Mwanamkiwi
JF-Expert Member
- Mar 7, 2019
- 2,023
- 2,399
Pembetatu ya Kionga ilikuwa eneo dogo la kilomita za mraba 395 kusini mwa Mto Rovuma kwenye Bahari ya Hindi, ambayo ilienea kaskazini mwa Rasi Delgado . Ndani ya eneo hilo kuna mji wa Kionga (Kireno "Quionga"), ambao mwaka wa 1910 ulikuwa na karibu wakazi 4,000.
Eneo hili lilikuwa sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani lakini tangu 1918 ni sehemu ya Msumbiji.
Baada ya kuanzishwa kwa Afrika Mashariki ya Kijerumani mwaka 1885, nguvu ya Zanzibar ilififia. Wakati tume ya kuangalia mipaka ya Ujerumani-Kiingereza-Ufaransa iliposafiri ufukweni mwaka 1886 ili kujua ukubwa wa eneo la Wazanzibari, gavana wa Ureno alituma msafara wa kijeshi katika sehemu ya kusini ya Hori ya Tungi, ambapo tume iliamua kuwa eneo la Zanzibar linaenea katika kusini hadi kwenye mdomo wa Mto Minengani [4] kwenye hori hiyo. [5] . Makubaliano yafuatayo ya mipaka baina Uingereza na Ujerumani ya tarehe 29 Oktoba 1886 yalirudia azimio hili, lakini yalitaja eneo la kutenganisha maslahi ya Uingereza na Ujerumani kuwa liliamza tu kwenye Mto Rovuma. [6]
Mzozo wa Ureno na Ujerumani
Katika makubaliano yafuatayo ya Kijerumani-Kireno ya Desemba 30, 1886, mstari wa Rovuma kutoka mdomoni ulitajwa kuwa mpaka kati ya milki za Wareno na Wajerumani. [7] Ukanda wa pwani bado ulikuwa wa Zanzibar. Katika Mkataba wa Helgoland-Zanzibar wa mwaka 1890, Ujerumani ilichukua eneo la kusini mwa ukanda wa bara la Zanzibar katika pwani ya Afrika Mashariki, ingawa maandishi ya mkataba huo yalitaja tu "mpaka wa kaskazini wa jimbo la Msumbiji" na "njia ya mto Rovuma" kama mpaka wa kusini. Kwa hiyo, hali ya eneo la Kizanzibari upande wa kusini mwa Rovuma haikuwa wazi kimkataba.
Upande wa Ujerumani uliamua baadaye kidogo kuchukua udhibiti wa pande zote mbili za mdomo wa Rovuma na kumaliza mahali pa Kionga kama bandari ya magendo. [8] Kikosi cha wanamaji cha Ujerumani kilivamia eneo hilo tarehe 16. Juni 1894 na kuanzisha kituo cha Kionga penye ofisi ya forodha. [9] Hatimaye Ureno ilikubali kushiriki katika tume ya pamoja ya mpaka, ambayo mwaka wa 1895 ilikubali mpaka ambao ulipita kaskazini kidogo mwa Rasi Delgado kando ya latitudo 10° 40' hadi Rovuma, ambayo ilifuata kutoka hapa [10] . Hii ilianzisha "pembetatu ya Kionga".
Mnamo tarehe 25. Septemba 1919 katika Mkataba wa Versailles Rovuma hatimaye ilifafanuliwa kama mto wa mpaka. Ureno ilipewa pembetatu ya Kionga kama fidia kwa uharibifu wa vita. Tarehe 10 Januari 1920 eneo hilo lilikuwa eneo la kudhaminiwa chini ya mamlaka ya Shirikisho la Mataifa. Pembetatu ya Kionga ilijumuishwa rasmi katika Afrika ya Mashariki ya Kireno kwa sheria n.º 962 tarehe 2. Aprili 1920.
Mamlaka ya Shirikisho la Mataifa na udhamini wa Umoja wa Mataifa baadaye ulimalizika tarehe 25 Juni 1975 wakati wa uhuru wa Msumbiji, ambayo eneo hilo likawa sehemu ya jimbo la Cabo Delgado . [13]
Eneo hili lilikuwa sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani lakini tangu 1918 ni sehemu ya Msumbiji.
