tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,511
- 17,747
Nusura sherehe ya harusi ivunjike ghafla bi harusi alipoduwaa na kushindwa kutia sahihi cheti cha ndoa alipomwona mpenzi wake wa zamani kanisani.Bi harusi alionekana kuchanganyikiwa alipomwona jamaa huyo akiingia kanisani alipokuwa akijiandaa kutia sahihi cheti hicho na kwa dakika mbili akasimama kama sanamu.
Ilisemekana kuwa, jamaa alikuwa amepanga kumuoa kidosho huyo lakini akahama mji na mwasiliano kati yao yakakatika.
Ndipo kipusa akaamua kuolewa na bwana huyu wa sasa alipokosa matumaini ya kumpata jamaa huyo tena. Mpenzi wake wa zamani alitokea wakati bwana harusi alipokuwa akitia sahihi cheti cha harusi. Alipomaliza alitaka kumkabidhi bi harusi kalamu lakini akashangaa kuona akiduwaa huku akikaza macho yake kwa jamaa aliyeingia kanisani na ikabidi Pastor amshawishi mwanadada atie sahihi cheti hicho.
Kisa hiki kimetokea huko BUNGOMA, mashariki mwa Kenya.
Je, ungekuwa wewe ndiye bwana harusi ungefanyaje?
Ilisemekana kuwa, jamaa alikuwa amepanga kumuoa kidosho huyo lakini akahama mji na mwasiliano kati yao yakakatika.
Ndipo kipusa akaamua kuolewa na bwana huyu wa sasa alipokosa matumaini ya kumpata jamaa huyo tena. Mpenzi wake wa zamani alitokea wakati bwana harusi alipokuwa akitia sahihi cheti cha harusi. Alipomaliza alitaka kumkabidhi bi harusi kalamu lakini akashangaa kuona akiduwaa huku akikaza macho yake kwa jamaa aliyeingia kanisani na ikabidi Pastor amshawishi mwanadada atie sahihi cheti hicho.
Kisa hiki kimetokea huko BUNGOMA, mashariki mwa Kenya.
Je, ungekuwa wewe ndiye bwana harusi ungefanyaje?