Je upoje kitandani??

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,778
Nazima Tv, halafu nakwambia kitu!! Picha kwa hisani ya inmagine


Je unadhani wewe ni mwanaume mzuri kitandani? Hapa kuna maswali kwa ajili yako.
Je ni mara nyingi mke wako huwa anakuhitaji kwa ajili ya tendo la ndoa?
Je, kila unapofanya mapenzi yeye hufika kileleni? Je unauhakika jinsi ulivyo mzuri kitandani
Basi jibu maswali yafuatayo kwa uangalifu na uhakika bila kudanganya na angalia mapendekezo ya majibu ambayo yapo kila baada ya swali.

Kama ni mwanamke basi unaweza kumuonesha mume wako haya maswali ili ajibu ajipime yupo wapi katika kukuhakikishia unapata raha inayotakiwa kitandani siku zote.

Je, ni mara ngapi huwa unajisifu sana kwamba wewe ni mzuri kitandani?
(a) Kamwe sijisifu
(b) Mara chache
(c) Kila wakati
Watu ambao hujisifu kwamba ni wazuri kitandani mara nyingi hawajiamini. Suala la tendo la ndoa ni maada sensitive sana kwa wanaume, hivyo kujisifu inawezekana ni kujaribu kufunika ukweli.

Je, nini mtazamo wako kuhusu usafi?
(a) Nipo kawaida, naoga, najinyoa ndevu na kutumia vipodozi vya wanaume na kuvaa nguo safi
(b) Kuna siku siogi, pia naweza kuvaa nguo moja hata mara mbili
(c) Nipo makini mno, naosha mikono kila wakati na sipendi kabisa kugusana na mtu mwingine asije nichafua
Kuwa msafi siku zote ni kitu kizuri sana. Wanawake wapo sensitive sana na kile wananusa kuliko wanaume.
Hii ina maana kwamba harufu mbaya huweza kumuathiri mwanamke kuliko mwanaume. Ni muhimu kuoga kila mara na kuvaa nguo safi, ingawa kuwa msafi kupitiliza kunaweza kuzima hamu ya mapenzi kwa mpenzi wako kwani huwezi kubusu kila sehemu kwa kuogopa kuchafuka.

Je, mwonekano wako upoje? Umepinda au umenyoka?
(a) Imara na mara zote mgongo umenyooka
(b) Imara sana labda niwe nimechoka basi mgongo huinama
(c) Kila wakati natembea nimeinama na kupinda mgongo
Mwonekano (posture) ovyo siku zote unahusiana na Uvivu. Na kama ni mvivu maana yake wewe si mzuri kitandani pia.
Wanaume wenye posture nzuri siku zote huwa wanasimama wima na mabega yakiwa sawa bila kuinama na pia ni wanaume ambao hupenda ku-improve vitu vingi katika maisha mojawapo ni suala la kitandani. Wanaume wenye mwonekano (posture) nzuri ni wazuri kitandani pia.

Je, ni mara ngapi unaongea na mikono
(a) Sifanyi kabisa
(b) Nafanya kila ninapoongea
(c) Mara moja au mbili kila ninapoongea
Wanaume wanaongea huku mikono nayo ikisaidia mara nyingi ni wabunifu na wafikiriaji wazuri. Hujitahidi sana kuhakikisha wanapofanya mapenzi kunakuwa na matokeo mazuri. Kama una mwanaume wa jinsi hii basi utafurahia kitandani maisha yako yote hadi uzeeni.

Je, wewe ni mbunifu kiasi gani kitandani?
(a) Nafanya kwa utaratibu uleule kila siku miaka Nenda miaka rudi
(b) Ninafanya tofauti kidogo angalau baada ya muda
( c) Najitahidi kuwa na kitu kipya angalau kila ninapofanya mapenzi
Kuwa bored ndiyo sababu kubwa ya uhusiano wa mapenzi kuwa ovyo na hata hamu kwisha kabisa. Kujaribu kitu kipya pamoja na mikao tofauti wakati wa kufanya mapenzi husaidia kitanda kuwa cha moto kila mara.
Wapo wanandoa ambao wapo kwenye ndoa zaidi ya miaka 60 na bado wana enjoy mapenzi.

