Je, unaamini opposition kuingia Ikulu ndiyo suluhu ya matatizo yetu?

Wapinzani wamejaa maboriti tele. Wakutusaidia ni God tu.


Mungu akitupa huo msaada tutaweza kuutambua?
Mwaka 2005 alitupatia kiongozi kilaza ili kutupunguzia ugumu wa kufichua maovu serikalini.


Je, sababu tunazo za kushinikiza yale tunayotaka yafanyike? Katiba yetu kwa mfano, inakidhi hali ya sasa?
Kila mmoja wetu atumie nafasi aliyo nayo walau tuweze kuwa na idadi kubwa ya wabunge wa vyama mbadala 2010; labda kama hatujaona kazi wanayofanya.


Ni makosa kuketi chini tumekunja mikono kifuani tukisubiri wapinzani wafanye hiki au kile. Mwananchi anayeitakia mema familia na uzao wake ndiye mwenye jukumu. Wapinzani wasikilize kutoka kwetu na sio kinyume chake.


Kwa maoni yangu, msaada tushapewa - swali ni je, tunajua tunachotaka?
Rejea hoja ya Pundamilia07.


...Nasi tumkubali Jakaya Mrisho Kikwete kwa mapungufu yake yote, ukimya, uzembe, uvivu, uzubaaji, kutokuchangamka, kutokuwajibika na dhana kuwa analinda wale wahujumu. Mapungufu yake, ndiyo ngao na silaha yetu tuliyopewa na Mungu dhidi ya wale wenye kutaka kutufanyia dhuluma na kutuumiza.

....Kila jamii ina njia yake ambayo Mungu kawatengenezea. Njia yetu ya Ukombozi ni wakati huu wa ndugu yetu Muungwana akiwa Raisi!

Tutumie fursa hii ku....

KASOME: Thank God for Giving Us Kikwete!




.
 
Wakuu,

Kwanza naomba niseme kwamba, niliamua kuachana na siasa kwa muda hapa jamvini baada ya kukerwa na ile hotuba ya rais bungeni. Hotuba ile niliichukulia kama janga la kitaifa, hivo niliamua kuomboleza kisiasa kwa kipindi chote kilichopita baada ya hotuba!

Katika kuchangia thread hii napenda niseme kwamba, vyama vya upinzani bado vina nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi wa 2010 kama tu vitafanya mambo yafuatayo:

1. Watengeneze mazingira yatakayowawezesha kuungana kwa dhati kabla ya 2010 na kisha wasimamishe mgombea mmoja wa serikali za mitaa, udiwani na ubunge ambaye anakubalika kwa watu wengi wa mtaa, kata na jimbo husika, na kisha vyama vyao vyote kwa pamoja vimuunge mkono!

2. Wasimamishe mgombea mmoja wa urais na aungwe kwa dhati na vyama vyao vyote.

3. Nawashauri wamchague bwana Hamadi Rashidi (CUF) agombee kiti cha urais, na Dr. Slaa (CHADEMA) awe Mgombea mwenza.

Wakifuata huu ushauri wangu, amini usiamini, wapinzani watashinda kwenye uchaguzio mkuu wa 2010!

Mungu vibariki vyama vya upinzani viweze kuungana kwa dhati ili watz wapate ukombozi wa kweli!

Mungu wabariki bwana Hamadi Rashidi (CUF) na Dr. Slaa (CHADEMA)!

Is Freeman Mbowe ready for this?
 
Nikijibu kama Darwin.

Wapinzani wakiingia Ikulu inategemea nani umemuweka Ikulu, sio kuangalia tu mtu kwamba ni mpinzani wa CCM basi tumuweke Ikulu, lazima tujue anachotaka kufanya akiwa Ikulu nasio kusema tu CCM wanafanya vibaya.

Kwa upande wangu kama wapinzani wataingia Ikulu hata miaka mitano tu na CCM wakawa wapinzani ndio tutayajua hasa matunda ya vyama vingi.

Kwanini?

Wapinzani watajitahidi kwa uwezo wao kuwaridhisha wananchi ili waendelelee kuwa chama tawala.

CCM kwa wakati huo kama wapinzani ndio watakaotoa changamoto sana kuhusu taifa letu.
Wanajua pesa zinapatikana wapi na zitatumika vipi kuwanufaisha wananchi na kwahio wapinzani hawataweza kuwadanganya wananchi.

Wapinzani nao kwa wakati huo kama chama tawala watajitahidi kuwatendea mema wananchi ili usukani usiende tena na mwingine.

Yaani hao wapinzani wapewe hata miaka mitatu tu, hapo ndio tutayaona manufaa ya vyama vingi.

Lakini kama toka mfumo huu wa vyama vingi uanze aliyekua ni huyo huyo wa mwanzo basi Tanzania haitafika kokote japokua ni nchi yenye utajiri.

Ukimkabidhi mtu madaraka kwenye nyumba yako, na keshokutwa unata sukari akakunyima na akakuambia hana sukari, basi utamuambia unaniongopea kwasababu iko sehemu fulani, hii ilikua nyumba yangu na najua sukari ilipo, na kama haipo basi inapatikana sehemu fulani.
Hii ndio itakavyofanya CCM ikiwa mpinzani.

Darwini, asante kwa mchango wako mzuri. Mimi pia naamini kama hata wapinzani wataweza kuingia ikulu tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana kwani kila chama kitajitahidi kufa na kupona kukusanya nguvu ili kupata hiyo nafasi.

Kwa upande wangu kila chama kina haki kabisa ya kuingia ikulu kwani ni wapiga kura ndio wanachokiweka. Tatizo kubwa hapa kwepa ni kuiba kura. Hata kama chama fulani kinaweza kushinda kura zinaibiwa au watu wanadanganywa kukipigia chama fulani ili kipate ushindi zaidi.

Mpaka Watanzania tuje tuelemike na kutokubali kudanganywa tutakuwa tumepoteza bahati nyingi sana.

Nilikuwa Malawi wakati wa kushindwa kwa chama tawala Malawi Congress Party (MCP) mwaka 1992. Nadhani hakuna chama ambacho kilikuwa kimeishajiimarisha kisiasa kama chama hicho hapa Afrika. Kwa kwa wakati huo ukisikika tu unasema Rais hafai au chama tawala ni hivyo, ulikuwa unapotea na hutajulikana umekwenda wapi.

Siyo kwamba kulikuwa na uchawi, bali kulikuwa na makachero kila mahali na walikuwa wanaapa kwa Banda hata kumtoa mzazi au ndugu kwa ajili ya kulinda "nchi". Hivyo, mtu akiongea kitu chochote cha siasa ripoti zilikuwa zinatumwa kwa kuogopa kuwa kama huyo mtu hataripotiwa hao makachero wanaweza kufahamika kuwa hawakutimiza wajibu wao.

Yaani, karibu kila raia alikuwa anamchunga mwenzake anasema nini. Hata makanisani na misikitini wahubiri walipewa masharti kuhubiri yote isipokuwa kusema mambo ni mabaya. Ndiyo maana wakati huo Malawi ilijulikana kama nchi ya amani sana duniani lakini watu waliishi kwa woga mkubwa.

Ninachotaka kusema ni kwamba, pamoja na kujiimarisha kote huko, MCP ilishindwa 1992 na United Democratic Front (UDF) ikaingia madarakani na ikakaa kwa miaka 10 tu.

Nina hakika kadiri Watanzania wanavyozidi kuelemika na kuondoa woga na unafiki, ndivyo hivyo hivyo nchi yetu itakavyoendelea kusonga mbele zaidi na zaidi. Lakini tukikubali kuendelea kudanganywa kwa kupewa vijisenti na kuweka maisha yetu rehani tutaendelea kulia na kusaga meno.
 
Sina hakika unaposema opposition unamaanisha nini? Mtu yeyote, kikundi chochote cha watu nk. ambacho hakiko upande wa chama tawala ni "opposition side". Opposition sio CHADEMA tu, CUF, TLP nk. hapana hata wewe mwenyewe ni upinzani maadam hauridhishwi na utendaji wa kifisadi, na ukiritimba uliomo ndani ya CCM.

Hivyo, binafsi ninaamini kuwa opposition kuingia Ikulu ni suluhisho la matatizo yetu ilimradi tu kuwe na nia ya dhati ya kutatua matatizo haya, Hili mpaka sasa hivi limeonekana jinsi watanzania kupitia vyama vya upinzani, vikundi vya haki za binadamu, na wanaharakati mbalimbali.

Ni ukweli usiopingika tena kuwa CCM kimepoteza dira, na hakiko tena kwenye kumtetea mnyonge wa Tanzania. Rejea mikataba mibovu ya madini, ufisadi, na USWAHIBA katika serikali ya CCM.

Mabadiliko ya kweli yataletwa na watanzania wenyewe, tuungane na vyama vya upinzani ambavyo tayari vimeonyesha njia ili kwa pamija tuikomboe nchi yetu kutoka mikononi mwa mafisadi hawa wa CCM waliolewa madaraka.

Mungu ibariki Tanzania,
 
Is Freeman Mbowe ready for this?


Mkuu,

Kama Mr. Mbowe anauchungu na anayathamini maisha ya watz; na kama atairuhusu busara yake ifanye kazi, basi naamini atakubaliana na ushauri wangu wa kumwachia MR. HAMADI RASHIDI (CUF) agombee kiti cha urais akiwakilisha wapinzani wote, na DR. SLAA (CHADEMA) awe mgombea mwenza KATIKA UCHAGUZI MKUU WA 2010!
 
KunguruMwupe,

Mawazo yako mazuri sana na nadhani niliwahi kusema hivyo kuhusiana na haguzi za majimboni... Hata hivyo, huo Muungano kusema kweli leo hii ni ndoto ya mwendawazimu - According to....(jina nalihifadhi). Unafiki umejengwa ndani ya vyama hivi huwezi hata kuamini na kibaya zaidi wachawi wenyewe ndio wameshuka madaraka ya juu.
Kuna kitu kimoja ambacho ningependa unifahamishe hasa ktk uchaguzi wako wa huyo Mh. Hamad Rashid ambaye nina hakika ni asilimia 20 au chini ya wananchi wanamfahamu ama wamewahi kumsikia..
Kutofahamika ni moja ya kikwazo lakini pamoja na hayo unaweza kunambia wewe ni kitu gani hasa kilichokuvutia kuhusu huyu mheshimiwa kiasi kwamba umempendekeza mbele ya wenyeviti wote wa vyama vya Upinzani..
 
Sina hakika unaposema opposition unamaanisha nini? Mtu yeyote, kikundi chochote cha watu nk. ambacho hakiko upande wa chama tawala ni "opposition side". Opposition sio CHADEMA tu, CUF, TLP nk. hapana hata wewe mwenyewe ni upinzani maadam hauridhishwi na utendaji wa kifisadi, na ukiritimba uliomo ndani ya CCM.

Hivyo, binafsi ninaamini kuwa opposition kuingia Ikulu ni suluhisho la matatizo yetu ilimradi tu kuwe na nia ya dhati ya kutatua matatizo haya, Hili mpaka sasa hivi limeonekana jinsi watanzania kupitia vyama vya upinzani, vikundi vya haki za binadamu, na wanaharakati mbalimbali.

Ni ukweli usiopingika tena kuwa CCM kimepoteza dira, na hakiko tena kwenye kumtetea mnyonge wa Tanzania. Rejea mikataba mibovu ya madini, ufisadi, na USWAHIBA katika serikali ya CCM.

Mabadiliko ya kweli yataletwa na watanzania wenyewe, tuungane na vyama vya upinzani ambavyo tayari vimeonyesha njia ili kwa pamija tuikomboe nchi yetu kutoka mikononi mwa mafisadi hawa wa CCM waliolewa madaraka.

Mungu ibariki Tanzania,

Ntaramuka
Ahsante sana kwa mchango wako.
Lakini sentensi yako iliyofungua maelezo yako imeonesha huenda uliendelea kutoa hoja bila ya kujali kama hujanielewa vizuri. Kwa kufanya hivyo basi maelezo mengine yote yaliyofuatia yameendelea kubeba kutokuwa na hakika ya kile ulichokuwa unakieleza.

TAFSIRI: Neno 'opposition' limemaanisha vyama vya upinzani kama ambavyo nilivyoandika katika posting hiyo ya mwanzo kabisa. Any tafsiri isiyokwenda na maelezo niliyotoa inakuwa null and void, hatimaye kupoteza mwelekeo.

Mawazo yako ni mazuri, rephrase ili ueleweke zaidi.
 
