Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

ypte tisa kumi matumiz ya mustin lol!!
yaani mboga moto, ugal moto bakuli moto utakulaje utajiua wewe

kutandika kitanda jeeee....................unatandika afu usiku una opt kulala chin manake kukipatia kutandika asbh ni shidaa........
 
enzi zile makamanda hawakuwa na shule kabisa na walijitahidi kukariri maneno machache ya kingereza na kuyatumia kila mara.....nakumbuka ile adhabu ya push up!!!!!afande atakwambia ....haya...chini!down!chini!down....akimaanisha juu ..chini sasa ujifanye hujamuelewa!!!cha moto utakiona kwa kujifanya msomi!!!

Ulikua kambi gani, mwaka gani na operation gani mkuu?
 
ypte tisa kumi matumiz ya mustin lol!!
yaani mboga moto, ugal moto bakuli moto utakulaje utajiua wewe

kutandika kitanda jeeee....................unatandika afu usiku una opt kulala chin manake kukipatia kutandika asbh ni shidaa........

Waliita mustin ila ni mess tin, yale yale. Unakumbuka mambo ya green vest ya njano au nyekundu?
 
lol!!.................green vest af nyekundu

ila ukweli ukakamavu tulijifunza sana ivi wa siku hizi bado zile staili za zaman zipo?
ivi yale amteso tuliyopata bado wa siku hizi wanayapata?

Hakuna hekaheka kama zamani. Siku hizi hakuna kutafuta kuni wala kupika kuna mzabuni wa chakul pia muda ni mfupi sana,
 
Dah nakumbuka 841kj pale mafinga .... Jkt ya zaman ilikuwa na mafunzo mazur sana... Sitawasahau makamanda hawa. Lt nkya, Lt liundi, Lt alloys, na wiliam Sagala... Mpaka leo nina alama mgongon na mkono wa kushoto... Nilichimba handak kwa sahan na panga
 
Mafinga JKT 1981 sitasahau tulipopewa ng'ombe mimi na bw. Hezron Kigondo (sasa ni SACP wa Polisi Makao Makuu), kufika malishoni tukalala usingizi kwenye mti mmoja wa kivuli. Tulipoamshana hatukukuta ng'ombe hata mmoja, walitutoroka. TULIULIZANA TUTAEALEAZA NINI KIKOSINI? tuliamua twende liwalo na liwe tukiamini kwamba tutasaidiwa na kikosi kuwatafuta walipo.
Tulipowaeleza maafande acha watuhenyeshe kwa kwata mpaka tukawa mbendembende. KUMBE NG'OMBE WALIRUDI WENYEWE NA WALIKUWA KWENYE ZIZI LAO SALAMA KABISA.
 
Nakumbuka Mafinga mkuu wa Kikosi alikuwa Col. Mpakani. Nikiwa kombania D kwa afande Kazi,akina Ungele, Munishi. Ilikuwa raha tupu. Operation yetu ilikuwa inaitwa Wajibu.
 
Mafinga JKT 1981 sitasahau tulipopewa ng'ombe mimi na bw. Hezron Kigondo (sasa ni SACP wa Polisi Makao Makuu), kufika malishoni tukalala usingizi kwenye mti mmoja wa kivuli. Tulipoamshana hatukukuta ng'ombe hata mmoja, walitutoroka. TULIULIZANA TUTAEALEAZA NINI KIKOSINI? tuliamua twende liwalo na liwe tukiamini kwamba tutasaidiwa na kikosi kuwatafuta walipo.
Tulipowaeleza maafande acha watuhenyeshe kwa kwata mpaka tukawa mbendembende. KUMBE NG'OMBE WALIRUDI WENYEWE NA WALIKUWA KWENYE ZIZI LAO SALAMA KABISA.

Kuna jamaa alikuwa lindo na SAR, akaamua kwenda Disco na bunduki akaificha angani. Aliporudi bunduki haipo ! :confused2:
Jamaa akachukua Begi lake usiku huo huo, akaishi mpaka leo !

Kazi ya Jeshi.jpg
 
Mko wapi operation miaka 25 jkt makutupora kuni mtunduru nakumbuka afande alifiwa na mtoto tukapewa adhabu ya kuchimba kaburi lilikua kubwa mpaka co Matingas akapinga adhabu za hivyo

Nakumbuka zabibu kindi vyeyula na yule demu aliyefumaniwa na afande akatembezwa kikosi kizima eti malaya wa kikosi

Siku ya nyama familia zote zilikua zinakula nyama ,"pololo"
 
Daaa ezi hizo mafinga jkt tulienda kuzima moto msitu wa saohilli saa kumi tulitoka kikosini mpaka kesho yake saa 6mchana bila ya kula chochote pata picha na baridi la mufindi
 
Jaman mmenikumbusha vya jkt Mimi nlienda ruvu uwiiiiiii ni shida nmemiss Yale maisha kwa kweli mwendo wa kujila na jeshi amna shubwela hata sekunde mabio ya kutoshaaa daaa acha kabisaa
 
Back
Top Bottom