Je, utendaji kazi wa Rais Magufuli ndiyo umewafanya CHADEMA wakumbuke tume sio huru au ni kuweweseka kisiasa?

Idugunde

JF-Expert Member
May 21, 2020
6,273
6,637
Miaka karibu yote tangu kuanza kwa vyama vingi Chadema na vyama vingine vya upinzani wamekuwa wakishiriki uchaguzi na wamekuwa wakipata ushindi kwa ngazi mbali mbali kama vile ubunge na udiwani.

Lakini sio siri walikuwa wanakichachafya CCM kwenye kampeni hasa kwa kutumia madhaifu ya kutopambana ufisadi na ubadhirifu.

Natolea mfano tu Uchaguzi wa 2010 Chadema pamoja na kutokuwa na washirika wa Ukawa waliitikisa CCM hasa ikuchukuliwa maanani ajenda ya ufisadi iliwabeba sana. Walipata madiwani wengi na karibu miji mikubwa kama Mwanza, Mbeya na Arusha walivuna madiwani wengi na wabunge. Je, baada ya uchaguzi wa 2010 hawakubaini kuwa tume sio huru?

Kwa mujibu wa katiba ya JMT ibara ya 74(7) tume ya uchaguzi ni chombo huru ambacho kinatakiwa kifanye kazi kwa mujibu wa katiba na sheria.

Baada ya uchaguzi wa 2015 na JPM kuwa Rais mambo yamebadilika. Natoa mfano tu, ufisadi na ubadhirifu umedhibitiwa. Na kwa sababu hii serikali imetekeleza miradi mingi yenye tija kwa taifa kwa muda mfupi. Sioni umuhimu wa kuitaja kila mwanachama wa Chadema na mpinzani anaifahamu.

Kwa mantiki hiyo wapinzani wamekosa ajenda ya kuikosoa serikali ni hii dhahiri hawawezi kushinda urais na hata ubunge na udiwani ni kwa nadra sana.

Sasa wao wanadai eti tume ya uchaguzi sio huru. Kwa nini madai haya hawayakuyaleta toka hata 2010? Au ni kwa sababu CCM chini ya JPM imewakaba kila kona na hawapumui, kwa utendaji kazi mzuri na unaokubalika.
 
Mkuu wanaweweseka mno, hilo liko wazi halihitaji Utaalam wowote au PhD ya fani yoyote ndiyo ulibaini.
 
Jibu hoja JPM amewabana mbavu mnasingizia tume sio huru? Hamna mahala pa kuikosoa serikali.
Aliyebamwa mbavu ni yule aliekosa ajira sababu baadhi ya wenye mitaji wamefunga shughuli zao au serikali kutoajiri watu wengi.
Aliebanwa mbavu ni yule katika kipindi cha miaka mitano hakupewa nyongeza ya mshahara.
Aliebanwa mbavu ni yule alieshindwa kulipa mkopo wa benki kwa sababu ya mzunguko wa fedha upo ICU.
 
Aliyebamwa mbavu ni yule aliekosa ajira sababu baadhi ya wenye mitaji wamefunga shughuli zao au serikali kutoajiri watu wengi.
Aliebanwa mbavu ni yule katika kipindi cha miaka mitano hakupewa nyongeza ya mshahara.
Aliebanwa mbavu ni yule alieshindwa kulipa mkopo wa benki kwa sababu ya mzunguko wa fedha upo ICU.
Out of point. Hayo masuala ya kiuchumi yaanzushie uzi. Na watu hawadai nyongeza ya mshahara bali ongezeko la mshahara wa kima cha chini
 
Out of point. Hayo masuala ya kiuchumi yaanzushie uzi. Na watu hawadai nyongeza ya mshahara bali ongezeko la mshahara wa kima cha chini
Wewe ulifikiri Chama cha kisiasa kama Chadema kinapodai Tume huru ya uchaguzi,ni Chadema imebanwa,kumbe Chadema inawakilisha mawazo ya watu walio wengi wasiopenda bao la mkono.
Na ukishapata washindi kwa bao la mkono usitegemee kukuza uchumi wa wengi.
 
Miaka karibu yote tangu kuanza kwa vyama vingi Chadema na vyama vingine vya upinzani wamekuwa wakishiriki uchaguzi na wamekuwa wakipata ushindi kwa ngazi mbali mbali kama vile ubunge na udiwani.

Lakini sio siri walikuwa wanakichachafya CCM kwenye kampeni hasa kwa kutumia madhaifu ya kutopambana ufisadi na ubadhirifu.

Natolea mfano tu Uchaguzi wa 2010 Chadema pamoja na kutokuwa na washirika wa Ukawa waliitikisa CCM hasa ikuchukuliwa maanani ajenda ya ufisadi iliwabeba sana. Walipata madiwani wengi na karibu miji mikubwa kama Mwanza, Mbeya na Arusha walivuna madiwani wengi na wabunge. Je, baada ya uchaguzi wa 2010 hawakubaini kuwa tume sio huru?

Kwa mujibu wa katiba ya JMT ibara ya 74(7) tume ya uchaguzi ni chombo huru ambacho kinatakiwa kifanye kazi kwa mujibu wa katiba na sheria.

Baada ya uchaguzi wa 2015 na JPM kuwa Rais mambo yamebadilika. Natoa mfano tu, ufisadi na ubadhirifu umedhibitiwa. Na kwa sababu hii serikali imetekeleza miradi mingi yenye tija kwa taifa kwa muda mfupi. Sioni umuhimu wa kuitaja kila mwanachama wa Chadema na mpinzani anaifahamu.

Kwa mantiki hiyo wapinzani wamekosa ajenda ya kuikosoa serikali ni hii dhahiri hawawezi kushinda urais na hata ubunge na udiwani ni kwa nadra sana.

Sasa wao wanadai eti tume ya uchaguzi sio huru. Kwa nini madai haya hawayakuyaleta toka hata 2010? Au ni kwa sababu CCM chini ya JPM imewakaba kila kona na hawapumui, kwa utendaji kazi mzuri na unaokubalika.
Nashangaa mkuu umekuwa msahaulifu kiasi hiki. Rejea mchakato wa katiba na chaguzi zilipita hiki kimekuwa kilio cha vyama mbadala. Nadiriki kusema kwa hili UMEKURUPUKA.
 
Wanaweseka vibaya sana.

Ww ndio hizi id mpya zilizojazwa humu mitandaoni na ccm kuja kupiga propaganda mfu kuelekea uchaguzi? Wenzako humu ndani wanakimbia maana hizo propaganda ni kwa ajili ya wazee.
 
Mkuu, hata marehemu kabla hajakata roho huweweseka sana tuwavumilie tu ndugu zetu wapo kwenye hatua za mwisho.
Inabidi huyu marehemu mtarajiwa aandike WOSIA mapema mkuu.

Maana muda si mrefu tutaanza kuimba wimbo wa MSONDO NGOMA.
 
Wewe ulifikiri Chama cha kisiasa kama Chadema kinapodai Tume huru ya uchaguzi,ni Chadema imebanwa,kumbe Chadema inawakilisha mawazo ya watu walio wengi wasiopenda bao la mkono.
Na ukishapata washindi kwa bao la mkono usitegemee kukuza uchumi wa wengi.
Nafikiri ungejibu hoja yangu kwanza 2010 walipata wabunge wengi na madiwani bila ukawa. Mbona hawakusema tume sio huru?
 
Back
Top Bottom