Shadida Salum
Journalist at JamiiForums
- Sep 11, 2020
- 69
- 104
Fainali hiyo ilipigwa kati ya Liverpool ya England na Milan ya Italia kwenye Uwanja wa Olimpiki wa Atatürk huko Istanbul, Uturuki mnamo 25 Mei 2005.
Liverpool, ambaye alikuwa ameshinda mashindano mara nne, hii ilikuwa fainali yake ya sita, na ya kwanza tangu 1985. Milan, ambaye alikuwa ameshinda mashindano hayo mara sita, hii ilikuwa fainali yake ya pili katika miaka mitatu na ya kumi kwa jumla.
Kila klabu ilihitaji kuendelea kupitia hatua ya makundi na raundi ya mtoano kufikia fainali, ikicheza mechi 12 kwa jumla. Liverpool walimaliza wa pili kwenye kundi lao nyuma ya AS Monaco, na baadaye wakaifunga Bayer Leverkusen, Juventus na Chelsea na kutinga hatua ya fainali.
Milan walishinda kundi lao mbele ya Barcelona na wakakutana na Manchester United, Inter Milan na PSV Eindhoven kabla ya kufika fainali.
Milan walichukuliwa kama ndo wenye mchezo ama mabingwa kabla ya mechi na waliongoza ndani ya dakika ya kwanza kupitia nahodha Paolo Maldini. Mshambuliaji wa Milan Hernán Crespo aliongeza mabao mengine mawili kabla ya muda wa mapumziko na kuufanya ubao wa matokeo kusoma 3-0.
Katika kipindi cha pili Liverpool walirudi kwa kasi na kufunga mabao matatu katika dakika sita za kushangaza na kusawazisha ikawa 3-3, kwa jitihada za Steven Gerrard, Vladimír Šmicer na Xabi Alonso.
Ubao uliendelea kusoma 3-3 hata baada ya dakika za nyongeza kumalizika, na mikwaju ya penati ilihitajika kuamua mabingwa.
Matokeo ya mikwaju ya penati yalikuwa 3-2 kwa Liverpool wakati penati ya Andriy Shevchenko iliokolewa na kipa wa Liverpool Jerzy Dudek. Kwa hivyo Liverpool walishinda Kombe lao la tano la ligi ya mabingwa barani Ulaya.
Steven Gerrard alitajwa kuwa 'Man of the Match' katika fainali hizo.
Comeback ya Liverpool ilisababisha fainali hiyo kujulikana kama "Muujiza wa Istanbul", na inachukuliwa kama moja ya fainali kubwa zaidi katika historia ya mashindano hayo.