Wapendwa wanajamvi ningependa tujadili mada hii kama inavyosomeka katika kichwa chake. Awali ya yote ni mara nyingi jeshi lapolisi limekuwa na kawaida ya kutangaza mafanikio yake katika kupambana na na wahalifu. Mara kadha, tumeripotiwa na kuoneshwa watu mbali mbali wanaotuhumiwa kuwa ni majambazi (tena majambazi sugu) na kushuhudishwa silaha zilizokamatwa zikihusishwa na watuhumiwa hao.
Binafsi nimekuwa nikijihoji hivi taarifa za polisi zina ukweli usiohojika kama ukweli usiohojika wa biblia na Quran? Je, ni nani mwenye kuthibitisha kwamba silaha zinazotangazwa ni kweli zinahusika na ujambazi na uhalifu unaosemwa?
Hoja zangu zinatokana na ukweli kwamba jeshi la polisi la Tanzania limetuhumiwa mara kadha kwamba lina kawaida ya kubambikia watu kesi, kuanzia za ujambazi hadi mauaji. Watu muhimu na taasisi na asasi kadhaa zimethibitisha haya.
Aidha, mapema miaka ya 2000 hii kuna kijana, dereva wa daladala, aliwahikamatwa pale Maktaba Bar & Guest House eneo la Mabibo akituhumiwa kuwa ni jambazi. Alipofikishwa katika kituo cha Polisi cha Urafiki akaandikiwa ripoti kwamba kakutwa na silaha yeye ni jambazi sugu. Bahati ilioje kwa kijana huyu, alikuwa na mjomba wake, mwenye cheo katika serikali ya Mapinduzi. Huyu afisa akahoji ujambazi wa kijana wake na silaha hiyo aliyokutwa nayo.
Mambo yakawamazito kwa ma-CID walioshika kesi hiyo. Alimanusura wafukuzwe kazi. Wakamsihi kijana (dereva) awasaidie kuwatetea. Basi tuhuma zikafutwa kijana akaachiwa huru.
Na sio shuhuda chache zinazoelezwa kuwahusu polisi na jeshi lao lote. Mathalan, vijana na watu wengi wanaokatwa na polisi kwa tuhuma za uharifu mbali mbali, huwawanaombwa rushwa. Wanaposhindwa kutoa rushwa hutishiwa kubambikizwa kesi za ujambazi wa kutumia silaha.
Sasa, swali ni je, tuendelee kumwamini afande wetu kila anapotuonesha silaha za majambazi? Wasi wasi ni kwamba jeshi hili linataka kujenga kuaminika kwa lazima wakati wananchi waliowengi wameanza kuhoji utendaji haki wa jeshi hili. Aidha, katika miaka ya hivi karibuni tumeona kwa macho yetu jeshi likifanya shughuli zake kwa maagizo ya wanasiasa wa chama kinachotawala.
Baraza laa Congress la Marekani mwaka jana, lililitaja Jeshi la Pol.isi la Tanzania kwamba ni miongoni mwa vyombo vya dola vinavyoongoza kuvunja haki za raia na kufanya mauaji yasiyohojiwa na yeyote katika nchi ya Tanzania.
Kwa hiyo, kwa machache hayo ukiondoa tuhuma za rushwa zinazofanywa na jeshi hilo, itaonekana wazi kwamba sio kila taarifa za jeshi hilo ni za kweli.
NAOMBA KUWASILISHA!
Binafsi nimekuwa nikijihoji hivi taarifa za polisi zina ukweli usiohojika kama ukweli usiohojika wa biblia na Quran? Je, ni nani mwenye kuthibitisha kwamba silaha zinazotangazwa ni kweli zinahusika na ujambazi na uhalifu unaosemwa?
Hoja zangu zinatokana na ukweli kwamba jeshi la polisi la Tanzania limetuhumiwa mara kadha kwamba lina kawaida ya kubambikia watu kesi, kuanzia za ujambazi hadi mauaji. Watu muhimu na taasisi na asasi kadhaa zimethibitisha haya.
Aidha, mapema miaka ya 2000 hii kuna kijana, dereva wa daladala, aliwahikamatwa pale Maktaba Bar & Guest House eneo la Mabibo akituhumiwa kuwa ni jambazi. Alipofikishwa katika kituo cha Polisi cha Urafiki akaandikiwa ripoti kwamba kakutwa na silaha yeye ni jambazi sugu. Bahati ilioje kwa kijana huyu, alikuwa na mjomba wake, mwenye cheo katika serikali ya Mapinduzi. Huyu afisa akahoji ujambazi wa kijana wake na silaha hiyo aliyokutwa nayo.
Mambo yakawamazito kwa ma-CID walioshika kesi hiyo. Alimanusura wafukuzwe kazi. Wakamsihi kijana (dereva) awasaidie kuwatetea. Basi tuhuma zikafutwa kijana akaachiwa huru.
Na sio shuhuda chache zinazoelezwa kuwahusu polisi na jeshi lao lote. Mathalan, vijana na watu wengi wanaokatwa na polisi kwa tuhuma za uharifu mbali mbali, huwawanaombwa rushwa. Wanaposhindwa kutoa rushwa hutishiwa kubambikizwa kesi za ujambazi wa kutumia silaha.
Sasa, swali ni je, tuendelee kumwamini afande wetu kila anapotuonesha silaha za majambazi? Wasi wasi ni kwamba jeshi hili linataka kujenga kuaminika kwa lazima wakati wananchi waliowengi wameanza kuhoji utendaji haki wa jeshi hili. Aidha, katika miaka ya hivi karibuni tumeona kwa macho yetu jeshi likifanya shughuli zake kwa maagizo ya wanasiasa wa chama kinachotawala.
Baraza laa Congress la Marekani mwaka jana, lililitaja Jeshi la Pol.isi la Tanzania kwamba ni miongoni mwa vyombo vya dola vinavyoongoza kuvunja haki za raia na kufanya mauaji yasiyohojiwa na yeyote katika nchi ya Tanzania.
Kwa hiyo, kwa machache hayo ukiondoa tuhuma za rushwa zinazofanywa na jeshi hilo, itaonekana wazi kwamba sio kila taarifa za jeshi hilo ni za kweli.
NAOMBA KUWASILISHA!