Je, upo uwezekano wa kukariri darasa kwa Mwanachuo?

Naja naja

JF-Expert Member
Sep 13, 2016
747
1,452
Inafahamika kwa ngazi za chini za elimu mathalani elimu ya sekondari mwanafunzi akiona ana mapungufu sehemu anaomba kukariri darasa na anakubaliwa bila tatizo lolote,je jambo hili kwa ngazi ya chuo linawezekana au mpaka mwalimu aamue kukukaririsha darasa kilazima na si wewe mwanafunzi kwa mapenzi yako?

Case yangu nilisoma kwa tabu na baada ya mzazi kufariki nikaishia njiani kielimu kutokana na kukosa mtu wa kunisomesha na sikuona sababu ya kuandika barua ya kusitisha masomo kwa muda maana nilishafanya mwanzoni kisha nika resume bila mafanikio yoyote sasa.

Kwa sasa wametokea baadhi ya ndugu wanataka kuunganisha nguvu kunisomesha na nikimaliza kusoma kuna kazi nzuri ninaweza nikapata hivyo nimeona nikaombe nikariri darasa moja nyuma ili niwe competent enough nisiweze kuharibu kazi ya watu maana hilo darasa japo nimeshalisoma semester zote mbili ila nataka nilirudie maana kipindi kile cha shida nilipunyua punyua kutokana na ugumu wa maisha uliopitiliza.

Nifuate taratibu zipi au nikaongee na dean na mkuu wa chuo kumueleza lengo langu?
 
Yani sijakuelewa, kukariri kama ile ya what is physics unakariri tu bila kujua physics is the study of mattee in relation tu energy au unazungumzia kukariri ipi??
 
Inafahamika kwa ngazi za chini za elimu mathalani elimu ya sekondari mwanafunzi akiona ana mapungufu sehemu anaomba kukariri darasa na anakubaliwa bila tatizo lolote,je jambo hili kwa ngazi ya chuo linawezekana au mpaka mwalimu aamue kukukaririsha darasa kilazima na si wewe mwanafunzi kwa mapenzi yako?...
Soma hivyo hivyo umalize.

Jiamini, hata usome vipi theory bado kazini utaanza kujifunza upya.

Practicality is far from theory.
 
Yani sijakuelewa, kukariri kama ile ya what is physics unakariri tu bila kujua physics is the study of mattee in relation tu energy au unazungumzia kukariri ipi??
Ku carry course mkuu ndio anazungumzia
 
Rudia mwaka mzima sio semester mkuu.

Ila kwa ushauri ikiwezekana anza upya tu chuo kingine wakikukatalia hapo.

Nina ndugu yangu alikuwa ifm, cheti kilikuwa na makarai mengi kwasababu yeye chuoni alikuwa mzee wa bata sana, Baada ya kuona ana gpa ya 3.1 hakufurahi, aliendaa kusoma degree ya pili chuo cha uhasibu arusha (IAA).

Alikaza sana aliachana na michezo yake ya zamani, ikawa ni kitabu na yeye, alitoka na gpa yake ya 4.2. akaunganisha masters mzumbe na huko akapasua fresh, Mwaka jana alipata ajira mwezi wa tano na akaweza kuipata cpa yake mwezi wa 11. yani saizi ana degree yake safi, masters safi, cpa yake na ajira yake.

Kama vp hama chuo mapema tu uende kuanza upya kwengine
 
Rudia mwaka mzima sio semester mkuu.

Ila kwa ushauri ikiwezekana anza upya tu chuo kingine wakikukatalia hapo..
Ndicho ninachotaka kukifanya maana sitaki nianzie nilipoishia bali kurudi mwaka mmoja nyuma.
 
Rudia mwaka mzima sio semester mkuu.

Ila kwa ushauri ikiwezekana anza upya tu chuo kingine wakikukatalia hapo.

Nina ndugu yangu alikuwa ifm, cheti kilikuwa na makarai mengi kwasababu yeye chuoni alikuwa mzee wa bata sana, Baada ya kuona ana gpa ya 3.1 hakufurahi, aliendaa kusoma degree ya pili chuo cha uhasibu arusha (IAA).

Alikaza sana aliachana na michezo yake ya zamani, ikawa ni kitabu na yeye, alitoka na gpa yake ya 4.2. akaunganisha masters mzumbe na huko akapasua fresh, Mwaka jana alipata ajira mwezi wa tano na akaweza kuipata cpa yake mwezi wa 11. yani saizi ana degree yake safi, masters safi, cpa yake na ajira yake.

Kama vp hama chuo mapema tu uende kuanza upya kwengine
Hii comment inanipa nguvu sana
 
Inafahamika kwa ngazi za chini za elimu mathalani elimu ya sekondari mwanafunzi akiona ana mapungufu sehemu anaomba kukariri darasa na anakubaliwa bila tatizo lolote,je jambo hili kwa ngazi ya chuo linawezekana au mpaka mwalimu aamue kukukaririsha darasa kilazima na si wewe mwanafunzi kwa mapenzi yako?

Case yangu nilisoma kwa tabu na baada ya mzazi kufariki nikaishia njiani kielimu kutokana na kukosa mtu wa kunisomesha na sikuona sababu ya kuandika barua ya kusitisha masomo kwa muda maana nilishafanya mwanzoni kisha nika resume bila mafanikio yoyote sasa.

Kwa sasa wametokea baadhi ya ndugu wanataka kuunganisha nguvu kunisomesha na nikimaliza kusoma kuna kazi nzuri ninaweza nikapata hivyo nimeona nikaombe nikariri darasa moja nyuma ili niwe competent enough nisiweze kuharibu kazi ya watu maana hilo darasa japo nimeshalisoma semester zote mbili ila nataka nilirudie maana kipindi kile cha shida nilipunyua punyua kutokana na ugumu wa maisha uliopitiliza.

Nifuate taratibu zipi au nikaongee na dean na mkuu wa chuo kumueleza lengo langu?
Chuo kikuu ni chuo kinachoelekeza kurudia darasa au somo na si mwanafunzi. Ukishafaulu mwaka hakuna kurudi nyuma labda uhame degree.
Kama ulifaulu basi rudi chuo na weka bidii kwenye masomo yaliyobaki.
 
Back
Top Bottom