Je, una mzio (allergy) au uoga (phobia) na kitu gani?

Gemini Are Forever

JF-Expert Member
Sep 10, 2019
1,457
2,435
Salaam wakuu.

Tulikuwa maeneo fulani leo mchana, tulienda kucheki mashamba ya jamaa yangu aliweka vibarua.

Tulipofika ktk mizunguko ya hapa na pale shambani, tukaenda kupumzika. Sasa kulikuwa na ndoo ya maji, ikabidi jamaa achukue kikombe anywe maji.

Jamaa kwa vile alishikwa na kiu ikabidi achote maji akaanza kunywa. Kapiga kama mafundo mawili hivi, ghafla akayamwaga maji na akaweka kikombe chini akainama kama anataka kutapika.

Baada ya sekunde kadhaa akaanza kutapika kweli. Kumuuliza kulikoni akasema kikombe kina harufu ya maziwa kitu ambacho roho yake haitaki kabisa. Nikashangaa sana. Yaani Maziwa mi nayapiga hata yakikamuliwa hapo hapo halafu yeye harufu tu anatapika!?

Mi kitu ambacho sikipendi ni bilinganya. Aisee ukinilisha bilingaya natapika hadi nyongo. Kuna jamaa nilisikia akinusa harufu ya nyama ya kondoo anatoa hadi nyongo.

Kuhusu phobia mi naogopa radi jamani duh.

Je, wewe phobia yako au allergy yako ni ipi?
 
Kuna mtu hapa kasema BA100😂😂

Kwangu Mimi Ni maziwa Hasa fresh Ni huwa najisikia VIBAYA Sijapata ona
Kwenye RADI. Naona twafanana hiyo kitu nainyali mbaya ukizingatia tu juzi Kati hapa Kama 2 months hivi imesepa na dogo mmoko hivi
 
Aisee nina Phobia tatu zanisumbua sana..
  • Height Phobia
Nina uoga urefu/kimo kirefu toka utoto Nilikua sipandi miti. Mpaka leo kwenye madaraja mpaka nivushwe kama ni kutembea.
  • Motors Phobia
Naujanja wangu wote ila nikipanda gari naumwa kabisa masikio yanaziba, kwanza masikio yanaziba Pannic attack inanishika hapo siwezi kulala kama ni basi likiyumba nalisukuma huku. Kwangu mimi kusafiri ni adhabu hua sifurahii. Hata private cars ni hivo hivo sema kuna dawa fulani zilinisaidia.
Afadhali kwa sasa..

  • Eye Contact / Crowd Phobia.
Mara nyingii sitoi sadaka ajili ya hiki kitu Lol

Allergy...

Ndizi ilikua hata upike uweke nini Siti nikila naumwa. Kuna Mtumishi alinimwagia injili afadhali kwasasa nakula kiasi. Allergies sometimes zinakua tied na mambo ya kiroho kutokana na maagano ya kwenye ukoo juu ya vyakula fulani. Vizazi na vizazi nyuma yako.
So kama una Allergies ya vyakula fulani waone hawa watu Mungu wanaweza kukusaidia
Pole mkuu, binafs n maziwa, yan hata kwenye hicho chombo kama ni kikombe hata ukioshaje ila kikishafika tu usawa wa mdomo n makosaaaa. Nitatema vyoye na vya jana utumbo ubak mweupeee🤣🤣

Zamani pia nilikuwa na allergy ya nyama zote zitokanazo na wanyama wa miguu minne, aiseee zimenitesa sana kitambo hichooo. Nyama pekee nilikuwa nakula ni nyama ya kuku, bata sikuwahi jaribu mana tulikuwa hatujafuga bata. Ila nashukuru Mungu maza alinipa dawa ikaniponya ila nyama ya kondoo ishagoma kabisaaaa😁
 
Kwa kweli kitu kinachonisumbua ni pumzi sina asthma
Ila kila sehemu nikiingia kama madirisha hayako wazi panic inaanza
Basi lililojaa watu nashuka
Chumba lazima dirisha liwe wazi kwa weather zote

Kingine ni kenge huyu mnyama bora niamke nyoka yuko chumbani kuliko Kenge
 
Wanangu walipokua wadogo, kukiwa na radi kwenye sala ya usiku wanamuomba Mungu aondoe radi, ikipoga tena wanasema mama Mungu hajasikia sala zetu.
Hapo kabla mi nilikuwa siogopi radi, ila miaka kam 15 iliyopita nilinusurika kupigwa na radi. Yan radi ilipita mita kadhaa tu kutoka nilipo ikapiga mti nikashuhudia kwa macho.

Tangu hapo, nikiona tu mvua yenye kila dalili ya radi huwa naenda ndani nafunga madirisha yote, nazima simu, nalala kifudifudi kitandani, nafunika macho kwa kukandamizia kwenye mto au shuka na huwa sitaki kelele ya aina yoyote.

Kiukwel kipindi cha mvua yenye radi huwa napata tabu sana.
 
Astra phobia. I have extreme fear to thunderstorms and lightening. Nilipokuwa shule ya msingi early 2000's radi ilimuua mwalimu akiandika ubaoni. Na siku nyingine pia mti mbichi upenuni mwa nyumbani ulipigwa radi ukakauka hapo hapo kesho yake tukaufanya kuni. Matukio hayo yamenifanya niwe mwoga mno wa radi.
 
Aisee nina Phobia tatu zanisumbua sana..
  • Height Phobia
Nina uoga urefu/kimo kirefu toka utoto Nilikua sipandi miti. Mpaka leo kwenye madaraja mpaka nivushwe kama ni kutembea.
  • Motors Phobia
Naujanja wangu wote ila nikipanda gari naumwa kabisa masikio yanaziba, kwanza masikio yanaziba Pannic attack inanishika hapo siwezi kulala kama ni basi likiyumba nalisukuma huku. Kwangu mimi kusafiri ni adhabu hua sifurahii. Hata private cars ni hivo hivo sema kuna dawa fulani zilinisaidia.
Afadhali kwa sasa..

  • Eye Contact / Crowd Phobia.
Mara nyingii sitoi sadaka ajili ya hiki kitu Lol

Allergy...

Ndizi ilikua hata upike uweke nini Siti nikila naumwa. Kuna Mtumishi alinimwagia injili afadhali kwasasa nakula kiasi. Allergies sometimes zinakua tied na mambo ya kiroho kutokana na maagano ya kwenye ukoo juu ya vyakula fulani. Vizazi na vizazi nyuma yako.
Duh, pole sana mkuu
 
Pole mkuu, binafs n maziwa, yan hata kwenye hicho chombo kama ni kikombe hata ukioshaje ila kikishafika tu usawa wa mdomo n makosaaaa. Nitatema vyoye na vya jana utumbo ubak mweupeee
Dawa gani hiyo ulipewa na maza kuhusu allergy ya nyama? Share nasi mkuu
 
Back
Top Bottom