Fredrick Sanga
JF-Expert Member
- Jan 27, 2011
- 3,153
- 697
- Thread starter
- #41
Sasa wanataka kutunyanganya lake Nyasa. Duhh.
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...udi-kwanza-ndipo-rasimu-ya-katiba-ifuate.html. Tafadhali natafauta maoni ya wana JF kuhusu aina ya muungano au kama hawautaki kabisa. Bofya hiyo page, hakikisha umelog in ili utoe maoni yako.
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...udi-kwanza-ndipo-rasimu-ya-katiba-ifuate.html. Tafadhali natafauta maoni ya wana JF kuhusu aina ya muungano au kama hawautaki kabisa. Bofya hiyo page, hakikisha umelog in ili utoe maoni yako.
Binafsi ningependa serikali moja na kama hili haliwezekani muungano uvunjike...hakuna cha serikali tatu (ambayo ni mzigo na haina faida yoyote kwa Tanganyika ingawa kwa mbali naweza kuikubali shingo upande) wala serikali mbili (ambayo naikataa katakata)
Shirikisho ni nini kwa kiingereza? Nataka nipate literature yake.Ninegepanda kuwe na shirikisho la nchi mbili yaani Zanzibar na Tanganyika. Kila nchi iendeshe mambo yake ya dola na makubaliano ya kushirikiana katika mambo mbali mbali kama vile ulizi, usalama na biasharai.Inavyooekana hivi sasa muungano umekaa kinafiki. Zanzibar wameshakuwa na bendera, Rais, kmkm, Bunge n.k. Tanganyika ina nini?Hatuwahitaji wabunge wa Zanzibar katika bunge la Tanganyika.Mungu Ibariki Tanganyika.
Siku hizi watua wanataka kutumia mabavu tu. yaani liwalo na liwe.Hakuna kitu kizuri kama nchi zilizo jirani na zinazoishi kwa maelewano kuweza kuungana na kuwa nchi moja yenye nguvu, lakini inapotokea kwamba huo muungano ambao ni wa serikali "mbili" unaleta kutoelewana na manung'uniko, basi hapo hapana budi kurudi mezani na hasa kurudi kwa wananchi kuangalia ni muungano gani unaotakiwa.
Mimi binafsi napendekeza kama ni muungano basi uwe ni wa serikali moja tu, vinginevyo hakuna muungano.
Kura ya maoni inahitajika.Hakuna kitu kizuri kama nchi zilizo jirani na zinazoishi kwa maelewano kuweza kuungana na kuwa nchi moja yenye nguvu, lakini inapotokea kwamba huo muungano ambao ni wa serikali "mbili" unaleta kutoelewana na manung'uniko, basi hapo hapana budi kurudi mezani na hasa kurudi kwa wananchi kuangalia ni muungano gani unaotakiwa.
Mimi binafsi napendekeza kama ni muungano basi uwe ni wa serikali moja tu, vinginevyo hakuna muungano.
Lakini pia tunataka shirikisho?Watanzania bara tunahitaji nchi yetu ya TANGANYIKA halafu ndio tuanze kujadili mambo ya muungano