Je, unayajua mamlaka ya Jeshi la Polisi kama yalivyoainishwa katika Sheria ya Makosa ya Mtandao (2015)

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
1: Kifungu cha 31: Polisi au watekelezaji wa sheria wanaweza kutoa amri inayoruhusu kuingia, kupekua, au kutwaa vifaa na mifumo ya kompyuta, na kutwaa data au taarifa zilizohifadhiwa kwenye kompyuta

Wanaweza kufanya hivyo iwapo watajiridhisha kwamba kuna sababu za msingi kuamini kwamba mfumo huo wa kompyuta unaweza kutumika kama sehemu ya ushahidi

2: Kifungu cha 32: Kumtaka mtu anayemiliki data au taarifa zinazohitajika katika uchunguzi wa makosa au uendeshaji wa mashauri ya jinai kuweka wazi taarifa hizo

3: Kifungu cha 34: Kumtaka mtu anayemiliki taarifa au data zinazohitajika kwa ajili ya uchunguzi kuweka wazi, kukusanya, au kurekodi mwenendo wa taarifa au data za mawasiliano ya aina fulani, au kumruhusu na kumsaidia afisa wa utekelezaji sheria kukusanya au kurekodi taarifa hizo.

Taarifa au data hizo ni zile zinazoonesha chanzo, mwisho, njia, na muda wa mawasiliano husika

4: Kifungu cha 35: Polisi wanaweza kutoa amri ya kukusanya, kurekodi, kuruhusu au kusaidia mamlaka sahihi kukusanya au kurekodi data au taarifa yenye maudhui yanayoainisha mawasiliano fulani ikiwemo matumizi ya njia za kiufundi, kitaalam au kiteknolojia

5: Kifungu cha 37: Kinaruhusu polisi kutumia kifaa cha uchunguzi katika kukusanya data au taarifa kwa ruhusa ya mahakama, mwanzoni kwa muda wa siku kumi na nne
 
Katika tasnia ambayo inavunja sheria na muongozo wa kazi zao katika kutekeleza majukumu ni polisi, wanaamini katika nguvu na kufata vile walivyoagizwa na mamlaka yake kimadaraka au wenye vyeo vya kisiasa. Ngumu sana kutanguliza hoja au kukwambia sheria inachowaruhusu kufanya kabla ya nguvu.
 
The laws are made to be broken, hasa kwa watu ambao wana level ya chini ya civilization, hizo sheria. In afrika ili kuleta jamii iliyobora sheria kwanza wafunzwe polisi, pia mafunzo yao yasiwe abusive kwa kuwa abuse begets abuse, hili ni swala ambalo niliwahi kujadili kwa kiasi kikubwa na ndugu yangu Justine Kakoko

Ikumbukwe ujuzi wa sheria ni jambo ambalo linawatia wengi matatani, na kutokana na umasikini ni ngumu mtu kukubali kuacha shughuli zake kuendelea kufuatilia kesi ya kutotendewa vyema na askari polisi nk, Laws are laws in softcop kwenye hardcopy life...civilization starts
 
Hiki kifungu kilikosewa, kinatakiwa kufanyiwa marekebisho. Vinginevyo Polisi wasio wema wanaweza kukitumia Vibaya. "Kifungu cha 35: Polisi wanaweza kutoa amri ya kukusanya, kurekodi, kuruhusu au kusaidia mamlaka sahihi kukusanya au kurekodi data au taarifa yenye maudhui yanayoainisha mawasiliano fulani ikiwemo matumizi ya njia za kiufundi, kitaalam au kiteknolojia"
 
Hii sheria ina dosari, imewapa polisi mamlaka makubwa sana kiasi kwamba na kuundoa uhuru kwa raia. Inaweza kutumiwa vibaya na kuviadhibu vyombo vya habari kwa sababu binasfi kwa kisingizio cha usalama wa taifa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom