JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 625
- 938
Kujiua ni kitendo cha mtu kukatisha maisha yake. Kwa mujibu wa American Foundation for Suicide Prevention, kujiua ni sababu ya 10 ya vifo duniani. Tabia ya kutaka kujiua ni ile hali ya mtu kuchukua hatua zinazohusiana na kukatisha maisha yake. Mawazo na tabia ya kutaka kukatisha maisha inachukuliwa kama dharura ya ugonjwa wa akili. Zifuatazo zinatambulika kama dalili za mtu anayetaka kujiua
Huwezi kutambua kwa urahisi mtu anavyojisikia ndani ya mwili wake, kwahiyo ni kazi ngumu sana kumtambua mtu anayetaka kujiua. Hatahivyo kuna dalili za nje zinazoweza kukutambulisha dalili za mtu anayetarajia kukatisha uhai wake.
- Kutishia ama kuzungumzia kuhusu kutaka kujiua
- Kujitenga ghafla na marafiki, familia na jamii
- Kuongeza kiwango cha matumizi ya pombe na dawa za kulevya
- Tabia ya ukali ya ghafla
- Mabadiliko makubwa ya mhemko (mood swing)
- Kuongelea, kuandika au kuwaza kuhusu kifo mara kwa mara kama njia sahihi
- Tabia ya ghafla ya uzembe au kusukumwa kufanya jambo
- Kulala sana au kidogo
- Kuzungumzia kuhusu kukosa tumaini na upweke
- Katika maongezi zingatia yafuatayo;
- Tulia na ongea kwa sauti ya utulivu
- Tambua ama kiri kwake kuwa hisia zake ni halali
- Muoneshe hali ya kumsaidia na kumpa moyo
- Mwambie kuwa msaada wa kile kinachomsumbua utapatikana na atajisikia vizuri pindi atakapotibiwa
Vilevile unaweza kumsaidia kupata msaada kwa mtaalamu kwa kupiga simu au kumpeleka kwenda kuonana nae.