Originally Posted by Pundamilia07
Wengi wetu tumeshuhudia katika chaguzi kuu za mwaka 1995 hadi 2005 vyama vya upinzani viliwekeza nguvu kubwa ya kuingia Ikulu kwa maana resouces nyingi zilitumika katika kutafuta kiti cha urais huku viti vya ubunge vikiachwa vitafutwe bila ya kuwekeza vya kutosha. Aidha, miaka 10 baadae baada ya uchaguzi wa kwanza uliohusisha vyama vingi, vyama vya siasa vya upinzani bado havijaelekeza nguvu zao nyingi za kuimarisha shughuli zao za kisiasa katika ngazi za chini kwa maana kuwa na matawi ambayo ndiyo majukwaa ya kukusanya wananchi na kusambaza shughuli zake.

Je, bado tunaamini kuwa kwa wapinzani kuipata Ikulu ndiyo suluhisho la matatizo yetu?



no sio kweli wapinzaani ni watu wanaolala kila siku wakikesha na kuomba serekali ikosee ili wapate mbinu ya kupata nafasi yala na wao

Well, ninajaribu kuoanisha maelezo yako vv hoja yangu lakini sipati uhusiano wa moja kwa moja, je unaweza kuandika kwa kina zaidi ni ipi hoja yako hasa?
 
Mimi bado naona hakuna haja ya kukimbilia vyama vya upinzani kwani vyenyewe bado ni vichanga sana na bado havijajikamilisha sawasawa ila mimi nadhani chama tawala kisipojikamilisha sawa itabidi sasa tujaribu upinzani na nina muomba sana muheshimiwa Rais wetu kwenye baraza lake lijalo kama mungu akipenda awe makini sana na jamaa anaowachagua kuingia kwenye nafasi mbalimbali kwani yeye anaweza kuwa mchapa kazi ila jamaa wa chini wanaweza kumuharibia sana sifa yako.
 
Wachangiaji kutoka Kenya, Malawi na Zambia wangetufungua macho kwenye suala hili.
 
Upinzani unaingia ikulu hatuna muda mrefu CCM baada ya kikwete imeshakuwa marehemu tayari watakuwa kikundi cha wezi ambao "friends for convenience" kila mtu anatengeneza mtandao kwa ajili ya maslahi maalum..wakati huo wakibomoana wenyewe kwa wenyewe...10 down the line hakuna kitu...
 
Vyama vya upinzani kuwania urais kwa sasa ni sawa sawa na kujenga nyumba kwenye foundation ya mchanga. Kwanza vijenge foundation ya mawe ndo viinue kuta.
 
Sidhani kama watu wanaokiendesha chama bila kuwa na ofisi ya kudumu kwa muda wa miaka 20 wanaweza simamia nchi..
 
Tazama katiba za vyama vyote vya siasa nchini, CCM pekee ambayo moja ya madhumuni yake ni kukamata mamlaka ya dola. Hakuna dhumuni hili kwenye katiba za vyama vingine. Mpaka hapa bado unaamini kuwa primal objective ya vyama vya upinzani ni kwendq Ikulu?
sasa mkuu hiyo prime objective unayoiona wewe kwa wapinzani ni ipi?
 
Ni akili matope plus kufikiri wewe ukishindwa ni lazima na wenzako washindwe.
 
Wengi wetu tumeshuhudia katika chaguzi kuu za mwaka 1995 hadi 2005 vyama vya upinzani viliwekeza nguvu kubwa ya kuingia Ikulu kwa maana resouces nyingi zilitumika katika kutafuta kiti cha urais huku viti vya ubunge vikiachwa vitafutwe bila ya kuwekeza vya kutosha. Aidha, miaka 10 baadae baada ya uchaguzi wa kwanza uliohusisha vyama vingi, vyama vya siasa vya upinzani bado havijaelekeza nguvu zao nyingi za kuimarisha shughuli zao za kisiasa katika ngazi za chini kwa maana kuwa na matawi ambayo ndiyo majukwaa ya kukusanya wananchi na kusambaza shughuli zake.

Je, bado tunaamini kuwa kwa wapinzani kuipata Ikulu ndiyo suluhisho la matatizo yetu?
hivii kung'ang'ania gari bovu linalokupeleka kwenu kwa siku mbili nzima njiani na kupewa gari jipya lenye uhakika wa kukufikisha kwenu ndani ya masaa 7 tu ipi bora?
nishaona unataka kujibu nnini... haya jibu sasa
 
Back
Top Bottom