Shadeeya
JF-Expert Member
- Mar 12, 2014
- 48,321
- 115,321
Habarini Wakuu. Leo nataka tupeane mawili matatu ya namna ya kupika kwa kutumia nazi hapa haijalishi nazi iwe ni ile ya kukuna mwenyewe au zile zinazouzwa madukani.
- Je unaandaa tui lako katika sehemu ngapi?
- Au hata kama ni zile tui za kununua madukani unapikaje pikaje au unaliweka kwenye upishi wako wakati gani?
- Je unaungaje wewe mpaka kikawa tayari hicho chakula chako cha nazi?
-Unatanguliza nini kisha unamalizia na nini?
- Pia unaweka nini na nini kwenye huo upishi wako ambao ndani yake unaweka nazi?
Mfano: Mimi nikitaka kupika maharage ya nazi huwa naandaa tui langu katika makundi mawili moja lile zito na lingine la kawaida tu ila chache.
Basi nikishayachemsha na maji yakaiva hayo maharage huwa nakatia kitunguu maji kikishachemkia na maji na kuweka maji kidoogo, yakikauka huwa naweka lile tui la pili ambalo wakati wa kuchuja lilikuwa la kwanza nakoroga kisha naweka chumvi ya saizi yangu baada ya hapo namalizia lile tui la nazi la mwanzo ambalo hapa huwa la mwisho kisha naliacha lichemke kidogo baada ya hapo maharage yanakuwa tayari kwa kuliwa.
Haya wenzangu mnapikaje iwe ni
- Maandazi
- Ubwabwa
- Mboga za majani
- Mchuzi wa samaki
- Dagaa wa nazi
- Njegere
- Makande
- Ndizi
- Viazi vitamu
- Visheti
- Mkate wa Mchele
- Mihogo
- Magimbi
- Maharage
Yaani chakula chochote kile ilimradi ndani yake unaweka nazi.
KARIBUNI TUBADILISHANE UJUZI.
- Je unaandaa tui lako katika sehemu ngapi?
- Au hata kama ni zile tui za kununua madukani unapikaje pikaje au unaliweka kwenye upishi wako wakati gani?
- Je unaungaje wewe mpaka kikawa tayari hicho chakula chako cha nazi?
-Unatanguliza nini kisha unamalizia na nini?
- Pia unaweka nini na nini kwenye huo upishi wako ambao ndani yake unaweka nazi?
Mfano: Mimi nikitaka kupika maharage ya nazi huwa naandaa tui langu katika makundi mawili moja lile zito na lingine la kawaida tu ila chache.
Basi nikishayachemsha na maji yakaiva hayo maharage huwa nakatia kitunguu maji kikishachemkia na maji na kuweka maji kidoogo, yakikauka huwa naweka lile tui la pili ambalo wakati wa kuchuja lilikuwa la kwanza nakoroga kisha naweka chumvi ya saizi yangu baada ya hapo namalizia lile tui la nazi la mwanzo ambalo hapa huwa la mwisho kisha naliacha lichemke kidogo baada ya hapo maharage yanakuwa tayari kwa kuliwa.
Haya wenzangu mnapikaje iwe ni
- Maandazi
- Ubwabwa
- Mboga za majani
- Mchuzi wa samaki
- Dagaa wa nazi
- Njegere
- Makande
- Ndizi
- Viazi vitamu
- Visheti
- Mkate wa Mchele
- Mihogo
- Magimbi
- Maharage
Yaani chakula chochote kile ilimradi ndani yake unaweka nazi.
KARIBUNI TUBADILISHANE UJUZI.