Je, unaweza kumruhusu partner wako asome sms zako hivi?

mi once in a while lazima nichungulie chungulie simu yake just for "curiosity", na yeye mara kadhaa nimeshamuona aki pitia inbox kwenye simu yangu tena mbele yangu wala hajifichi..!
 
Kama mimi vimeo vyangu viwili vimepigwa pin masaa 24. Ila wife ya kwake iko free. Siku akii lock hiyo kesi itaamuliwa kwa baba mkwe.

hahahaaaa, mkuu bana!,
mi mai waifu huwa hana taimu kabisaaaaa na simu yangu, na hana longolongo na simu yake nikiishika wala hakuna cha kwenda kupokelea simu pembeni na tukiwa wote humuoni yuko anabofyabofya simu!.
ukiona demu anapokelea simu pembeni ujue unaibiwa, stuka mpwa!.
 
Je, unaweza kumruhusu partner wako asome sms zako hivi???? Kama kuna neno moja la msingi ambalo ni msingi wa ndoa yoyote neon hili ni Uangavu (transparency).

Kamusiinafafanua kwamba neno uangavu maana yake ni kuona kitu moja kwa moja hadi ndani, ni kuwa wazi, kuwa huru kimawasiliano na zaidi ni kuwajibika.
Uangavu katika ndoa maana yake kumuona mpenzi wako hadi ndani na kumfahamu vizuri bila shaka maeneo yote ya maisha yenu.

uangavu katika ndoa ni mwanaume au mwanamke kuweza kusoma sms na kupokea simu za mwenzake bila mashaka wala wasiwasi, kusoma emails zilizomo kwenye inbox yake bila wasiwasi wala hofu, Kufahamu akaunti yake benki ina kiasi gani, kuongea siri zako kwake bila mashaka na zaidi kuwa huru kuhakikisha mwenzako anajisikia vizuri kihisia.
Uangavu ni kuwa wewe bila kuwa na aina yoyote ya unafiki.

wanadamu tuliumbwa na uwezo au hamu ya kutaka kumfahamu mwenzako kwa undani hadi usiwe na shaka wala wasiwasi.
Transparency ni process na haiwezi kutokea usiku mmoja tangu umefahamiana na mpenzi wako ingawa wapo watu ambao hata akiwa kwenye mahusiano hataki mwenzake afahamu mambo yake kitu ambacho si lengo la mahusiano.

Uangavu ni kugundua au kupata uvumbuzi wa mambo mbalimbali mapya kwa mume wako au mke wako kwa sababu ya kuwekana wazi.

Bila kuwa na mawasiliano ambayo ni wazi mahusiano yanaweza kukwama.
Jambo la msingi ni wewe kuwa wazi kueleza kilichondani yako au siri zako kwa mwenzi wako (sincerely & straightfowawrd) na zaidi kushirikiana kupeana habari za kila kitu kinachohusu maisha yenu ili kuondoa wasiwasi, hofu na mashaka kwa mwenzako.

Kuficha vitu si jambo la busara na unapokuwa wazi na mwenzako naye anakuwa wazi kwako kwani kuwa wazi ni kufahamiana na kufahamiana ni mahusiano na binadamu tuliumbwa kuwa na mahusiano.

Je, upo wazi kwa mke wako au mume, au mchumba wako kiasi kwamba chake ni chako na chako ni chake?

kama una vimeo huwezi kuthubutu.....
 
Mobile are private entities, naruhusiwa kusoma zake ila simu yangu hairuhusiwi asije pata pressure bure! Akikuta picha za akina Joketi Mwengelo akiwa watupu itakuwaje?
 
Kama mimi vimeo vyangu viwili vimepigwa pin masaa 24. Ila wife ya kwake iko free. Siku akii lock hiyo kesi itaamuliwa kwa baba mkwe.



mhhh halafu mnasema wake zenu wagomvi, kwa hapo mie tungeongea vizuri, kwanini ya mwenzio uwe na mamlaka nayo?...
 