Je, kuna umuhimu wowote kwako kwa mke kufika kileleni?
(a) Huwa sijali afike au asifike, ni kama hainihusu
(b) Ni vizuri akifika kileleni
(c) Nahusika sana na napenda afike kileleni na pia namsaidia kwa kiasi kikubwa kuhakikisha anafika kileleni
Kufanya mapenzi kuzuri kunategemea sana jinsi ya kutoa na kupokea kati ya wahusika. Wanaume wengi wao ni rahisi sana kufika kileleni kuliko wanawake wakati wapo kitandani. Wanawake ni viumbe wa hisia hivyo huhitaji muda zaidi ili kuweza kufika kileleni. Ingawa wanawake wengi hawapowazi kuongelea hili, bado kufika kileleni ni kitendo kinachowapa kuridhika vizuri na tendo la ndoa.
Hivyo kama huwa unahakikisha anafika kileleni basi wewe ni mwanaume mzuri kitandani.

Je, ni mahali gani unamtumia kwa ajili ya tendo la ndoa?
(a) siku zote ni kitandani kwetu chumbani
(b) Chumbani sehemu yoyote, chini au kitandani
(c) Mahali popote ambapo tunaweza
Kama kunakitu kinatakiwa kuepukwa kwa nguvu zote basi ni ile kuwa na mazoea ya kuwa na sehemu au utaratibu mmoja wa kufanya mapenzi miaka Nenda rudi. Jaribu kuwa na sehemu tofauti za kufanya mapenzi, mnaweza kusafiri au kwenda camping au sehemu yoyote.
Hawezi kusahau kumbukumbu za hizo sehemu.

Je, unapokuwa kwenye tendo la ndoa huwa unasimamamisha kwa muda gani?
(a) Dakika mbili au pungufu
(b) Kama dakika 15 hivi
(c) Hadi saa nzima kama kuna umuhimu
Hakuna ubishi uume uliodinda husaidia kumsisimua mwanamke wakati wa kufanya mapenzi. Wakati mwingine mwanamke hukata tamaa kama akijisikia wewe husisimki na matokeo yake wote mnaambulia sifuri.
Ni ukweli pia uume uliosimama na kudinda vizuri huwezi kumpa mwanamke msisimko ambao huwezesha kumfikisha kileleni.

Je, ni muda kiasi gani huwa unatumia kumuandaa mpenzi wako
(a) Sina huo muda
(b) Dakika tano hivi
(c) Hadi nihakikishe yupo tayari au amesisimka vya kutosha kiasi cha yeye kutaka.
Kama wote tunavyojua maandalizi (foreplay) ni muhimu mno kwa ajili ya tendo la ndoa.
Bila maandalizi tendo la ndoa halina ladha yoyote zaidi ya kuumizana.
Kama huwa hufanyi maandalizi yoyote hapo ni dhahiri kwamba haitawezekana kwa mkeo kufika kileleni na hatafurahia inapofika muda wa kwenda kitandani.

Na kama unatoa muda wa kutosha kwa wajili ya foreplay basi atakuwa anasubiri kwa hamu kubwa kusikia muda wa kitandani umefika.
Pia ni vizuri kufahamu kwamba mwanaume mzuri ni yule ambaye hata baada ya kumaliza tendo la ndoa si mtu wa kukurupuka na kutoa uume wakati mke hajamruhusu kwani utamu wa tendo la ndoa kwa mwanamke ni wa muda mrefu zaidi hivyo ni vizuri kubaki ndani zaidi ya dakika 10.


Je, ni mara ngapi unafanya mapenzi kwa kushtukiza?
(a) Si rahisi na kawaida
(b) Mara moja kwa mwaka
(c) Mara kwa mara tunapotaka kufanya mapenzi
Kuna raha yake kwa mwanamke kufanya mapenzi kwa kushtukiza. Utaratibu wakati mwingine huwa una bore, ni kama mazoea. Sex ya kushtukiza wakati mwingine huleta kumbukumbu nzuri zaidi na kuwa enjoyable.
Wanawake huwafurahia wanaume ambao huwapa kile wanatarajia linapokuja suala la kitandani.
Ukiwa mbunifu na mwanaume mwenye utundu kitandani basi mkeo atakushukuru na kukupenda zaidi kwa sababu unampa raha kamili
 
Haya bana kezi kwenu kulinda heshima kwenye ndoa na kwenye mahusiano
 
Nimeipenda hiyo, naamini wanaume wenye ndoa zao wakisoma hii lazima wake zao wafurahie tendo takatifu. Binafsi najivunia wangu ana sifa zote zinazofaa.
 
Mi naamini nampa mwenza wangu kilicho bora zaidi kuliko mtu yeyote yule, na pia najituma ipasavyo na kuweka ubunifu unaokubalika na maadili ya kitanzania. Na pia naamini kuwa na ndivyo ilivyo kuwa wangu mie naye anafanya kama mimi!
 
Back
Top Bottom