Je, unapenda kuwa na makalio makubwa bila kutumia dawa yoyote?

ben brancoII

Member
Mar 19, 2017
40
27
images%2B%25282%2529.jpg

Kwa wasichana ambao wanaona kuwa maisha hayawezi kuwa matamu bila kunenepesha makalio, mapaja na matiti yao, ni busara kufanya hivyo kwa njia za asili zisizokuwa na madhara kwa afya zao. Sehemu hizi za mwili zinaweza kunenepeshwa kwa kutumia sayansi ya lishe bora, kunywa maji mengi na mazoezi ya mwili.

Kula vyakula vyenye protini ya kutosha na vyakula vyenye asili ya mimea yaani mbogamboga, matunda, nafaka zisizokobolewa na mafuta yenye asili ya mimea pamoja na kupunguza sukari na chumvi kwenye chakula, husaidia sana katika uimarishaji na unenepeshaji wa misuli ya makalio, matiti na mapaja. Kuepuka ulaji wa nyama yenye mafuta mengi au mazao ya maziwa kama vile siagi na samli pia husaidia.

Mazoezi ya kila siku (asubuhi na jioni) ya kupunguza mafuta katika nyama za tumbo, kufanya kiuno kuwa chembamba na kuimarisha misuli ya mapaja pamoja na makalio ni njia bora ya kumpatia msichana umbo la kupendeza na kunenepesha au kutunisha makalio bila madhara ya kiafya.

Baadhi ya watafiti na wataalamu wa mambo ya urembo wanadai kuwa, kiuno cha msichana au mwanamke chenye uwiano wa 70% ya mzunguko wa mapaja yake (hips circumference) au kipimo cha 0.7 WHR (waist to hip ratio) kinaonyesha afya nzuri ya msichana au mwanamke na kinafanya makalio na mapaja ya msichana au mwanake kuonekana kuwa makubwa.

Mazoezi yanayosaidia katika jitihada za kufikia lengo hili kwa kutumia njia za asili na kwa usalama huku yakiimarisha afya ni pamoja na kuruka juu, kupanda ngazi za nyumba (stair climbing), kuinama, kuchuchumaa pamoja na kuminya au kuchua misuli ya makalio (massage) kila siku.

Ili zoezi la kuchuchumaa lilete matokeo yanayokusudiwa fuata kanuni zifuatazo: Kwanza tambua kuwa lengo lako ni kubadilisha muonekano wa umbo lako kwa njia salama, hivyo basi ni lazima ujitume kufikia lengo hilo. Anza mazoezi ya kusimama wakati miguu yako ikiwa imeachana kiasi cha upana wa kifua chako kisha taratibu kunja miguu yako kwenye magoti ili kuchuchumaa hadi mapaja yawe sambamba na sakafu au ardhi kwa dakika kadhaa kisha panda juu taratibu ili usimame kama mwanzo. Fanya zoezi hili angalau mara ishirini kabla hujapumzika au kubadilisha mtindo wa zoezi.

Fanya mtindo mwingine wa zoezi la kuchuchumaa wakati miguu ikiwa imepishana, weka mguu mmoja mbele kiasi cha umbali wa hatua moja na mguu mwingine uwe nyuma kisha chuchumaa kwa kukunja magoti yote, mguu wa mbele ujikunje na kutengeneza kona yenye 90° digrii na mguu wa nyuma uwe chini kiasi cha nchi 2 hivi juu ya sakafu. Kisha simama na kubadilisha mguu uliokuwa nyuma uwe mbele na kurudiarudia zoezi mara kwa mara.

Zoezi jingine ni lile la kuweka magoti yote na viganja vya mikono yote sakafuni kama mtu anayetaka kusujudu, kisha inua mguu mmoja kwa nyuma wakati goti moja na mikono ikiwa sakafuni. Badilishabadilisha mguu wa kuinua na fanya hivyo kwa dakika 20 kila siku asubuhi na jioni. Lakini pia unaweza kusimama wima na kunyoosha mikono yako yote mbele usawa wa kifua chako kisha ishushe taratibu hadi uguse vidole vya miguu yako kwa mikono yote miwili. Baada ya hapo inuka taratibu hadi usimame wima kama mwanzo na urudierudie zoezi hili kwa dakika 20.

Zoezi jingine linaloweza kusaidia ni lile la kuchua au kiminyaminya misuli ya makalio (massage) kwa dakika 30, asubuhi na jioni kila siku. Zoezi hili huimarisha misuli na kuongeza kiasi cha mzunguko wa damu katika nyama za makalio. Zoezi la kuchua misuli pia linaweza kusaidia katika utunishaji wa matiti kwa wale wanaohitaji matiti makubwa yaliyojaa.

Fanya massage ya matiti kwa kutumia vikanja vyako kila siku asubuhi na jioni na kuchezea chezea chuchu kwa dakika 30, hii itaongeza mzunguko wa damu katika matiti na kupunguza damu ya hedhi lakini pia itasababisha ongezeko la kichocheo cha prolactin na kuimarisha misuli ya matiti. Ili mazoezi haya yalete matokeo yaliyokusudiwa ni lazima yawe endelevu na yaende sambamba na kanuni zingine za afya na urembo kama vile lishe bora, kunywa maji ya kutosha na kuwa na mtazamo chanya katika maisha.

tazama video ya mazoezi hapa na uanze sasa!
JE UNAPENDA KUWA NA MAKALIO MAKUBWA BILA KUTUMIA DAWA YEYOTE? - TIBA ZETU BLOG
 
ndiyo. maana kuna sehemu nilikuta wasichana wanakuja kufanyiwa hizo masaji
 
tako ni tako tu hata liwe kubwa kama jiwe la bismack pale mwanza ziwa victoria na kazi yake ni moja tu
 
Back
Top Bottom