Je, unamfahamu Aziz Ally, aliyechochea kuwepo kwa eneo la Mtoni kwa Aziz Ally?

Crocodiletooth

JF-Expert Member
Oct 28, 2012
18,589
20,895
AZIZ ALI DOSSA KIDONYO-MMOJA WA WAAFRIKA MATAJIRI WAKATI WA UKOLONI NCHINI TANGANYIKA

AZIZ Ali alijitengenezea umaarufu Kutokana na kwamba aliweza kumiliki majumba mengi na magari ya biashara ( yaani malori ya mchanga) pamoja na ya kutembelea na vitu vingine kadhaa, kutokana na kazi yake ya kuwa mtaalamu wa kujenga ( Building Contractor).

Hili jina la Aziz Ali alipewa na watu wa Dar es salaam kwa hisani na wema wake ,alikuwa ni tajiri na Contractor wa kujenga nyumba na mwafrika wa kwanza kununua magari na kujenga nyumba ya vigae na vioo mtoni.

Aziz Ali alikuwa ni mdigo aliyetokea sehemu za Tanga na kuja kuweka kambi mjini Mzizima ( sasa Dar es salaam) mwanzo wa vita kuu ya kwanza ya dunia (1914-1918) akiwa askari katika jeshi la wajerumani na baada ya vita aliajiriwa na Goa mmoja.

Mwajiri wake huyo alipoondoka nchini alimwachia Aziz Ali gari mbili na hizi ndizo alizoanzia kufanyia biashara hapo mwanzo na kufungua kampuni ya ujenzi na kuajiri Mafundi kadhaa. Mwezi wa Ramadhani milango ya nyumba yake ilikuwa wazi kuwahudumia kwa futari mamia ya watu, Temeke imehifadhi jina lake kwa eneo moja la "Mtoni kwa Aziz Ali).

Kwenye Nyumba zake alikuwa akitoa fursa kwa watu kumpa pesa kidogo kidogo kama malipo ya nyumba alizokuwa anawajengea na alikuwa mtu akishindwa kulipa alimpa muda hadi atakapoweza, Nyumbani kwake mwezi mtukufu wa Ramadhani alikuwa akitandika majamvi nje na kufuturisha hadi watu 100 asiowajua wakija wanafuturu na kuondoka.

Nyumba hii hadi leo ipo na sehemu hiyo kando kando ya barabara ya Kilwa na ndipo hapo pakaja kuitwa Mtoni kwa Aziz Ali. Lakini katika sifa yake kubwa sana Aziz Ali alikuwa akifanya ujenzi wa misikiti na kuihudumia misikiti hii ilikuwa miaka ya 1930 na hapakuwa na umeme kariakoo, Misikiti ilikuwa ikitumia karabai kuonea, Aziz Ali yeye alinunua karabai kwa kila msikiti na ikifika magharibi mwanae Hamza alikuwa akizitia mafuta na kuziwasha kisha akizipeleka kila msikiti tayari kwa sala ya Magharibi.

Inapomalizika sala ya Isha alikuwa anapita tena katika ile misikiti kukusanya karabai zake na kurudi nazo nyumbani kwao Mtaa wa Mbaruku na Kongo. Mzee Aziz Ali alikuwa na nyumba nyingi sana Dar es salaam, na ndiyo zilikuwa moja ya utajiri wake, katika nyumba hizo nyumba ya mtaa wa mbaruku na Kongo, nyumba hii ilikuwa moja ya sehemu ambazo harakati za kupigania Uhuru wa Tanganyika zilianzia hapo, nyumba nyingine ilikuwa mtaa wa Kipata kwa Ally Sykes, hapo zamani lilipokuwa duka la baba yake na baraza la wazee.

Nyumba nyingine ilikuwa Stanley Street, kwa Abdul Sykes ,Nyumba hii ilikuwa pia ya Kleist na kulikuwa na duka la vifaa vya ujenzi katika uhai wake. Mzee Aziz Ali alitoa mchango mkubwa sana katika harakati za Uhuru wa nchi hii, kwa kujitolea mali zake na nguvu zake mfanyabiashara aliyemiliki kampuni ya ujenzi wa nyumba nyingi tu mjini mitaa ya kariakoo, yeye alikuwa amezijenga tena kwa kumlipa kidogo na baadaye kummalizia malipo yake kwa makubaliano maalum na wala hajawahi kuishtaki mtu kwa kumcheleweshea malipo yake.

Ndipo Kutokana na ukarimu wake mkubwa wakamwita "Aziz" yaani "kipenzi" ikawa wakimtaja jina wanatanguliza " Aziz" yaani *kipenzi chetu Ali" kiasi kwamba ikapelekea jina la kidonyo kufa kabisa kwa hakika Aziz Ali alikuwa ncha Mungu sana. Alipokufa mwaka 1951 miaka miwili baada ya kifo cha rafiki yake Kleist Gazeti la "Tanganyika Standard "liliandika kifo chake kwa Maneno haya " Aziz Ali the builder of mosques is dead; yaani Aziz Ali mjenzi wa misikiti amefariki".

Alipofariki mzee Aziz Ali, biashara zake ziliendelezwa na mmoja wa watoto zake Dossa Aziz Ali, na hata zile harakati za Uhuru alijihusisha nazo tena kwa undani zaidi, Hii ilikuwa mwanzoni mwa 1950, Mambo yalipamba moto sana kuanzia mwaka huo pale Vijana wazalendo walipoanza kufanya mipango ya kuunda chama cha siasa halisi kupambana na ukoloni wa Muingereza.

Nyumba zilizokuwa anamiliki Mzee Aziz Ali ndizo zikawa nyumba ambazo Nyerere alikuwa akifikia kuanzia mwaka 1952 kila anapokuja mjini kutokea Pugu alipokuwa akifundisha Dossa alikuwemo Katika kuasisi vyombo vyote vya mwanzo vinavyonasibishwa na harakati za kumng'oa mkoloni kama vike TAA na TANU akiwa Afisa na mjumbe mwandamizi aliye na sauti hili sawa hili Fanya, hili wacha, na mambo yakawa hivyo asemavyo.

Dossa kwa kushirikiana na mwanachama mwingine Alexander Tobias walichaguliwa na wenzao wakati fulani wawe makatibu wa pamoja wa muhtasari .harakati ziliposuasua alikuwa hachoki kuwapitia wenzake na kuwakumbusha majukumu waliyopewa akienda kwa mmoja mmoja nyumbani kwake kwa kutumia gari lake na kutaka kujua kulikoni mambo hayaendi ipasavyo.

Katika Sikuwa mwanzo harakati ,chama cha TAA na baadaye TANU havikuwa na uwezo wa kifedha wa kujiendesha mambo yote hata kidogo Tegemeo lao kubwa lilikuwa ni kwa watu kama akina Dossa Aziz, aliyekuwa Mkurugenzi na msimamizi Mkuu wa biashara na mali za babake ,wengine ni Mzee John Rupia ,na wale akina Sykes watatu, Abdul ,Ally na Abbas, ambao baba zao walikuwa na uwezo wa fedha ,wawapige jeki ,wachangie pakubwa.

Habari zinasema ilikuwa ni Dossa Aziz aliyemwomba Nyerere kuacha tena kuvaa kaptula mbele ya wazee, kwani sasa ameshakuwa kiongozi ambaye atakuwa akikutana na watu wazima na hivyo si vizuri kuonekana na Kaptula na Stockings ( zile soksi ndefu mpaka kwenye magoti). Mzee Dossa alifanikiwa katika hilo kwani alimnunulia pia Nyerere suti kadhaa, maridadi katika ile safari yake ya kibali.

