha CHADEMA?
Kuna mtu route za makananisani haziishi ila binadamu wenzake anawaona kama wanyama.

Mpende jirani yako kwanza kabala huajampenda mungu wa mbinguni.
 
Hana issue za kuripotiwa , hakuna MTU wa kuripoti matusi na kejeri za muungano . Yeye akazane kuita wenzake , Wajinga, wapuuzi, washamba, Dictator, atukane majina yote lakini hakuna media yeyote itaripoti maneno hayo tena.
Sasa mbona mikutano ya jamaa chuchu, Titi kama barakoa, nitakupa mama angu ?

Hayo ni maneno common ayo sio matusi?
 
Wewe umesikia tusi?
Kama hukusikia jua walinyofoa (edit)
Hakuna speech asiyotoa bila kuwaita wenzake majina ya ajabu .
Yaani yeye anajua kila kitu, anaweza kila kitu, wenzake wote ni zero, wenzake hawajui chochote. Yaani hata watanzania nao hawajui kabisa , yeye peke yake anajua na anaweza na anaomba mchango kwa lazima.
Nikiona kijana anatetea CCM na conclude kuwa ni mvivu,mnafiki, muongo.

Na hataenda mbinguni.
 
Tundu anatukana na kukejeli hilo ni kosa, lakini yeye kuitwa shoga, msaliti, na matusi mengine ni sawa kwa CCM.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom