Je, Viongozi wa Idara ambao ni Wachagga waachie ngazi!??

Status
Not open for further replies.

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
A MODEST PROPOSAL

Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna vumbi la chuki, fitina, wivu, kisasi, na hisia za kibaguzi dhidi ya jamii ya Wachagga nchini. Kuna kila dalili kuwa jamii ya Wachagga nchini siyo tu inaanza kutengwa lakini uwepo wake katika nafasi mbalimbali za uongozi inazua hoja ya ukabila kwa haraka zaidi yawezekana kuliko kabila jingine lolote nchini. Katika Tanzania yetu, wachagga wameanza kunyoshewa kidole siyo kwa siri tena bali kwa wazi kabisa tena na watu ambao wakati mwingine hawapati hata kigugumizi.

Ubaguzi huo msingi wake mkubwa ni idadi ya wachagga katika nafasi mbalimbali za uongozi na hasa kuhusiana na elimu yao. Kuanzia mara tu baada ya uhuru jamii ya wachagga mojawapo ya jamii ambayo watu wake wengi wamesoma sana na kufanikiwa kielimu na kiuchumi imekuwa ikinyoshewa kidole cha kupendelewa.

Mtu yeyote ambaye anaweza akafanya uchambuzi yakinifu hatoshangaa kukuta wataalamu wa kichagga katika nafasi mbalimbali za uongozi au taaluma nchini. Kwenye vyuo vikuu, kwenye idara za serikali na hata kwenye taasisi binafsi kumejaa watu wenye asili ya mkoa wa Kilimanjaro na hususan watu wa jamii ya Kichagga.

Endapo itatangazwa nafasi yoyote ya kitaalamu usishangazwe ukiona kuwa waombaji wengi wana majina ya "Kichagga".

Ni kwa sababu hiyo basi kuna kila dalili kuwa kutokana na wingi wao katika nafasi muhimu na vyeo mbalimbali (hata ndani ya Jeshi la Polisi) Wachagga siyo tu ni wengi lakini wanaonekana kufanikiwa zaidi. Hili ni tishio kwa baadhi ya watu. Ni tishio kwa watu ambao hawako tayari kuangalia jitihada za watu katika kufanikiwa kwao na matokeo yake kushutumu ukabila kila idadi ya Wachagga kwenye kitengo fulani inazidi mmoja.

Ushauri wangu ni kuwa, kwa vile Wachagga wameshasoma sana na kuendelea katika biashara karibu mikoa mingi nchini. Na kwa vile wanaendelea kufanikiwa pia katika nafasi mbalimbali za uongozi nchini, basi itakuwa vizuri kama watajitolea kuachilia nafasi hizo ili kuwapa nafasi watu wa makabila mengine.

Kwa vile ni wao wanaonekana kulalamikiwa kutokana na mambo ya kifisadi aidha kwa moja kwa moja au kwa kuashiria basi ni vizuri wawape watu wengine nafasi hizo hata kama watu hao hawajasoma sana. Hii yote itakuwa ni katika kudumisha mshikamano, umoja na udugu wa Taifa letu.

Endapo Wachagga wataachilia nafasi mbalimbali kama UCEO, Ukurugenzi, Ukuu wa Idara n.k watasababisha watu wawapende na kuwakubali kuwa ni wazalendo wa kweli. Sitoshangaa kuwa ndugu zetu wa Jamii ya Kichagga wakikaa pembeni, basi ufisadi utakoma serikalini, idara zitaongozwa na watu wazuri, na mara moja na daima Tanzania itaanza kukua katika uongozi.

Kwa kupendekeza nashauri wabunge wote ambao ni Wachagga au wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro kuachia ngazi mara moja ili watu wa makabila mengine wapewe nafasi hizo. Siyo wao tu bali pia wabunge ambao wameoa au kuolewa uchagani vile vile wafuate nyazo hizo.

Wakishamaliza hao, wakuu wote wa idara za serikali ambao wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro na hasa wa jamii ya kichagga (wamarangu, wamachame, wa Rombo, na wa Kibosho) na wao waamue kuachilia nafasi hizo kwa ndugu zao Wamakua, Wamwera, Wa Ndali, Wadigo n.k Katika hili Wapare hawahusishwi.

Tukishamaliza wakuu hao wa idara za serikali ningependekeza madaktari wote wenye kumiliki hospitali binafsi ambao ni wachagga au wameoa/kuolewa uchagani na wenyewe waamue kuingia ubia na watu wa makabila mengine kama wangengereko, wambuu, na wanjiro ili hayo makabila madogo na wenyewe wapate nafasi ya kujifunza fani hizi muhimu.

Zaidi ya yote, majaji na mahakimu wote ambao wana asili ya Uchaggani na wenyewe waamue kujitoa katika nafasi hizo kwani wingi wao pia unaonekana sana na hivyo kuwa kikwako kwa watu wa makabila mengine kufanikiwa zaidi katika nyanja ya sheria. Kwanza kabisa wale majaji wa Kichagga wa mahakama ya Rufaa na Mahakama Kuu wawe wa kwanza kuweka manyanga chini.

Katika kufanya hivyo jamii ya Watanzania ambao inaona ukabila wa wachagga katika sehemu nyingi itaridhika kwani kwa mara ya kwanza tutakuwa tumeshughulikia chanzo cha matatizo yetu mengi.


NB: (Added Commentary: Jan 20, 2011)

Kwa watu wengi wanaosoma makala hii hawajui ilianza lini na wanaisoma bila kuangalia tarehe. Nimeona niweke nyongeza hii ili wasomaji wapya wasije kurukia mahitimisho ambayo siyo kusudio langu kwani nimekuja kutambua ni wachache sana wanafahamu aina hii ya uandisi wa kejeli (satire).

Niliandika mtindo huu kufuatia mfano wa Jonathan Swift's "A Modest Proposal". Nashauri watu wasome kidogo juu ya uandishi wa "Modest Proposal" ulivyo ili waelewe. Wachache hata hivyo walinielewa.
 
here is far and beyond. Kujiondoa kwenye nafasi nadhani sio suluhisho mbadala. Suluhisho needs critical thinking and analysis, this is so conclusive, hebu iweke vizuri as frankly speaking hakuna atakayejiondoa, kwa hiari!!!! none.
 
hahaha mwanakijiji shauri yako.....watu watashindwa kukuelewa na kuona kuwa umekuwa mbaguzi kwa wachaga sasa!

kwa upande wangu naona mtu anaelalamika sehemu fulani kumejaa wachaga au kabila jengine anakosea as logn as hajaja na hoja ya kutuonyesha kuwa kwa nafasi anayoipigia kelele kulikuwa na watu wa makabila mengine ambao ni bora zaidi hawakuchaguliwa na akachaguliwa mchaga.

na hapo itabidi atuthibitishie bila ya shaka kuwa alipendelewa kwa kuwa mchaga na sio kwa sababu nyengine kama kwa jinsia yake, au kwa urafiki wao, au kwa favour nyengin
 
here is far and beyond. Kujiondoa kwenye nafasi nadhani sio suluhisho mbadala. Suluhisho needs critical thinking and analysis, this is so conclusive, hebu iweke vizuri as frankly speaking hakuna atakayejiondoa, kwa hiari!!!! none.

Kama kwa hiari haiwezekani, Rais anaweza kutoa agizo (executive order) na kutaka wachagga waachie ngazi na wakae pembeni kwa angalau miaka mitano ili watu wa makabila mengine wapate nafasi. Hili linaweza kuwahusu Wanyakyusa na Wahaya vile vile. Kama hawatafanya kwa hiari tunaweza kufanya kwa nguvu hata kwa kutunga sheria maalum ya kuwalazimisha.
 
A MODEST PROPOSAL

Na. M. M. Mwanakijiji


.

Kwa kupendekeza nashauri wabunge wote ambao ni Wachagga au wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro kuachia ngazi mara moja ili watu wa makabila mengine wapewe nafasi hizo. Siyo wao tu bali pia wabunge ambao wameoa au kuolewa uchagani vile vile wafuate nyazo hizo.


mengi.

MMM

Kuna hoja inatolewa kwamba kati ya Wabunge wa CCM wachagga ni asilimia kubwa zaidi. Unayoorodha ya Wabunge tuweze kuchambua nani ni mchagga na nani sio mchagga?

Sio kwa lengo la kuchochea ubaguzi, ila kwa lengo la kufahamu ukweli manake CCM wamekuwa wakisema kuwa chama mpinzani wao cha CHADEMA kina wachagga wengi sana wabunge wa viti maalum.

PM
 
Mwanakijiji acha mzaha, tumia mbinu nyingine kufikisha hoja unayotaka kuwasilisha hapa, ikitumia kabila watu watadicusss emotions zao tu.
 
Kama kwa hiari haiwezekani, Rais anaweza kutoa agizo (executive order) na kutaka wachagga waachie ngazi na wakae pembeni kwa angalau miaka mitano ili watu wa makabila mengine wapate nafasi. Hili linaweza kuwahusu Wanyakyusa na Wahaya vile vile. Kama hawatafanya kwa hiari tunaweza kufanya kwa nguvu hata kwa kutunga sheria maalum ya kuwalazimisha.

kwa hiyo na rais aruhusu waajiri wakwere, wamasai, waha, wahadzabe na wengineo ambao hawana qualifications ili tu kuwaeliminate wachagga? Will be total deflection from the right path. Mapinduzi hayaji kwa siku moja.
 
tukimaliza hapo tutasema wapemba wasipewe vibali vya kufanay biashara kwa miaka mitano .......manake wanachukua kazi zote
 
Mtu anaweza kusearch kupata the original "A Modest Proposal" essay iliyoandikwa 1729 kule Ireland. Nilipoisoma hii miaka michache iliyopita katika Writing Class nilijikuta nafikiria siku moja na mimi niendike kitu kama hiki. This is my first attempt.
 
Mtu anaweza kusearch kupata the original "A Modest Proposal" essay iliyoandikwa 1729 kule Ireland. Nilipoisoma hii miaka michache iliyopita katika Writing Class nilijikuta nafikiria siku moja na mimi niendike kitu kama hiki. This is my first attempt.

UNREALISTIC PROPOSAL though good attempt
 
Mwanakijiji,

..actually kuna mpango ambao unakaribiana na mapendekezo yako ulitekelezwa ktk sekta ya ELIMU.

..mpango huo wa serikali ulijulikana kama QUOTA-SYSTEM ktk kuchagua wanafunzi wanaokwenda shule za sekondari za serikali.

..quota-system iliweka pass-mark ya chini ktk mikoa ya pembezoni, kulinganisha na pass-mark ktk mikoa ya kilimanjaro,kagera,mbeya,..

..lengo lilikuwa kutoa nafasi zaidi kwa wanafunzi wanaochaguliwa kwenda sekondari toka mikoa ya pembezoni.

..ilifika kipindi watoto wa kichaga wakalazimika kubadili majina na kuhamia mikoa mingine ili kupata nafasi kusoma ktk sekondari za serikali.

NB:

..hii uliyoleta hapa kwa kweli ni CHANGAMOTO. nategemea watu watakuja na short-term pamoja na long-term proposals za jinsi ya kushughulikia tatizo hili.
 
toa pendekezo ya njia ambayo atumie basi......

ianzishwe directorate ya kuajiri kwa ajili serikali na agency zake zote. Nafasi zote za kazi ziwe zinapelekwa kwenye hiyo directorate ambayo itazitangaza na kufanya usaili kwa kuhusisha experts from the appropriate unit inayotaka mfanyakazi.
 
ianzishwe directorate ya serikali na agency zake zote. Nafasi zote za kazi ziwe zinapelekwa kwenye hiyo directorate ambayo itazitangaza na kufanya usaili kwa kuhusisha experts from the appropriate unit inayotaka mfanyakazi.


Mama kwenye hiyo directorate Wachagga wataruhusiwa kuomba nafasi? Je Mchagga ataruhusiwa kuwemo katika nafasi za uongozi wa hiyo directorate? Binafsi nisingependa wachagga wawemo...
 