UNO Umoja wa Mataifa (wakati ule) ili kupeleka kilimo cha Watanganyika kudai Uhuru.
72870608_2411050098992586_2466625646810365952_n.jpg
 
AZIZ ALI DOSSA KIDONYO-MMOJA WA WAAFRIKA MATAJIRI WAKATI WA UKOLONI NCHINI TANGANYIKA.
AZIZ Ali alijitengenezea umaarufu Kutokana na kwamba aliweza kumiliki majumba mengi na magari ya biashara ( yaani malori ya mchanga) pamoja na ya kutembelea na vitu vingine kadhaa, kutokana na kazi yake ya kuwa mtaalamu wa kujenga ( Building Contractor).

Hili jina la Aziz Ali alipewa na watu wa Dar es salaam kwa hisani na wema wake ,alikuwa ni tajiri na Contractor wa kujenga nyumba na mwafrika wa kwanza kununua magari na kujenga nyumba ya vigae na vioo mtoni. Aziz Ali alikuwa ni mdigo aliyetokea sehemu za Tanga na kuja kuweka kambi mjini Mzizima ( sasa Dar es salaam) mwanzo wa vita kuu ya kwanza ya dunia (1914--1918) akiwa askari katika jeshi la wajerumani na baada ya vita aliajiriwa na Goa mmoja.

Mwajiri wake huyo alipoondoka nchini alimwachia Aziz Ali gari mbili na hizi ndizo alizoanzia kufanyia biashara hapo mwanzo na kufungua kampuni ya ujenzi na kuajiri Mafundi kadhaa. Mwezi wa Ramadhani milango ya nyumba yake ilikuwa wazi kuwahudumia kwa futari mamia ya watu, Temeke imehifadhi jina lake kwa eneo moja la "Mtoni kwa Aziz Ali).
Kwenye Nyumba zake alikuwa akitoa fursa kwa watu kumpa pesa kidogo kidogo kama malipo ya nyumba alizokuwa anawajengea na alikuwa mtu akishindwa kulipa alimpa muda hadi atakapoweza ,Nyumbani kwake mwezi mtukufu wa Ramadhani alikuwa akitandika majamvi nje na kufuturisha hadi watu 100 asiowajua wakija wanafuturu na kuondoka.

Nyumba hii hadi leo ipo na sehemu hiyo kando kando ya barabara ya Kilwa na ndipo hapo pakaja kuitwa Mtoni kwa Aziz Ali. Lakini katika sifa yake kubwa sana Aziz Ali alikuwa akifanya ujenzi wa misikiti na kuihudumia misikiti hii ilikuwa miaka ya 1930 na hapakuwa na umeme kariakoo, Misikiti ilikuwa ikitumia karabai kuonea, Aziz Ali yeye alinunua karabai kwa kila msikiti na ikifika magharibi mwanae Hamza alikuwa akizitia mafuta na kuziwasha kisha akizipeleka kila msikiti tayari kwa sala ya Magharibi.

Inapomalizika sala ya Isha alikuwa anapita tena katika ile misikiti kukusanya karabai zake na kurudi nazo nyumbani kwao Mtaa wa Mbaruku na Kongo. Mzee Aziz Ali alikuwa na nyumba nyingi sana Dar es salaam, na ndiyo zilikuwa moja ya utajiri wake, katika nyumba hizo nyumba ya mtaa wa mbaruku na Kongo, nyumba hii ilikuwa moja ya sehemu ambazo harakati za kupigania Uhuru wa Tanganyika zilianzia hapo, nyumba nyingine ilikuwa mtaa wa Kipata kwa Ally Sykes ,hapo zamani lilipokuwa duka la baba yake na baraza la wazee.

Nyumba nyingine ilikuwa Stanley Street, kwa Abdul Sykes ,Nyumba hii ilikuwa pia ya Kleist na kulikuwa na duka la vifaa vya ujenzi katika uhai wake. Mzee Aziz Ali alitoa mchango mkubwa sana katika harakati za Uhuru wa nchi hii, kwa kujitolea mali zake na nguvu zake mfanyabiashara aliyemiliki kampuni ya ujenzi wa nyumba nyingi tu mjini mitaa ya kariakoo, yeye alikuwa amezijenga tena kwa kumlipa kidogo na baadaye kummalizia malipo yake kwa makubaliano maalum na wala hajawahi kuishtaki mtu kwa kumcheleweshea malipo yake.

Ndipo Kutokana na ukarimu wake mkubwa wakamwita "Aziz" yaani "kipenzi" ikawa wakimtaja jina wanatanguliza " Aziz" yaani *kipenzi chetu Ali" kiasi kwamba ikapelekea jina la kidonyo kufa kabisa kwa hakika Aziz Ali alikuwa ncha Mungu sana. Alipokufa mwaka 1951 miaka miwili baada ya kifo cha rafiki yake Kleist Gazeti la "Tanganyika Standard "liliandika kifo chake kwa Maneno haya " Aziz Ali the builder of mosques is dead; yaani Aziz Ali mjenzi wa misikiti amefariki".
Alipofariki mzee Aziz Ali, biashara zake ziliendelezwa na mmoja wa watoto zake Dossa Aziz Ali, na hata zile harakati za Uhuru alijihusisha nazo tena kwa undani zaidi, Hii ilikuwa mwanzoni mwa 1950, Mambo yalipamba moto sana kuanzia mwaka huo pale Vijana wazalendo walipoanza kufanya mipango ya kuunda chama cha siasa halisi kupambana na ukoloni wa Muingereza.

Nyumba zilizokuwa anamiliki Mzee Aziz Ali ndizo zikawa nyumba ambazo Nyerere alikuwa akifikia kuanzia mwaka 1952 kila anapokuja mjini kutokea Pugu alipokuwa akifundisha Dossa alikuwemo Katika kuasisi vyombo vyote vya mwanzo vinavyonasibishwa na harakati za kumng'oa mkoloni kama vike TAA na TANU akiwa Afisa na mjumbe mwandamizi aliye na sauti hili sawa hili Fanya, hili wacha, na mambo yakawa hivyo asemavyo.

Dossa kwa kushirikiana na mwanachama mwingine Alexander Tobias walichaguliwa na wenzao wakati fulani wawe makatibu wa pamoja wa muhtasari .harakati ziliposuasua alikuwa hachoki kuwapitia wenzake na kuwakumbusha majukumu waliyopewa akienda kwa mmoja mmoja nyumbani kwake kwa kutumia gari lake na kutaka kujua kulikoni mambo hayaendi ipasavyo.

Katika Sikuwa mwanzo harakati ,chama cha TAA na baadaye TANU havikuwa na uwezo wa kifedha wa kujiendesha mambo yote hata kidogo Tegemeo lao kubwa lilikuwa ni kwa watu kama akina Dossa Aziz, aliyekuwa Mkurugenzi na msimamizi Mkuu wa biashara na mali za babake ,wengine ni Mzee John Rupia ,na wale akina Sykes watatu, Abdul ,Ally na Abbas, ambao baba zao walikuwa na uwezo wa fedha ,wawapige jeki ,wachangie pakubwa.

Habari zinasema ilikuwa ni Dossa Aziz aliyemwomba Nyerere kuacha tena kuvaa kaptula mbele ya wazee, kwani sasa ameshakuwa kiongozi ambaye atakuwa akikutana na watu wazima na hivyo si vizuri kuonekana na Kaptula na Stockings ( zile soksi ndefu mpaka kwenye magoti). Mzee Dossa alifanikiwa katika hilo kwani alimnunulia pia Nyerere suti kadhaa, maridadi katika ile safari yake ya kibali.

UNO Umoja wa Mataifa (wakati ule) ili kupeleka kilimo cha Watanganyika kudai Uhuru.
Kazi nzuri
 
Sawa, huko america wako self made billionaires, lakini wapo pia matajiri ambao utajiri wao umerithishwa vizazi na vizazi.
kama akina rockfeller etc

hapa Tanzania wapo akina manji, akina Rostamu kwa mujibu wa maelezo yao.

Kizazi cha huyu jamaa ni kina nani, haiwezekani ukwasi wote huo upotelee kwenye historia.
 
Sawa, huko america wako self made billionaires, lakini wapo pia matajiri ambao utajiri wao umerithishwa vizazi na vizazi.
kama akina rockfeller etc

hapa Tanzania wapo akina manji, akina Rostamu kwa mujibu wa maelezo yao.

Kizazi cha huyu jamaa ni kina nani, haiwezekani ukwasi wote huo upotelee kwenye historia.
Ukwasi umekwenda na Marehemu hao.Nadhani limebakia jina tu pale kwa Azizi Ally.
Mana kwa Utajiri huo uliotajwa hapo kwa miaka hiyo Labda kwasasa familia hii ingekuwa moja ya Matajiri wakubwa Tanzania na Africa Mashariki.
 
Tatizo la matajiri wengi wa kiafrika, utajiri wao unahusishwa na majini.....mwenye mali akifa tu na kila kitu kinakwenda naye.
 
Wapo waafrika waliokuwa na upeo wa mambo kitambo, watu kama kina Marehemu Aziz Ally Ni nadra sana kuwapata katika kizazi hiki cha pesa mbele utu nyuma
 
Ukwasi umekwenda na Marehemu hao.Nadhani limebakia jina tu pale kwa Azizi Ally.
Mana kwa Utajiri huo uliotajwa hapo kwa miaka hiyo Labda kwasasa familia hii ingekuwa moja ya Matajiri wakubwa Tanzania na Africa Mashariki.
Tajiri...
Nimeona mara kwa mara zinakuja post zinazomhusu Dossa Azizi au baba yake Aziz Ali.
Katika miaka ya 1930s babu yangu Salum Abdallah alikuwa na nyumba Mtaa wa Mbaruku, mtaa ambao Aziz Ali alikuwa anaishi.

Kwa ajili hii kwangu mimi ukoo wa Aziz Ali ukawa ni watu nawajua kwa kuwasikia kwanza kisha nikaja kufahamiana na baadhi ya wanae lakini aliyekuwa karibu sana na mimi na katika mapenzi makubwa baina yetu ni Hamza Aziz ambae alipata kuwa Inspector General of Police (IGP) katiika miaka ya 1970.

Dossa Aziz nilikuja kufahamiananae baadae sana na kitu ninachokumbuka alipojulishwa kuwa mimi ni mtoto wa Said Salum akafurahi sana na kunambia kuwa baba yangu alikuwa mtu mpole sana.

Ally Sykes ndiye aliyenipeleka kwake na ndiye aliyenitambulisha kwake.
Nakukaribisheni katika safari yangu na Ally Sykes siku aliponipeleka kwa Waziri Dossa Aziz wakati wa TANU alipokuwa mfadhili mkubwa wa chama wapenzi wake walimpa jina, ''The Bank,'':

''Ilikuwa katika miaka ya 1980 mwishoni siku mimi na Ally Sykes tulipokwenda kumtembelea Dossa Aziz. Wakati ule nilikuwa nafanya utafiti kuandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes kaka yake Ally Sykes. Tulikuwa tuko mbali katika kazi ile na siku moja nikamuomba Ally Sykes anipeleke kwa Dossa Aziz nikamfanyie mahojiano.

Ilikuwa siku ya Jumapili na nilimsubiri Ally Sykes Mbuyuni katika kituo cha basi mimi nikitokea Masaki. Hapa ni barabara ya Ali Hassan Mwinyi zamani ikiitwa (Upanga Road). Huu Mbuyu ulikuwa unaitwa Mbuyu wa Kigwe lakini si wengi walikuwa wanajua jina hili. Jina hili mimi alinipa Mzee Jimpota ambae yeye na baba yangu walikuwa pamoja katika Dar es Salaam ya 1950 na akaniambia kuwa hilo jina la Kigwe ni Mzee Mwinyikhamis Kigwe wa Msasani ambao wote wakijuana toka utoto wao. Mwinyikhamisi Kigwe akitoka kwao ni Msasani kuja kusoma shule ya Kitchwele Government School pamoja na baba yangu, Ally Sykes kaka yake Abdul na vijana wengine wa Dar es Salaam.

Jimpota yeye alikuwa fundi cherehani, siku moja katika mazungumzo ndipo akaniambia kuwa ule Mbuyu waliupa jina wao wakauita, ‘’Mbuyu wa Kigwe.’’

Ally Sykes ainipitia pale na Mercedes Benz yake mpya, nyeusi inang’ara kama kioo. Alikuwa na mama mmoja Mmarekani Mweusi akanitambulisha kuwa ni mwandishi wa ‘’Washington Post,’’ Ally Sykes akipenda muziki na safari kwenda Mlandizi ilikuwa ya raha sana muziki uliokuwa ukitoka katika spika za lile dude haukuwa wa kawaida. Unasikia kila chombo. Tulipofika Mlandizi tukasimama ofisi ya CCM kuuliza nyumbani kwa Dossa Aziz. Nilipata mshtuko mkubwa pale tulipojibiwa kuwa hawamjui Dossa Aziz. Tuliondoka na tukauliza mbele watu wawili, watatu hivi mwisho bwana mmoja akatuelekeza akatuambia tuifuate njia ya majani iliyokuwa pembeni yetu itatufikisha hadi nyumbani kwa Dossa.

Tulimkuta Dossa amekaa barazani kwake ilikuwa kiasi cha saa tatu asubuhi hivi mkononi ameshika radio ya kizamani kidogo na amefungua BBC anasikiliza. Alipomwona Ally Sykes, Dossa aliweka radio yake chini akapiga ukelele, ‘’Ally ndugu yangu karibu karibu…’’ Kwa jinsi walivyosalimiana na mazungumzo yao yalivyokuwa nilijua kuwa wawili hawa hawajaonana kwa miaka mingi. Pale pale Dossa akamuita mkewe akaja pale barazani. Dossa akamwambia, ‘’Huyu ni Ally kaka yake Bwana Mzuri.’’ Nikajakujua kuwa huyu, ‘’Bwana Mzuri,’’ ni Abbas Sykes ambae yeye alikuwa kila akija Dar es Salaam kutoka Ulaya alipokuwa balozi alikuwa lazima aende Mlandizi kumjulia hali Dossa. Baadae Dossa atanieleza mapenzi yake na Abbas yalianzaje na lini.

Ally Sykes akanijulisha kwa Dossa, ‘’Huyu Mohamed, mtoto wa Said,’’ Dossa akauliza, ‘’Said yupi?’’ Jibu likatoka, ‘’Said Popo.’’ Dossa akanipokea kwa tabasamu kubwa kabisa, ‘’Namjua baba yako alikuwa mpole sana…’’ Dossa akaagiza tuchinjiwe mbuzi lakini Ally Sykes akamwambia Dossa hatukuwa na muda. Ally Sykes akamweleza sababu ya mimi kumfuata.

Dossa alizungumza kwa kama saa moja hivi akianza mapinduzi waliyofanya Abdul Sykes na Hamza Mwapachu kuchukua uongozi wa TAA 1950 na vipi walijuana na Nyerere alipofika Dar es Salaam mwaka wa 1952 na vipi walimchagua kuwa rais wa TAA 1953 chama kikafa. Dossa akanieleza kwa kirefu sababu ya TAA kufifia na nini walifanya kukirudishia chama nguvu yake.

Dossa akanieleza maisha ya utoto wake na jinsi alivozuiwa na baba yake kuanza shule hadi awe amehitimu Qur’an kwanza hivyo ikawa yeye kaanza darasa la kwanza akiwa na miaka 14 na ndiyo sababu ya kuanza darasa la kwanza na Abbas ingawa Abbas ni mdogo sana kwake.

Mbele ya nyumba yake kulikuwa na mabaki ya Land Rover. Dossa akanyoosha kidole chake cha shahada akasema, ‘’Unaona gari hiyo hapo. Nimetembea na Nyerere Tanganyika nzima na gari hii tukiwaamsha wananchi waingie TANU tumtoe Mwingereza nchini kwetu. Tulikuwa tunakwama kwenye barabara mbovu na inabidi tushuke tusukume gari na Nyerere na yeye akipiga kibega kusukuma. Usimuone mwembamba vile ana nguvu yule…’’

Hili neno ‘’kupiga kibega,’’ lilinidhihirishia kuwa kweli Dossa ni mtoto wa Gerezani kabisa kwani ni lugha ambayo mimi nimeizoea kuisikia kwa wazee wengi wakati ule. Ally Sykes alikuwa kimya, mimi niko kimya sote tunamsikiliza Dossa akizungumza kwa taratibu tena bila ghadhabu. Nimefanya mahojiano na wazalendo wengi na huwa itafika mahali katika maelezo yake utaona ameghadhibika kwa yale ambayo yeye anaona hakustahili kutendewa. Dossa hakuwa hivyo alikuwa ametulia tuli akizungumza kwa upole.

Dossa alikuwa kachoka ufukara umempiga pasi na kiasi. Sifa za utajiri wa baba yake Aziz Ali na sifa zake mwenyewe Dossa zilikuwa zinafahamika. Rafiki zake wanasema walikuwa wakimuona Dossa ameingia kila mtu anapumua kwani watakula na kunywa kwa furaha. Dossa alikuwa mtu karimu sana. Rafiki zake wa karibu sana walimpa jina la utani, ‘’The Bank.’’

Mimi nilikuwa namwangalia huku nikishusha pumzi kwa huzuni. Katika miaka ya 1920 babu yangu alikuwa na nyumba Mtaa wa Mbaruku jirani na nyumba ya Aziz Ali. Sifa zao zikijulikana na wote. Mwisho Dossa akanieleza safari yake ya Nairobi alipokwenda kufanya usaili wa kozi ya urubani na jinsi Wazungu wakakataa kumfanyia usaili juu ya kuwa walimwita wenyewe yeye na mtoto wa Ali Mmanga aliyekuwa kati ya matajiri wakubwa wa Dar es Salaam miaka ile. Jumba lake la fahari bado lipo hadi leo pale Kisutu.

Dossa akanieleza alivyomkuta Ally Sykes Nairobi mwaka wa 1947 tayari keshajiingiza katika siasa za akina Kenyatta. Dossa akanieleza kuwa baada ya kukataliwa alipiga simu Dar es Salaam kwa baba yake huku analia. Baba yake kwa huruma siku ya pili akampelekea fedha akamwambia basi anunue gari kama kifuta machozi. Dossa akanyanyua uso akaniangalia akasema, ‘’Nilikwenda Nairobi na basi nikarudi Dar es Salaam naendesha gari yangu mwenyewe tena mpya. Gari hii ndiyo ikajakuwa gari ya kwanza ya TANU…’’

Mwalimu Nyerere alipokuwa anastaafu alitoa medali 3979 kwa Watanzania walioitumikia nchi hii. Jina la Dossa halikuwapo katika orodha ile…''
 
Tajiri...
Nimeona mara kwa mara zinakuja post zinazomhusu Dossa Azizi au baba yake Aziz Ali.
Katika miaka ya 1930s babu yangu Salum Abdallah alikuwa na nyumba Mtaa wa Mbaruku, mtaa ambao Aziz Ali alikuwa anaishi.

Kwa ajili hii kwangu mimi ukoo wa Aziz Ali ukawa ni watu nawajua kwa kuwasikia kwanza kisha nikaja kufahamiana na baadhi ya wanae lakini aliyekuwa karibu sana na mimi na katika mapenzi makubwa baina yetu ni Hamza Aziz ambae alipata kuwa Inspector General of Police (IGP) katiika miaka ya 1970.

Dossa Aziz nilikuja kufahamiananae baadae sana na kitu ninachokumbuka alipojulishwa kuwa mimi ni mtoto wa Said Salum akafurahi sana na kunambia kuwa baba yangu alikuwa mtu mpole sana.

Ally Sykes ndiye aliyenipeleka kwake na ndiye aliyenitambulisha kwake.
Nakukaribisheni katika safari yangu na Ally Sykes siku aliponipeleka kwa Waziri Dossa Aziz wakati wa TANU alipokuwa mfadhili mkubwa wa chama wapenzi wake walimpa jina, ''The Bank,'':

''Ilikuwa katika miaka ya 1980 mwishoni siku mimi na Ally Sykes tulipokwenda kumtembelea Dossa Aziz. Wakati ule nilikuwa nafanya utafiti kuandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes kaka yake Ally Sykes. Tulikuwa tuko mbali katika kazi ile na siku moja nikamuomba Ally Sykes anipeleke kwa Dossa Aziz nikamfanyie mahojiano.

Ilikuwa siku ya Jumapili na nilimsubiri Ally Sykes Mbuyuni katika kituo cha basi mimi nikitokea Masaki. Hapa ni barabara ya Ali Hassan Mwinyi zamani ikiitwa (Upanga Road). Huu Mbuyu ulikuwa unaitwa Mbuyu wa Kigwe lakini si wengi walikuwa wanajua jina hili. Jina hili mimi alinipa Mzee Jimpota ambae yeye na baba yangu walikuwa pamoja katika Dar es Salaam ya 1950 na akaniambia kuwa hilo jina la Kigwe ni Mzee Mwinyikhamis Kigwe wa Msasani ambao wote wakijuana toka utoto wao. Mwinyikhamisi Kigwe akitoka kwao ni Msasani kuja kusoma shule ya Kitchwele Government School pamoja na baba yangu, Ally Sykes kaka yake Abdul na vijana wengine wa Dar es Salaam.

Jimpota yeye alikuwa fundi cherehani, siku moja katika mazungumzo ndipo akaniambia kuwa ule Mbuyu waliupa jina wao wakauita, ‘’Mbuyu wa Kigwe.’’

Ally Sykes ainipitia pale na Mercedes Benz yake mpya, nyeusi inang’ara kama kioo. Alikuwa na mama mmoja Mmarekani Mweusi akanitambulisha kuwa ni mwandishi wa ‘’Washington Post,’’ Ally Sykes akipenda muziki na safari kwenda Mlandizi ilikuwa ya raha sana muziki uliokuwa ukitoka katika spika za lile dude haukuwa wa kawaida. Unasikia kila chombo. Tulipofika Mlandizi tukasimama ofisi ya CCM kuuliza nyumbani kwa Dossa Aziz. Nilipata mshtuko mkubwa pale tulipojibiwa kuwa hawamjui Dossa Aziz. Tuliondoka na tukauliza mbele watu wawili, watatu hivi mwisho bwana mmoja akatuelekeza akatuambia tuifuate njia ya majani iliyokuwa pembeni yetu itatufikisha hadi nyumbani kwa Dossa.

Tulimkuta Dossa amekaa barazani kwake ilikuwa kiasi cha saa tatu asubuhi hivi mkononi ameshika radio ya kizamani kidogo na amefungua BBC anasikiliza. Alipomwona Ally Sykes, Dossa aliweka radio yake chini akapiga ukelele, ‘’Ally ndugu yangu karibu karibu…’’ Kwa jinsi walivyosalimiana na mazungumzo yao yalivyokuwa nilijua kuwa wawili hawa hawajaonana kwa miaka mingi. Pale pale Dossa akamuita mkewe akaja pale barazani. Dossa akamwambia, ‘’Huyu ni Ally kaka yake Bwana Mzuri.’’ Nikajakujua kuwa huyu, ‘’Bwana Mzuri,’’ ni Abbas Sykes ambae yeye alikuwa kila akija Dar es Salaam kutoka Ulaya alipokuwa balozi alikuwa lazima aende Mlandizi kumjulia hali Dossa. Baadae Dossa atanieleza mapenzi yake na Abbas yalianzaje na lini.

Ally Sykes akanijulisha kwa Dossa, ‘’Huyu Mohamed, mtoto wa Said,’’ Dossa akauliza, ‘’Said yupi?’’ Jibu likatoka, ‘’Said Popo.’’ Dossa akanipokea kwa tabasamu kubwa kabisa, ‘’Namjua baba yako alikuwa mpole sana…’’ Dossa akaagiza tuchinjiwe mbuzi lakini Ally Sykes akamwambia Dossa hatukuwa na muda. Ally Sykes akamweleza sababu ya mimi kumfuata.

Dossa alizungumza kwa kama saa moja hivi akianza mapinduzi waliyofanya Abdul Sykes na Hamza Mwapachu kuchukua uongozi wa TAA 1950 na vipi walijuana na Nyerere alipofika Dar es Salaam mwaka wa 1952 na vipi walimchagua kuwa rais wa TAA 1953 chama kikafa. Dossa akanieleza kwa kirefu sababu ya TAA kufifia na nini walifanya kukirudishia chama nguvu yake.

Dossa akanieleza maisha ya utoto wake na jinsi alivozuiwa na baba yake kuanza shule hadi awe amehitimu Qur’an kwanza hivyo ikawa yeye kaanza darasa la kwanza akiwa na miaka 14 na ndiyo sababu ya kuanza darasa la kwanza na Abbas ingawa Abbas ni mdogo sana kwake.

Mbele ya nyumba yake kulikuwa na mabaki ya Land Rover. Dossa akanyoosha kidole chake cha shahada akasema, ‘’Unaona gari hiyo hapo. Nimetembea na Nyerere Tanganyika nzima na gari hii tukiwaamsha wananchi waingie TANU tumtoe Mwingereza nchini kwetu. Tulikuwa tunakwama kwenye barabara mbovu na inabidi tushuke tusukume gari na Nyerere na yeye akipiga kibega kusukuma. Usimuone mwembamba vile ana nguvu yule…’’

Hili neno ‘’kupiga kibega,’’ lilinidhihirishia kuwa kweli Dossa ni mtoto wa Gerezani kabisa kwani ni lugha ambayo mimi nimeizoea kuisikia kwa wazee wengi wakati ule. Ally Sykes alikuwa kimya, mimi niko kimya sote tunamsikiliza Dossa akizungumza kwa taratibu tena bila ghadhabu. Nimefanya mahojiano na wazalendo wengi na huwa itafika mahali katika maelezo yake utaona ameghadhibika kwa yale ambayo yeye anaona hakustahili kutendewa. Dossa hakuwa hivyo alikuwa ametulia tuli akizungumza kwa upole.

Dossa alikuwa kachoka ufukara umempiga pasi na kiasi. Sifa za utajiri wa baba yake Aziz Ali na sifa zake mwenyewe Dossa zilikuwa zinafahamika. Rafiki zake wanasema walikuwa wakimuona Dossa ameingia kila mtu anapumua kwani watakula na kunywa kwa furaha. Dossa alikuwa mtu karimu sana. Rafiki zake wa karibu sana walimpa jina la utani, ‘’The Bank.’’

Mimi nilikuwa namwangalia huku nikishusha pumzi kwa huzuni. Katika miaka ya 1920 babu yangu alikuwa na nyumba Mtaa wa Mbaruku jirani na nyumba ya Aziz Ali. Sifa zao zikijulikana na wote. Mwisho Dossa akanieleza safari yake ya Nairobi alipokwenda kufanya usaili wa kozi ya urubani na jinsi Wazungu wakakataa kumfanyia usaili juu ya kuwa walimwita wenyewe yeye na mtoto wa Ali Mmanga aliyekuwa kati ya matajiri wakubwa wa Dar es Salaam miaka ile. Jumba lake la fahari bado lipo hadi leo pale Kisutu.

Dossa akanieleza alivyomkuta Ally Sykes Nairobi mwaka wa 1947 tayari keshajiingiza katika siasa za akina Kenyatta. Dossa akanieleza kuwa baada ya kukataliwa alipiga simu Dar es Salaam kwa baba yake huku analia. Baba yake kwa huruma siku ya pili akampelekea fedha akamwambia basi anunue gari kama kifuta machozi. Dossa akanyanyua uso akaniangalia akasema, ‘’Nilikwenda Nairobi na basi nikarudi Dar es Salaam naendesha gari yangu mwenyewe tena mpya. Gari hii ndiyo ikajakuwa gari ya kwanza ya TANU…’’

Mwalimu Nyerere alipokuwa anastaafu alitoa medali 3979 kwa Watanzania walioitumikia nchi hii. Jina la Dossa halikuwapo katika orodha ile…''
wote nyie, kama babu yako alikuwa na nyumba nchi hii mwaka 1930 leo hata wewe ulipaswa kuwa mmoja wa mabilionea.
miaka hiyo historia inatuambia mababu zetu wengine walikuwa wanalala mapangoni, utajiri ni ufahamu tu.

maana ake wewe umekuwa kwenye familia ambayo mababu tayari walikuwa wastraabu. sasa hela imeenda wapi?
 
Dah natamani sana ningekuwepo dar miaka ya 1950's nijue dar ilikuwaje enzi hizo
 
Tajiri...
Nimeona mara kwa mara zinakuja post zinazomhusu Dossa Azizi au baba yake Aziz Ali.
Katika miaka ya 1930s babu yangu Salum Abdallah alikuwa na nyumba Mtaa wa Mbaruku, mtaa ambao Aziz Ali alikuwa anaishi.

Kwa ajili hii kwangu mimi ukoo wa Aziz Ali ukawa ni watu nawajua kwa kuwasikia kwanza kisha nikaja kufahamiana na baadhi ya wanae lakini aliyekuwa karibu sana na mimi na katika mapenzi makubwa baina yetu ni Hamza Aziz ambae alipata kuwa Inspector General of Police (IGP) katiika miaka ya 1970.

Dossa Aziz nilikuja kufahamiananae baadae sana na kitu ninachokumbuka alipojulishwa kuwa mimi ni mtoto wa Said Salum akafurahi sana na kunambia kuwa baba yangu alikuwa mtu mpole sana.

Ally Sykes ndiye aliyenipeleka kwake na ndiye aliyenitambulisha kwake.
Nakukaribisheni katika safari yangu na Ally Sykes siku aliponipeleka kwa Waziri Dossa Aziz wakati wa TANU alipokuwa mfadhili mkubwa wa chama wapenzi wake walimpa jina, ''The Bank,'':

''Ilikuwa katika miaka ya 1980 mwishoni siku mimi na Ally Sykes tulipokwenda kumtembelea Dossa Aziz. Wakati ule nilikuwa nafanya utafiti kuandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes kaka yake Ally Sykes. Tulikuwa tuko mbali katika kazi ile na siku moja nikamuomba Ally Sykes anipeleke kwa Dossa Aziz nikamfanyie mahojiano.

Ilikuwa siku ya Jumapili na nilimsubiri Ally Sykes Mbuyuni katika kituo cha basi mimi nikitokea Masaki. Hapa ni barabara ya Ali Hassan Mwinyi zamani ikiitwa (Upanga Road). Huu Mbuyu ulikuwa unaitwa Mbuyu wa Kigwe lakini si wengi walikuwa wanajua jina hili. Jina hili mimi alinipa Mzee Jimpota ambae yeye na baba yangu walikuwa pamoja katika Dar es Salaam ya 1950 na akaniambia kuwa hilo jina la Kigwe ni Mzee Mwinyikhamis Kigwe wa Msasani ambao wote wakijuana toka utoto wao. Mwinyikhamisi Kigwe akitoka kwao ni Msasani kuja kusoma shule ya Kitchwele Government School pamoja na baba yangu, Ally Sykes kaka yake Abdul na vijana wengine wa Dar es Salaam.

Jimpota yeye alikuwa fundi cherehani, siku moja katika mazungumzo ndipo akaniambia kuwa ule Mbuyu waliupa jina wao wakauita, ‘’Mbuyu wa Kigwe.’’

Ally Sykes ainipitia pale na Mercedes Benz yake mpya, nyeusi inang’ara kama kioo. Alikuwa na mama mmoja Mmarekani Mweusi akanitambulisha kuwa ni mwandishi wa ‘’Washington Post,’’ Ally Sykes akipenda muziki na safari kwenda Mlandizi ilikuwa ya raha sana muziki uliokuwa ukitoka katika spika za lile dude haukuwa wa kawaida. Unasikia kila chombo. Tulipofika Mlandizi tukasimama ofisi ya CCM kuuliza nyumbani kwa Dossa Aziz. Nilipata mshtuko mkubwa pale tulipojibiwa kuwa hawamjui Dossa Aziz. Tuliondoka na tukauliza mbele watu wawili, watatu hivi mwisho bwana mmoja akatuelekeza akatuambia tuifuate njia ya majani iliyokuwa pembeni yetu itatufikisha hadi nyumbani kwa Dossa.

Tulimkuta Dossa amekaa barazani kwake ilikuwa kiasi cha saa tatu asubuhi hivi mkononi ameshika radio ya kizamani kidogo na amefungua BBC anasikiliza. Alipomwona Ally Sykes, Dossa aliweka radio yake chini akapiga ukelele, ‘’Ally ndugu yangu karibu karibu…’’ Kwa jinsi walivyosalimiana na mazungumzo yao yalivyokuwa nilijua kuwa wawili hawa hawajaonana kwa miaka mingi. Pale pale Dossa akamuita mkewe akaja pale barazani. Dossa akamwambia, ‘’Huyu ni Ally kaka yake Bwana Mzuri.’’ Nikajakujua kuwa huyu, ‘’Bwana Mzuri,’’ ni Abbas Sykes ambae yeye alikuwa kila akija Dar es Salaam kutoka Ulaya alipokuwa balozi alikuwa lazima aende Mlandizi kumjulia hali Dossa. Baadae Dossa atanieleza mapenzi yake na Abbas yalianzaje na lini.

Ally Sykes akanijulisha kwa Dossa, ‘’Huyu Mohamed, mtoto wa Said,’’ Dossa akauliza, ‘’Said yupi?’’ Jibu likatoka, ‘’Said Popo.’’ Dossa akanipokea kwa tabasamu kubwa kabisa, ‘’Namjua baba yako alikuwa mpole sana…’’ Dossa akaagiza tuchinjiwe mbuzi lakini Ally Sykes akamwambia Dossa hatukuwa na muda. Ally Sykes akamweleza sababu ya mimi kumfuata.

Dossa alizungumza kwa kama saa moja hivi akianza mapinduzi waliyofanya Abdul Sykes na Hamza Mwapachu kuchukua uongozi wa TAA 1950 na vipi walijuana na Nyerere alipofika Dar es Salaam mwaka wa 1952 na vipi walimchagua kuwa rais wa TAA 1953 chama kikafa. Dossa akanieleza kwa kirefu sababu ya TAA kufifia na nini walifanya kukirudishia chama nguvu yake.

Dossa akanieleza maisha ya utoto wake na jinsi alivozuiwa na baba yake kuanza shule hadi awe amehitimu Qur’an kwanza hivyo ikawa yeye kaanza darasa la kwanza akiwa na miaka 14 na ndiyo sababu ya kuanza darasa la kwanza na Abbas ingawa Abbas ni mdogo sana kwake.

Mbele ya nyumba yake kulikuwa na mabaki ya Land Rover. Dossa akanyoosha kidole chake cha shahada akasema, ‘’Unaona gari hiyo hapo. Nimetembea na Nyerere Tanganyika nzima na gari hii tukiwaamsha wananchi waingie TANU tumtoe Mwingereza nchini kwetu. Tulikuwa tunakwama kwenye barabara mbovu na inabidi tushuke tusukume gari na Nyerere na yeye akipiga kibega kusukuma. Usimuone mwembamba vile ana nguvu yule…’’

Hili neno ‘’kupiga kibega,’’ lilinidhihirishia kuwa kweli Dossa ni mtoto wa Gerezani kabisa kwani ni lugha ambayo mimi nimeizoea kuisikia kwa wazee wengi wakati ule. Ally Sykes alikuwa kimya, mimi niko kimya sote tunamsikiliza Dossa akizungumza kwa taratibu tena bila ghadhabu. Nimefanya mahojiano na wazalendo wengi na huwa itafika mahali katika maelezo yake utaona ameghadhibika kwa yale ambayo yeye anaona hakustahili kutendewa. Dossa hakuwa hivyo alikuwa ametulia tuli akizungumza kwa upole.

Dossa alikuwa kachoka ufukara umempiga pasi na kiasi. Sifa za utajiri wa baba yake Aziz Ali na sifa zake mwenyewe Dossa zilikuwa zinafahamika. Rafiki zake wanasema walikuwa wakimuona Dossa ameingia kila mtu anapumua kwani watakula na kunywa kwa furaha. Dossa alikuwa mtu karimu sana. Rafiki zake wa karibu sana walimpa jina la utani, ‘’The Bank.’’

Mimi nilikuwa namwangalia huku nikishusha pumzi kwa huzuni. Katika miaka ya 1920 babu yangu alikuwa na nyumba Mtaa wa Mbaruku jirani na nyumba ya Aziz Ali. Sifa zao zikijulikana na wote. Mwisho Dossa akanieleza safari yake ya Nairobi alipokwenda kufanya usaili wa kozi ya urubani na jinsi Wazungu wakakataa kumfanyia usaili juu ya kuwa walimwita wenyewe yeye na mtoto wa Ali Mmanga aliyekuwa kati ya matajiri wakubwa wa Dar es Salaam miaka ile. Jumba lake la fahari bado lipo hadi leo pale Kisutu.

Dossa akanieleza alivyomkuta Ally Sykes Nairobi mwaka wa 1947 tayari keshajiingiza katika siasa za akina Kenyatta. Dossa akanieleza kuwa baada ya kukataliwa alipiga simu Dar es Salaam kwa baba yake huku analia. Baba yake kwa huruma siku ya pili akampelekea fedha akamwambia basi anunue gari kama kifuta machozi. Dossa akanyanyua uso akaniangalia akasema, ‘’Nilikwenda Nairobi na basi nikarudi Dar es Salaam naendesha gari yangu mwenyewe tena mpya. Gari hii ndiyo ikajakuwa gari ya kwanza ya TANU…’’

Mwalimu Nyerere alipokuwa anastaafu alitoa medali 3979 kwa Watanzania walioitumikia nchi hii. Jina la Dossa halikuwapo katika orodha ile…''
Ahsante Mzee kwa history hii nzuri.Sasa utajiri wa Mzee Azizi Ali ulipotea mikononi mwa Mzee Dossa Azizi?
Na je,Unaweza kusema ni ule mchango wake wa hisani kwa Tanu na wana Tanu ndio umeifilisi familia hii iliyokuwa Tajiri?
 
Hii aya ya mwisho kiukweli imenistaajabisha.je waweza kutueleza kwanini mwalimu hakutambua mchango wa mtu aliyekua nae katika gari kuzunguka nchini wakati wa TANU? mohamed said
Tajiri...
Nimeona mara kwa mara zinakuja post zinazomhusu Dossa Azizi au baba yake Aziz Ali.
Katika miaka ya 1930s babu yangu Salum Abdallah alikuwa na nyumba Mtaa wa Mbaruku, mtaa ambao Aziz Ali alikuwa anaishi.

Kwa ajili hii kwangu mimi ukoo wa Aziz Ali ukawa ni watu nawajua kwa kuwasikia kwanza kisha nikaja kufahamiana na baadhi ya wanae lakini aliyekuwa karibu sana na mimi na katika mapenzi makubwa baina yetu ni Hamza Aziz ambae alipata kuwa Inspector General of Police (IGP) katiika miaka ya 1970.

Dossa Aziz nilikuja kufahamiananae baadae sana na kitu ninachokumbuka alipojulishwa kuwa mimi ni mtoto wa Said Salum akafurahi sana na kunambia kuwa baba yangu alikuwa mtu mpole sana.

Ally Sykes ndiye aliyenipeleka kwake na ndiye aliyenitambulisha kwake.
Nakukaribisheni katika safari yangu na Ally Sykes siku aliponipeleka kwa Waziri Dossa Aziz wakati wa TANU alipokuwa mfadhili mkubwa wa chama wapenzi wake walimpa jina, ''The Bank,'':

''Ilikuwa katika miaka ya 1980 mwishoni siku mimi na Ally Sykes tulipokwenda kumtembelea Dossa Aziz. Wakati ule nilikuwa nafanya utafiti kuandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes kaka yake Ally Sykes. Tulikuwa tuko mbali katika kazi ile na siku moja nikamuomba Ally Sykes anipeleke kwa Dossa Aziz nikamfanyie mahojiano.

Ilikuwa siku ya Jumapili na nilimsubiri Ally Sykes Mbuyuni katika kituo cha basi mimi nikitokea Masaki. Hapa ni barabara ya Ali Hassan Mwinyi zamani ikiitwa (Upanga Road). Huu Mbuyu ulikuwa unaitwa Mbuyu wa Kigwe lakini si wengi walikuwa wanajua jina hili. Jina hili mimi alinipa Mzee Jimpota ambae yeye na baba yangu walikuwa pamoja katika Dar es Salaam ya 1950 na akaniambia kuwa hilo jina la Kigwe ni Mzee Mwinyikhamis Kigwe wa Msasani ambao wote wakijuana toka utoto wao. Mwinyikhamisi Kigwe akitoka kwao ni Msasani kuja kusoma shule ya Kitchwele Government School pamoja na baba yangu, Ally Sykes kaka yake Abdul na vijana wengine wa Dar es Salaam.

Jimpota yeye alikuwa fundi cherehani, siku moja katika mazungumzo ndipo akaniambia kuwa ule Mbuyu waliupa jina wao wakauita, ‘’Mbuyu wa Kigwe.’’

Ally Sykes ainipitia pale na Mercedes Benz yake mpya, nyeusi inang’ara kama kioo. Alikuwa na mama mmoja Mmarekani Mweusi akanitambulisha kuwa ni mwandishi wa ‘’Washington Post,’’ Ally Sykes akipenda muziki na safari kwenda Mlandizi ilikuwa ya raha sana muziki uliokuwa ukitoka katika spika za lile dude haukuwa wa kawaida. Unasikia kila chombo. Tulipofika Mlandizi tukasimama ofisi ya CCM kuuliza nyumbani kwa Dossa Aziz. Nilipata mshtuko mkubwa pale tulipojibiwa kuwa hawamjui Dossa Aziz. Tuliondoka na tukauliza mbele watu wawili, watatu hivi mwisho bwana mmoja akatuelekeza akatuambia tuifuate njia ya majani iliyokuwa pembeni yetu itatufikisha hadi nyumbani kwa Dossa.

Tulimkuta Dossa amekaa barazani kwake ilikuwa kiasi cha saa tatu asubuhi hivi mkononi ameshika radio ya kizamani kidogo na amefungua BBC anasikiliza. Alipomwona Ally Sykes, Dossa aliweka radio yake chini akapiga ukelele, ‘’Ally ndugu yangu karibu karibu…’’ Kwa jinsi walivyosalimiana na mazungumzo yao yalivyokuwa nilijua kuwa wawili hawa hawajaonana kwa miaka mingi. Pale pale Dossa akamuita mkewe akaja pale barazani. Dossa akamwambia, ‘’Huyu ni Ally kaka yake Bwana Mzuri.’’ Nikajakujua kuwa huyu, ‘’Bwana Mzuri,’’ ni Abbas Sykes ambae yeye alikuwa kila akija Dar es Salaam kutoka Ulaya alipokuwa balozi alikuwa lazima aende Mlandizi kumjulia hali Dossa. Baadae Dossa atanieleza mapenzi yake na Abbas yalianzaje na lini.

Ally Sykes akanijulisha kwa Dossa, ‘’Huyu Mohamed, mtoto wa Said,’’ Dossa akauliza, ‘’Said yupi?’’ Jibu likatoka, ‘’Said Popo.’’ Dossa akanipokea kwa tabasamu kubwa kabisa, ‘’Namjua baba yako alikuwa mpole sana…’’ Dossa akaagiza tuchinjiwe mbuzi lakini Ally Sykes akamwambia Dossa hatukuwa na muda. Ally Sykes akamweleza sababu ya mimi kumfuata.

Dossa alizungumza kwa kama saa moja hivi akianza mapinduzi waliyofanya Abdul Sykes na Hamza Mwapachu kuchukua uongozi wa TAA 1950 na vipi walijuana na Nyerere alipofika Dar es Salaam mwaka wa 1952 na vipi walimchagua kuwa rais wa TAA 1953 chama kikafa. Dossa akanieleza kwa kirefu sababu ya TAA kufifia na nini walifanya kukirudishia chama nguvu yake.

Dossa akanieleza maisha ya utoto wake na jinsi alivozuiwa na baba yake kuanza shule hadi awe amehitimu Qur’an kwanza hivyo ikawa yeye kaanza darasa la kwanza akiwa na miaka 14 na ndiyo sababu ya kuanza darasa la kwanza na Abbas ingawa Abbas ni mdogo sana kwake.

Mbele ya nyumba yake kulikuwa na mabaki ya Land Rover. Dossa akanyoosha kidole chake cha shahada akasema, ‘’Unaona gari hiyo hapo. Nimetembea na Nyerere Tanganyika nzima na gari hii tukiwaamsha wananchi waingie TANU tumtoe Mwingereza nchini kwetu. Tulikuwa tunakwama kwenye barabara mbovu na inabidi tushuke tusukume gari na Nyerere na yeye akipiga kibega kusukuma. Usimuone mwembamba vile ana nguvu yule…’’

Hili neno ‘’kupiga kibega,’’ lilinidhihirishia kuwa kweli Dossa ni mtoto wa Gerezani kabisa kwani ni lugha ambayo mimi nimeizoea kuisikia kwa wazee wengi wakati ule. Ally Sykes alikuwa kimya, mimi niko kimya sote tunamsikiliza Dossa akizungumza kwa taratibu tena bila ghadhabu. Nimefanya mahojiano na wazalendo wengi na huwa itafika mahali katika maelezo yake utaona ameghadhibika kwa yale ambayo yeye anaona hakustahili kutendewa. Dossa hakuwa hivyo alikuwa ametulia tuli akizungumza kwa upole.

Dossa alikuwa kachoka ufukara umempiga pasi na kiasi. Sifa za utajiri wa baba yake Aziz Ali na sifa zake mwenyewe Dossa zilikuwa zinafahamika. Rafiki zake wanasema walikuwa wakimuona Dossa ameingia kila mtu anapumua kwani watakula na kunywa kwa furaha. Dossa alikuwa mtu karimu sana. Rafiki zake wa karibu sana walimpa jina la utani, ‘’The Bank.’’

Mimi nilikuwa namwangalia huku nikishusha pumzi kwa huzuni. Katika miaka ya 1920 babu yangu alikuwa na nyumba Mtaa wa Mbaruku jirani na nyumba ya Aziz Ali. Sifa zao zikijulikana na wote. Mwisho Dossa akanieleza safari yake ya Nairobi alipokwenda kufanya usaili wa kozi ya urubani na jinsi Wazungu wakakataa kumfanyia usaili juu ya kuwa walimwita wenyewe yeye na mtoto wa Ali Mmanga aliyekuwa kati ya matajiri wakubwa wa Dar es Salaam miaka ile. Jumba lake la fahari bado lipo hadi leo pale Kisutu.

Dossa akanieleza alivyomkuta Ally Sykes Nairobi mwaka wa 1947 tayari keshajiingiza katika siasa za akina Kenyatta. Dossa akanieleza kuwa baada ya kukataliwa alipiga simu Dar es Salaam kwa baba yake huku analia. Baba yake kwa huruma siku ya pili akampelekea fedha akamwambia basi anunue gari kama kifuta machozi. Dossa akanyanyua uso akaniangalia akasema, ‘’Nilikwenda Nairobi na basi nikarudi Dar es Salaam naendesha gari yangu mwenyewe tena mpya. Gari hii ndiyo ikajakuwa gari ya kwanza ya TANU…’’

Mwalimu Nyerere alipokuwa anastaafu alitoa medali 3979 kwa Watanzania walioitumikia nchi hii. Jina la Dossa halikuwapo katika orodha ile…''
 
Natamani siku nipate fursa mzee Mohamed Said unitembeze mjini dar nakunionesha mitaa ambayo vijana wa enzi hizoo akiwemo mwalimu nyerere walikuwa wakikutana na kufanya mambo yao.mji umebadilika nowadays.
 
Hii aya ya mwisho kiukweli imenistaajabisha.je waweza kutueleza kwanini mwalimu hakutambua mchango wa mtu aliyekua nae katika gari kuzunguka nchini wakati wa TANU? mohamed said
Waterloo,
Wakati nafanya utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes nimejiuliza mimi mwenyewe maswali mengi sana ambayo sikuwa na majibu na sikuweza pia kumuuliza mwingine yeyote kupata majibu kwani ithibati ya jibu la swali kama hilo lako kuwa iweje Dossa hakutambuliwa lisingeweza kutolewa na yeyote awae yule ila mwenyewe anaetoa hizo medali.

Lakini mimi nilikwenda mbali zaidi ya Dossa kwani walikuwapo wengi ambao michango yao katika kupigania uhuru wa Tanganyika ilikuwa ya kutukuka sana.

Hawa walikuwapo TANU HQ New Street na wengine walikuwapo katika majimbo mbalimbali ya Tanganyika.

Hawa wote hawakuwapo katika orodha ya kupewa medali.

Hata hivyo nilibahatika kupitia mtu wa kati kumjua Mwenyekiti wa Kutunuku Medali na kuuliza kuhusu utoaji wa medali kwa wazalendo waliotoa mchango mkubwa katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Jibu nililopokea kutoka kwa mpashaji wangu kutoka kwa Mwenyekiti wa Medali lilinishangaza sana.
 
Natamani siku nipate fursa mzee Mohamed Said unitembeze mjini dar nakunionesha mitaa ambayo vijana wa enzi hizoo akiwemo mwalimu nyerere walikuwa wakikutana na kufanya mambo yao.mji umebadilika nowadays.
Waterloo,
Fikra nzuri sana.
Napendekeza tupige video nadhani tutapata kipindi kizuri sana.

Nimeweka hapa baadhi ya nyumba zilizokuwa Dar es Salaam ya miaka ya 1950 na hizi ni nyumba za wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika.

Chini ya kila paa kuna historia.

Siku tutakapojaaliwa kutembea sehemu za Dar es Salaam nitakuonyesha sehemu zilipokuwapo nyumba za wazalendo ambao unawasoma hapa Barzani.

Nyumba mbili za akina Sykes ile ya Kipata ambapo akiishi Ally Sykes na ndimo alimoficha cyclostyle aliyokuwa akichapa makaratasi ya ''uchochezi,'' haipo badala yake kuna gorofa refu hali kadhalika nyumba ya Abdul Sykes ambayo ndipo alipoishi na Mwalimu Nyerere Mtaa wa Stanley pia haipo badala yake lipo gorofa refu.

Bahati mbaya sana hivi sasa kwetu sisi kuwa nyumba hizi hazipo tena badala yake kuna magorofa marefu lakini yale ambayo yamepitika katika nyumba hizi kumbukumbu zote bado katika vichwa vya wengi.

Kuna picha ya Alexander Thobias hapo chini kachero wa Waingereza ndani ya TAA.
Huyu aliajiriwa na TAA 1950.

''On his return to headquarters Abdulwahid recommended the establishment of a permanent secretariat at TAA New Street office to deal with routine duties of the Association.

TAA employed a Makerere graduate, Alexander Tobias, as its first salaried executive staff.''

Katika picha Alexander Thobias ni huyo aliyeinama alikuwa kajiriwa na Sauti ya Dar es Salaam kama Program Officer.

TAA waligundua usaliti wake na akafukuzwa kazi katika mkutano wa TAA wa 1954 uliounda TANU.
 

Attachments

  • MTAA WA TANDAMTI 1.jpg
    MTAA WA TANDAMTI 1.jpg
    18.5 KB · Views: 25
  • NYUMBA YA SYKES KIPATA.jpg
    NYUMBA YA SYKES KIPATA.jpg
    5.9 KB · Views: 27
  • NYUMBA YA MOHSIN KURASINI BUILDING.jpg
    NYUMBA YA MOHSIN KURASINI BUILDING.jpg
    66.2 KB · Views: 21
  • NYUMBA YA ABDUL SYKES STANLEY STREET.jpg
    NYUMBA YA ABDUL SYKES STANLEY STREET.jpg
    65 KB · Views: 21
  • NYUMBA ZA GEREZANI 1950s.jpg
    NYUMBA ZA GEREZANI 1950s.jpg
    42.5 KB · Views: 20
  • AL JAMIATUL ISLAMIYYA BUILDING.jpg
    AL JAMIATUL ISLAMIYYA BUILDING.jpg
    89.7 KB · Views: 18
  • ALEXANDER TOBIAS.png
    ALEXANDER TOBIAS.png
    95.2 KB · Views: 22
  • DOSSA AZIZ NA TITI MOHAMED.png
    DOSSA AZIZ NA TITI MOHAMED.png
    133.3 KB · Views: 25

Similar Discussions

Back
Top Bottom