Je Ungependelea Muundo Gani wa Muungano au Hautaki, Piga Hapa

Kwaza nakushukuru kwa kutoa sehemu hii ili tusamue kidogo kuhusu katiba,muungano ni kitu kimoja kizuri sana na mtu yoyote anaekataa muungano huwa haoneshi kukamilika ,lakini jee kwa aina hii ya muungano kweli ni haki kuukubali? Mimi binafsi siupendi tena na nauchukia ndani ya nafsi na sio nauchukia tu la! Bali ninazo hoja za kutoa kama ifuatavyo:- 1.kushindwa kwa serikali kuzitatua kero za muungano kwa mika takriban 41; tokea muungano huu ulipoanza pamekuwa na kasoro mbali mbali ambazo hadi sasa hapana iliyopatiwa ufumbuzi, hii inaonyesha kwamba tukikurupuka kuziingiza tena nchi katika muungano wa aina yeyote hatutofanikiwa na badala yake mmoja atanamiwa na mmoja atafaidi,kero hizi ni kero za kihistoria kwani zilianza muda mfupi baada ya muungano pale mzee karume alipokwenda kwa nyerere kumtaka waondoshe baadhi ya mambo ndani ya muungano na nyerere akajibu "muda bado"na hadi sasa umekuwa mchezo wa mtoto lalalala tu ,hadaa na dhulma ndio matokeo ya muungano. 2.kushindwa kwa wasimamizi wa muungano kuzieleza bayana faida za muungano kwa zanzibar:mikutano mingi ambayo nimekuwa nikihudhuria bado kabisa viongozi wasimamizi wa muungano hawajaeleza hasa ipi ni faida kwa zanzibar katika muungano kwa kipiondui chote cha muungano,ni juzi tu nilihudhuria katika mkutano wa kuwaaga wahitimu wa vyuo vikuu mkoani morogoro wa chama changu ccm, ambapo alialikwa mgeni rasmi mh. Abrahmani kinana pamoja na viongozi wengine kama mh.samia(waziri husika wa muungano),mh. Samia alipewa fursa ya kuzungumza na wananchi kuhusu faida za muungano,faida kubwa aliyoiogelea nikuwa watanganyika sasa wanajua kupika urojo! Ivi hii ni faida ya kuitaja mbele ya wasomi?, faida nyengine akasema kuwa yeye alisoma katika chuo kikuu cha mzumbe na lau si muungano ingebidi kusoma kwaoo zanzibar,huyu haifahamu historia ya zanzibar hasa katika nyanja ya elimu,zanzibar kabla ya muungano ilkuwa nchi ya tatu kwa wasomi katika nyanja zote,wakati huo tanganyika hata kuzaliwa bado. Na faida ya tatu akasema watu tayari wameshachanganya damu, pia hoja hii haina msingi, kuvunjika kwa muungabno kuna tofauti kubwa na kuvunjika kwa ndoa , bado watanganyika ni ndugu zetu lakini kinachodaiwa ni hii sababu ya udhalili kule zanzibar ife. 3.kukosekana kwa hati halali ya muungano hadi sasa: Nchi zozote zinapoungana lazima mkataba wa muungano uwekwe wazi kwa nhi zote na hata kwa raia ili papatikane uhalalai wa muungano huo, zanziba imishi ndani ya muungano kwa miaka isiyopungua 40,lakini dai unavo dai basi hupati maelezo yanayojitosheleza, mwisho wako ni kifungo na kuandaliwa kesi ya uhaini . 4.dhulma za makusudi zilizofanywa dhidi ya zanzibar.,ikiwa nipamoja na kuporwa haki ya kuwa dola kwa maelezo zaidi soma kitabu cha kanisa katoliki na siasa za tanzania bara cha dr. Sivalon, pia soma kwaheri ukoloni kwa heri uhuru cha dr. Mohammed saidi na hata maisha na nyakati za abdulwahid sykes.
 
