Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,707
Tukubali tukatae wapo ambao wanatamani dunia irudi nyuma ili ndoa zao zife,kwani wanashindwa kufanya hivyo sasa kwa sababu ya kidini au za kutokujiamini!Ngoja nikwambie kitu,hakuna Mungu atakaekuchoma moto au kukuadhibu kwa kuvunja ndoa yenye ufujaji au mateso ya aina yoyote.Mungu anataka ufurahie ndoa yako.Jisikie fahari kuwa na mkeo/mumeo.Kama ni kinyume hebu fikiria kama kuna ulazima wa kuwepo kwenye ndoa hiyo.Wanawake ndo wahanga wakubwa wa matatizo ya ndoa..Wengi huvumilia mateso ya ndoa kwa kuhofia usalama wa watoto,ngoja nikuambie,unapoendelea kukaa kwenye ndoa ya mateso unamharibu mwanao mpenzi kihisia na kimwili pia,kile unachoepuka kumpata mwanao ukiondoka,ndicho anakipata ukibaki.Usihofu kuhusu ugumu wa maisha,hata hapo unateseka pia.Ndoa ni furaha kwa mke ,mume na watoto,kama ni kinyume haina uhalali wa kuwepo!