Duh kweli Chacha Wangwe kawashika vibaya.....yaani yote haya ni mwendelezo wa hoja yake

my take:
Chadema hawana budi kushughulikia hoja za Wangwe badala ya kukaa kwenye comfort zone huku wakijiburudisha na kujiliwaza kwa hoja kama hii ya mwanakijiji ya eti "wachaga wanabaguliwa kwa kuwa wao ni wachagga tu" na si kwamba wao wachagga wanawabagua wasio wachagga kwa kuwapendelea wachagga wenzao
 
Duh kweli Chacha Wangwe kawashika vibaya.....yaani yote haya ni mwendelezo wa hoja yake

my take:
Chadema hawana budi kushughulikia hoja za Wangwe badala ya kukaa kwenye comfort zone huku wakijiburudisha na kujiliwaza kwa hoja kama hii ya mwanakijiji ya eti "wachaga wanabaguliwa kwa kuwa wao ni wachagga tu" na si kwamba wao wachagga wanawabagua wasio wachagga kwa kuwapendelea wachagga wenzao

vipi kuhusu makabila mengine, hawafanyi hayo au wachagga ndio wanafanya hivyo zaidi? empirical data zitasaidia kweli maana kusema kuwa "wao wachagga wanawabagua wasio wachagga kwa kuwapendelewa wachagga wenzao" si hoja ndogo.

Huoni kwamba kuwaondoa wachagga katika nafasi za uongozi kutasaidia sana kuondoa hilo tatizo unaloliona.?
 
Mama kwenye hiyo directorate Wachagga wataruhusiwa kuomba nafasi? Je Mchagga ataruhusiwa kuwemo katika nafasi za uongozi wa hiyo directorate? Binafsi nisingependa wachagga wawemo...

ToR za directorate ziwe brainstormed openly na mapendekezo yawe open. By the way wanaweza fanya needs assessment ili kujua hiyo directorate ifanye nini kwa kanuni zipi. Na Director au wafanyakazi wa hiyo directorate wasiwe wachaga, wanyakyusa, wasukuma, wapare wala wahaya. Watoke kwenye minority and under-represented groups. Ila makabila yapewe fursa sawa katika kuomba kazi.
 
A MODEST PROPOSAL

Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna vumbi la chuki, fitina, wivu, kisasi, na hisia za kibaguzi dhidi ya jamii ya Wachagga nchini. Kuna kila dalili kuwa jamii ya Wachagga nchini siyo tu inaanza kutengwa lakini uwepo wake katika nafasi mbalimbali za uongozi inazua hoja ya ukabila kwa haraka zaidi yawezekana kuliko kabila jingine lolote nchini. Katika Tanzania yetu, wachagga wameanza kunyoshewa kidole siyo kwa siri tena bali kwa wazi kabisa tena na watu ambao wakati mwingine hawapati hata kigugumizi.

Ubaguzi huo msingi wake mkubwa ni idadi ya wachagga katika nafasi mbalimbali za uongozi na hasa kuhusiana na elimu yao. Kuanzia mara tu baada ya uhuru jamii ya wachagga mojawapo ya jamii ambayo watu wake wengi wamesoma sana na kufanikiwa kielimu na kiuchumi imekuwa ikinyoshewa kidole cha kupendelewa.

Mtu yeyote ambaye anaweza akafanya uchambuzi yakinifu hatoshangaa kukuta wataalamu wa kichagga katika nafasi mbalimbali za uongozi au taaluma nchini. Kwenye vyuo vikuu, kwenye idara za serikali na hata kwenye taasisi binafsi kumejaa watu wenye asili ya mkoa wa Kilimanjaro na hususan watu wa jamii ya Kichagga.

Endapo itatangazwa nafasi yoyote ya kitaalamu usishangazwe ukiona kuwa waombaji wengi wana majina ya "Kichagga".

Ni kwa sababu hiyo basi kuna kila dalili kuwa kutokana na wingi wao katika nafasi muhimu na vyeo mbalimbali (hata ndani ya Jeshi la Polisi) Wachagga siyo tu ni wengi lakini wanaonekana kufanikiwa zaidi. Hili ni tishio kwa baadhi ya watu. Ni tishio kwa watu ambao hawako tayari kuangalia jitihada za watu katika kufanikiwa kwao na matokeo yake kushutumu ukabila kila idadi ya Wachagga kwenye kitengo fulani inazidi mmoja.