Namtahadharisha sana maihanei wangu hata kusogelea nusu mita simu yangu, hii kwa sababu za usalama wake mwenye. Ya kwake hata sitamani kuiona kila ikiita huwa mapigo ya moya wangu yanazidi sasa nikiishika si nita burst kabisa?
 
Kwenye blue mnaweza msiwe na malumbano lakini unaweza kuta unaliwa na we unakula nini bana tuelezee

Tizama vizuri. Nimesema hatuna malumbano yasiyo na msingi! Hayo ya kula au kuliwa hayawezi kuzuiwa kwa kusoma sms za mumeo/mkeo. Unajua mwanzo tulikuwa tunaweza kugombana kwa vitu vidogo tu. Inaweza kuanzia kwenye phonebook tu akiona majina ya kike inabidi ujiandae kujustfy uwepo wake kwenye phonebook yako!
 
Namtahadharisha sana maihanei wangu hata kusogelea nusu mita simu yangu, hii kwa sababu za usalama wake mwenye. Ya kwake hata sitamani kuiona kila ikiita huwa mapigo ya moya wangu yanazidi sasa nikiishika si nita burst kabisa?

Mpwa umenena jambo. Kabatan ka senks kamepotea ningekugongea. By the way how was your vekesheni at Segerea. Nilitaka kukuwekea dhamana mafisadi wakaniwekea uzibe.
 
Tizama vizuri. Nimesema hatuna malumbano yasiyo na msingi! Hayo ya kula au kuliwa hayawezi kuzuiwa kwa kusoma sms za mumeo/mkeo. Unajua mwanzo tulikuwa tunaweza kugombana kwa vitu vidogo tu. Inaweza kuanzia kwenye phonebook tu akiona majina ya kike inabidi ujianda kujustfy uwepo wake kwenye phonebook yako!

ki ujumla mkianza kuchokonoleana fone, hakutakosa vimalumbano fulani, najiachiaga anasoma sms weeee akichoka ndo utackia hivi SMU ni nani? namwambiaga ni SMU... mana cjamtuma asome sms zangu....
 
Kama mwezi mmoja uliopita jamaa mmoja best wa miaka mingi aliniandikia kwamba alimpa kipigo mkewe cha hali ya juu. Kisa jamaa alitaka kujua email addresses zote za mkewe na pia ampe password ili awe na access nazo na kusoma kila kinachoingia. Mke akagoma kabisa kutoa passwords basi ndiyo kipigo kibaya sana kikamkuta. Na hii issue sidhani kama imekwisha hivyo ama Mume aamue kuacha kufuatilia au Mke aamue kuzitoa hizo passwords, vinginevyo ndoa iko kwenye matata makubwa.

Kama hakuna kibaya chochote cha kumficha mkeo/mumeo basi hakuna madhara ya kupeana ruhusa kuziangalia SMS zenu, lakini kwenye ndoa nyingi hali haiko hivyo. Kwenye ndoa nyingine hata cell phones zinafichwa kabisa Mke hajui mume kama ana mobile phone na vice versa.
 
Mpwa umenena jambo. Kabatan ka senks kamepotea ningekugongea. By the way how was your vekesheni at Segerea. Nilitaka kukuwekea dhamana mafisadi wakaniwekea uzibe.

Vekesheni ilikuwa poa sana, hata sikuchungulia nje kunani, nilikaa natafakari maisha.Ungenipa dhamana siku ile ningekuja kuua mtu bora nilipumzika nilikuwa na hasira sana.
 
mi nafkiri heri kukaa ukijua sasa yeyote mwenzako anawezashika simu yako na kuifanyia chochote, na ujue kuwa ukikataa tu ndo unamuhamasisha kuisoma zaidi=ugomvi lazima unyanyuke kama utaamua kuwa kichwa ngumu.
Be free.
 
Back
Top Bottom