Eddy Love
JF-Expert Member
- Jul 25, 2011
- 13,652
- 8,541
Leo naongea na mabinti ambao wanalea watoto wenyewe au wamepewa mimba na wametelekezwa au wewe ambaye uko kwenye mahusiano na mwanaume huku hujui akikupa mimba ukimuambia atakataa au atakubali nakuambia kamwe usilie kwa sababu umeachiwa mtoto au ujauzito na mwanaume.
Kitu cha kwanza na cha msingi kwa binti unapoanza mahusiano na mwanaume lazima kuna kitu unique kwa huyo mwanaume ndio mana ukawaacha wote na ukampenda.Sasa kama huyo mwanaume ana kitu unique basi hiyo ndio sababu kubwa ambayo inatakiwa ikupe amani hata kama atakupa mimba akukimbie.
Kitu cha pili kama wakati unapata mimba ilikuwa sio kwa kubakwa na siku hiyo mimba inaingia ulifurahia lile tendo basi hiyo ni sababu nyingine ya kukufanya usilie kwa sababu amekuachia mimba.
Leo jiulize kama umempenda mwanaume wako sababu kasoma sana ni meneja sehemu flani je huoni kama huyo mtoto tumboni anakuja kurithi akili za baba yake aje kuwa msomi baadae, kama umempenda mwanaume sababu ni mcheza mpira mzuri huoni kama kakuachia mchezaji wa baadae ambaye atakuja kuchezea timu kubwa akusaidie,
Kama mpenzi wako ni mwanamuziki huoni amekuachia zawadi ambayo kuna siku huyo mtoto ataenda kuimba kwenye majukwaa makubwa mama ukiwa unafurahia umati wa watu waliojaa kwenye show ya mwanao, kama mpenzi wako ni mfanyabiashara akikupa mimba akakuacha huoni kakuachia zawadi ya mtoto ambaye atakuja kumiliki biashara zake baadae.
Haina haja ya kulia kabisa na wala usihuzunike kuwa amekupotezea muda wako bali furahi maana amekuachia zawadi ambayo baada ya miaka itakuwa ndio faraja yako ya kweli.
Kama wewe binti una akili na mume aliyekupa mimba ana akili jua mtoto atarithi kutoka kwenye hizo akili zenu kwa maana hiyo hujabeba tu mtoto tumboni bali umebeba dini ambalo siku litakupa faida kubwa.
Kulia sana ni kumtia nuksi mtoto wako bali shukuru mungu na uamini kila jambo linatokea kwa sababu.
Kitu cha kwanza na cha msingi kwa binti unapoanza mahusiano na mwanaume lazima kuna kitu unique kwa huyo mwanaume ndio mana ukawaacha wote na ukampenda.Sasa kama huyo mwanaume ana kitu unique basi hiyo ndio sababu kubwa ambayo inatakiwa ikupe amani hata kama atakupa mimba akukimbie.
Kitu cha pili kama wakati unapata mimba ilikuwa sio kwa kubakwa na siku hiyo mimba inaingia ulifurahia lile tendo basi hiyo ni sababu nyingine ya kukufanya usilie kwa sababu amekuachia mimba.
Leo jiulize kama umempenda mwanaume wako sababu kasoma sana ni meneja sehemu flani je huoni kama huyo mtoto tumboni anakuja kurithi akili za baba yake aje kuwa msomi baadae, kama umempenda mwanaume sababu ni mcheza mpira mzuri huoni kama kakuachia mchezaji wa baadae ambaye atakuja kuchezea timu kubwa akusaidie,
Kama mpenzi wako ni mwanamuziki huoni amekuachia zawadi ambayo kuna siku huyo mtoto ataenda kuimba kwenye majukwaa makubwa mama ukiwa unafurahia umati wa watu waliojaa kwenye show ya mwanao, kama mpenzi wako ni mfanyabiashara akikupa mimba akakuacha huoni kakuachia zawadi ya mtoto ambaye atakuja kumiliki biashara zake baadae.
Haina haja ya kulia kabisa na wala usihuzunike kuwa amekupotezea muda wako bali furahi maana amekuachia zawadi ambayo baada ya miaka itakuwa ndio faraja yako ya kweli.
Kama wewe binti una akili na mume aliyekupa mimba ana akili jua mtoto atarithi kutoka kwenye hizo akili zenu kwa maana hiyo hujabeba tu mtoto tumboni bali umebeba dini ambalo siku litakupa faida kubwa.
Kulia sana ni kumtia nuksi mtoto wako bali shukuru mungu na uamini kila jambo linatokea kwa sababu.