[sup] kwaza nakushukuru kwa kutoa sehemu hii ili tusamue kidogo kuhusu katiba,muungano ni kitu kimoja kizuri sana na mtu yoyote anaekataa muungano huwa haoneshi kukamilika ,lakini jee kwa aina hii ya muungano kweli ni haki kuukubali? Mimi binafsi siupendi tena na nauchukia ndani ya nafsi na sio nauchukia tu la! Bali ninazo hoja za kutoa kama ifuatavyo:- 1.kushindwa kwa serikali kuzitatua kero za muungano kwa mika takriban 41; tokea muungano huu ulipoanza pamekuwa na kasoro mbali mbali ambazo hadi sasa hapana iliyopatiwa ufumbuzi, hii inaonyesha kwamba tukikurupuka kuziingiza tena nchi katika muungano wa aina yeyote hatutofanikiwa na badala yake mmoja atanamiwa na mmoja atafaidi,kero hizi ni kero za kihistoria kwani zilianza muda mfupi baada ya muungano pale mzee karume alipokwenda kwa nyerere kumtaka waondoshe baadhi ya mambo ndani ya muungano na nyerere akajibu "muda bado"na hadi sasa umekuwa mchezo wa mtoto lalalala tu ,hadaa na dhulma ndio matokeo ya muungano. 2.kushindwa kwa wasimamizi wa muungano kuzieleza bayana faida za muungano kwa zanzibar:mikutano mingi ambayo nimekuwa nikihudhuria bado kabisa viongozi wasimamizi wa muungano hawajaeleza hasa ipi ni faida kwa zanzibar katika muungano kwa kipiondui chote cha muungano,ni juzi tu nilihudhuria katika mkutano wa kuwaaga wahitimu wa vyuo vikuu mkoani morogoro wa chama changu ccm, ambapo alialikwa mgeni rasmi mh. Abrahmani kinana pamoja na viongozi wengine kama mh.samia(waziri husika wa muungano),mh. Samia alipewa fursa ya kuzungumza na wananchi kuhusu faida za muungano,faida kubwa aliyoiogelea nikuwa watanganyika sasa wanajua kupika urojo! Ivi hii ni faida ya kuitaja mbele ya wasomi?, faida nyengine akasema kuwa yeye alisoma katika chuo kikuu cha mzumbe na lau si muungano ingebidi kusoma kwaoo zanzibar,huyu haifahamu historia ya zanzibar hasa katika nyanja ya elimu,zanzibar kabla ya muungano ilkuwa nchi ya tatu kwa wasomi katika nyanja zote,wakati huo tanganyika hata kuzaliwa bado. Na faida ya tatu akasema watu tayari wameshachanganya damu, pia hoja hii haina msingi, kuvunjika kwa muungabno kuna tofauti kubwa na kuvunjika kwa ndoa , bado watanganyika ni ndugu zetu lakini kinachodaiwa ni hii sababu ya udhalili kule zanzibar ife. 3.kukosekana kwa hati halali ya muungano hadi sasa: Nchi zozote zinapoungana lazima mkataba wa muungano uwekwe wazi kwa nhi zote na hata kwa raia ili papatikane uhalalai wa muungano huo, zanziba imishi ndani ya muungano kwa miaka isiyopungua 40,lakini dai unavo dai basi hupati maelezo yanayojitosheleza, mwisho wako ni kifungo na kuandaliwa kesi ya uhaini . 4.dhulma za makusudi zilizofanywa dhidi ya zanzibar.,ikiwa nipamoja na kuporwa haki ya kuwa dola kwa maelezo zaidi soma kitabu cha kanisa katoliki na siasa za tanzania bara cha dr. Sivalon, pia soma kwaheri ukoloni kwa heri uhuru cha dr. Mohammed saidi na hata mai[/sup]sha na nyakati za abdulwahid sykes.
 
Muhimu sana kusambaza link tupate maoni ya kutosha. Sasa ni kwa sisi wana JF ku hyperlink ili mwisho tuwe na kitu cha kuonyesha Wakulu wa Katiba.
 
Inavyoonekana mawazo ya CCM ya serikali mbili yanakataliwa kabisa. Kuna nini jamani
 
kwanza nakupongezeni kwa kuwa na hii forum 2napoweza kuchangia mawazo ye2 though cjajua kama kwa namna yoyote ile yanafikia wahusika au yanaishia hapahapa. ila kwa mtazamo wangu muungano una mapungufu mengi sana na sidhani kama ni jambo la busara kuendelea na mchakato wa katiba ya jamuhuri wakati hili halijakaa sawa tutakuja kuumia baadaye. mimi nadhani muungano ungekuwa wa serikari tatu lakini serikari hizi mbili (serikari ya Tanganyika na serikari ya Zanzibar) zisiwe na maraisi bali kuwe na makamu wa pili wa rais kila upande huku serikari ya muungano ikiwa na rais na makamu wa kwanza wa rais watakao shughulika na masuala ya taifa zima.
 
Nakushukuru mkuu Sanga.
Muungano baina ya nchi mbili huwa unatanguliwa na Political will.
Na nchi mbili zikiungana, basi hutengeneza nchi moja.

Mimi ningependa kama kutakuwa na muungano basi kuwe na nchi moja na Zanzibar na Pemba iwe ni mikoa ya Tanzania.
Binafsi yangu nisingependelea tuungane na Zanzibar, kwa sababu hatuna kitu chochote ambacho tutafaidika kwa kuungana na Zanzibar. Na Tanganyika ningependa irudi kama tutafanya biashara basi tufanye tu biashara, hayo mambo mengine sioni umuhimu wake.

Ila kama umma wa watanganyika na wazanzibari utapendelea kuungana, basi mimi wala sintakuwa na Tatizo ili mradi nchi iwe moja.
Ningependa sana tuungane na Mozambique.
Zanzibar, Kenya, Rwanda Burundi, Congo na Uganda sitaki tuungane nao asilani, wakitaka waungane wenyewe huko huko.
 
Binafsi ningependa serikali moja na kama hili haliwezekani muungano uvunjike...hakuna cha serikali tatu (ambayo ni mzigo na haina faida yoyote kwa Tanganyika ingawa kwa mbali naweza kuikubali shingo upande) wala serikali mbili (ambayo naikataa katakata)
 
Kwa ujumla kuna mawazo mazuri mno humu amboyo yatafanya mchakato uwe yakinifu.
 
Hali ni tete, naona mwelekeo wa kuvunja muungano ni mkubwa. Sijui nini kifanyike?
 
Cha msingi ni kwamba tunakubaliana kwamba kuna haja ya kuangalia kwa makini suala hili.
 
Muungano huu ni upuuzi, hauna faida yoyote kwa wazanzibari wala watanganyika ila kuongeza chuki tu katikajamii. Lau kwamba si muungano makanisa yasengechomwa moto zanzibar, na tanganyika na zanzibar zote zengekuwa dola huru. Wenzetu wakenya hawakuungana na yeyote lakini uchumi wao ni mkubwa kuliko wa tanzania. Wewe kikwete na shein mmekuwa mamwehu kiasi gani hata mfanye udikteta kama huu? hamsikizi wanalotaka wananchi. Nyinyi mtafute la kujibu mbele ya mungu wenu, au nyinyi ni fremason?
 
Back
Top Bottom