Historia ya awali
Mnamo karne ya 19 eneo karibu na Rasi Delgado lilitawaliwa na Usultani wa Tungi [1], ilhali Ureno ilidai pwani lote hadi Cape Delgado, lakini haikuwa tena na mamlaka yoyote kaskazini mwa kisiwa cha Ibo. [2] Sultani wake aliishi kwenye Hori ya Tungi, kusini mwa rasi. Mwaka 1844 mtawala wa Kizanzibari Said bin Sultani alikuwa ametangaza kwa Waingereza kwamba himaya yake ilienea hadi Rasi Delgado; lakini mwaka 1848 kutokana na udhaifu wa Ureno alimteua Sultani wa Tungi kuwa gavana, na mwaka 1854 Zanzibar ilimpeleka gavana wake pamoja na kikosi kidogo cha askari kwenda Tungi. [3]Baada ya kuanzishwa kwa Afrika Mashariki ya Kijerumani mwaka 1885, nguvu ya Zanzibar ilififia. Wakati tume ya kuangalia mipaka ya Ujerumani-Kiingereza-Ufaransa iliposafiri ufukweni mwaka 1886 ili kujua ukubwa wa eneo la Wazanzibari, gavana wa Ureno alituma msafara wa kijeshi katika sehemu ya kusini ya Hori ya Tungi, ambapo tume iliamua kuwa eneo la Zanzibar linaenea katika kusini hadi kwenye mdomo wa Mto Minengani [4] kwenye hori hiyo. [5] . Makubaliano yafuatayo ya mipaka baina Uingereza na Ujerumani ya tarehe 29 Oktoba 1886 yalirudia azimio hili, lakini yalitaja eneo la kutenganisha maslahi ya Uingereza na Ujerumani kuwa liliamza tu kwenye Mto Rovuma. [6]
Mzozo wa Ureno na Ujerumani
Katika makubaliano yafuatayo ya Kijerumani-Kireno ya Desemba 30, 1886, mstari wa Rovuma kutoka mdomoni ulitajwa kuwa mpaka kati ya milki za Wareno na Wajerumani. [7] Ukanda wa pwani bado ulikuwa wa Zanzibar. Katika Mkataba wa Helgoland-Zanzibar wa mwaka 1890, Ujerumani ilichukua eneo la kusini mwa ukanda wa bara la Zanzibar katika pwani ya Afrika Mashariki, ingawa maandishi ya mkataba huo yalitaja tu "mpaka wa kaskazini wa jimbo la Msumbiji" na "njia ya mto Rovuma" kama mpaka wa kusini. Kwa hiyo, hali ya eneo la Kizanzibari upande wa kusini mwa Rovuma haikuwa wazi kimkataba.
Upande wa Ujerumani uliamua baadaye kidogo kuchukua udhibiti wa pande zote mbili za mdomo wa Rovuma na kumaliza mahali pa Kionga kama bandari ya magendo. [8] Kikosi cha wanamaji cha Ujerumani kilivamia eneo hilo tarehe 16. Juni 1894 na kuanzisha kituo cha Kionga penye ofisi ya forodha. [9] Hatimaye Ureno ilikubali kushiriki katika tume ya pamoja ya mpaka, ambayo mwaka wa 1895 ilikubali mpaka ambao ulipita kaskazini kidogo mwa Rasi Delgado kando ya latitudo 10° 40' hadi Rovuma, ambayo ilifuata kutoka hapa [10] . Hii ilianzisha "pembetatu ya Kionga".
Pembetatu ya Kionga katika Vita ya Kwanza ya Dunia
Wakati wa Vita ya Kwanza ya Dunia, Wareno walivamia eneo hadi Mto Rovuma mnamo 1916. [11] Dola la Ujerumani liliwahi kutangaza vita dhidi ya Ureno mnamo tarehe 9. Machi 1916. [12]Mnamo tarehe 25. Septemba 1919 katika Mkataba wa Versailles Rovuma hatimaye ilifafanuliwa kama mto wa mpaka. Ureno ilipewa pembetatu ya Kionga kama fidia kwa uharibifu wa vita. Tarehe 10 Januari 1920 eneo hilo lilikuwa eneo la kudhaminiwa chini ya mamlaka ya Shirikisho la Mataifa. Pembetatu ya Kionga ilijumuishwa rasmi katika Afrika ya Mashariki ya Kireno kwa sheria n.º 962 tarehe 2. Aprili 1920.
Mamlaka ya Shirikisho la Mataifa na udhamini wa Umoja wa Mataifa baadaye ulimalizika tarehe 25 Juni 1975 wakati wa uhuru wa Msumbiji, ambayo eneo hilo likawa sehemu ya jimbo la Cabo Delgado . [13]