Ushauri wangu ni kuwa, kwa vile Wachagga wameshasoma sana na kuendelea katika biashara karibu mikoa mingi nchini. Na kwa vile wanaendelea kufanikiwa pia katika nafasi mbalimbali za uongozi nchini, basi itakuwa vizuri kama watajitolea kuachilia nafasi hizo ili kuwapa nafasi watu wa makabila mengine.

Kwa vile ni wao wanaonekana kulalamikiwa kutokana na mambo ya kifisadi aidha kwa moja kwa moja au kwa kuashiria basi ni vizuri wawape watu wengine nafasi hizo hata kama watu hao hawajasoma sana. Hii yote itakuwa ni katika kudumisha mshikamano, umoja na udugu wa Taifa letu.

Endapo Wachagga wataachilia nafasi mbalimbali kama UCEO, Ukurugenzi, Ukuu wa Idara n.k watasababisha watu wawapende na kuwakubali kuwa ni wazalendo wa kweli. Sitoshangaa kuwa ndugu zetu wa Jamii ya Kichagga wakikaa pembeni, basi ufisadi utakoma serikalini, idara zitaongozwa na watu wazuri, na mara moja na daima Tanzania itaanza kukua katika uongozi.

Kwa kupendekeza nashauri wabunge wote ambao ni Wachagga au wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro kuachia ngazi mara moja ili watu wa makabila mengine wapewe nafasi hizo. Siyo wao tu bali pia wabunge ambao wameoa au kuolewa uchagani vile vile wafuate nyazo hizo.

Wakishamaliza hao, wakuu wote wa idara za serikali ambao wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro na hasa wa jamii ya kichagga (wamarangu, wamachame, wa Rombo, na wa Kibosho) na wao waamue kuachilia nafasi hizo kwa ndugu zao Wamakua, Wamwera, Wa Ndali, Wadigo n.k Katika hili Wapare hawahusishwi.

Tukishamaliza wakuu hao wa idara za serikali ningependekeza madaktari wote wenye kumiliki hospitali binafsi ambao ni wachagga au wameoa/kuolewa uchagani na wenyewe waamue kuingia ubia na watu wa makabila mengine kama wangengereko, wambuu, na wanjiro ili hayo makabila madogo na wenyewe wapate nafasi ya kujifunza fani hizi muhimu.

Zaidi ya yote, majaji na mahakimu wote ambao wana asili ya Uchaggani na wenyewe waamue kujitoa katika nafasi hizo kwani wingi wao pia unaonekana sana na hivyo kuwa kikwako kwa watu wa makabila mengine kufanikiwa zaidi katika nyanja ya sheria. Kwanza kabisa wale majaji wa Kichagga wa mahakama ya Rufaa na Mahakama Kuu wawe wa kwanza kuweka manyanga chini.

Katika kufanya hivyo jamii ya Watanzania ambao inaona ukabila wa wachagga katika sehemu nyingi itaridhika kwani kwa mara ya kwanza tutakuwa tumeshughulikia chanzo cha matatizo yetu mengi.

SOUNDS LIKE "THE BUTIAMA DECLARATION"
Hizo nafasi hao wachagga walipewa na wachagga?
Haya naona kwasababu umesha mention na wale walio oa ama kuolewa uchaggani!
Vipi kuhusu watoto wao...? Na wao watachaguwa kabila gani?
Kama utasema kabila la baba ndilo wachaguwe...Then kwanini useme wale walioowa uchaggani na wao ni wachagga kama watoto wao hawataitwa wachagga?
Hii habari ni nzuri kwa RA...Ila si kwa wazalendo.
Na nilipsema mpango mzima wa kuwachafuwa wachagga ni Mkapa na Nyerere utabisha?
Kwamba hata pesa za EPA na kila kitu trend haijionyeshi?
Na kabla hujaanza hayo mambo ya kusema watu waachiwe...Na mimi nakwambia hivi...Kuachiana kwa uongozi kulikoletwa na mwalimu kwa mtiririko wa Mwinyi na Mkapa ni wa kupigwa vita na ccm ilikufa na mwalimu alipokufa!
Nchii hii itajengwa na wazalendo na si MA RACIST NA WAHAMIAJI HARAMU!
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom