Amavubi
JF-Expert Member
- Dec 9, 2010
- 30,145
- 13,216
Watu hukutana na kufahamiana kutokana na viunganishi mbalimbali, yaweza kuwa matukio, kupitia marafiki n.k
Hili la wapenzi/wanandoa kukutana nalo limekuwa na msisimko wa aina yake kutokana na simulizi mbalimbali, wapo wanaosema walikutana ofisini, shuleni, kwenye harusi, daladala nk, na wachache husimulia walianza anzanaje.
Je wewe unakumbuka ulikutana vipi na mpenzi/mwanandoa wako? pengine si bibaya ukatujuza zaidi ilikuwaje na mkaishiaje au mnaendeleaje hadi sasa....... hii itasaidia katika kujenga ujasiri kwa wengine humu.
Binafsi mpenzi wangu wa kwanza nilikutana naye nilipoenda kumuona bibi yangu aliyekuwa mgonjwa. Naye alikua amemsindikiza rafiki yake.
Ilitokea tu tukawa tunaangaliana sana na kwa bahati mbaya yule bibi alifariki na ikasaidia kuimarisha mahusiano kwani yule dada straight away aliniletea kadi.
Tulidumu miaka 4 kama marafiki tu mwishowe akaamua kufunga ndoa na mtu mwingine lakini bado tunawasiliana.
Hili la wapenzi/wanandoa kukutana nalo limekuwa na msisimko wa aina yake kutokana na simulizi mbalimbali, wapo wanaosema walikutana ofisini, shuleni, kwenye harusi, daladala nk, na wachache husimulia walianza anzanaje.
Je wewe unakumbuka ulikutana vipi na mpenzi/mwanandoa wako? pengine si bibaya ukatujuza zaidi ilikuwaje na mkaishiaje au mnaendeleaje hadi sasa....... hii itasaidia katika kujenga ujasiri kwa wengine humu.
Binafsi mpenzi wangu wa kwanza nilikutana naye nilipoenda kumuona bibi yangu aliyekuwa mgonjwa. Naye alikua amemsindikiza rafiki yake.
Ilitokea tu tukawa tunaangaliana sana na kwa bahati mbaya yule bibi alifariki na ikasaidia kuimarisha mahusiano kwani yule dada straight away aliniletea kadi.
Tulidumu miaka 4 kama marafiki tu mwishowe akaamua kufunga ndoa na mtu mwingine lakini bado tunawasiliana.