sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,028
Nakumbuka nywele zilikuwa nyingi sana hadi ikawa kero, nilipopata muda jioni ikabidi niende mtaani kunyoa,
Kinyozi alikuwa kavaa kiheshima na yeye kanyoa kiheshima nywele zake, hakuuliza ninyoe vipi ila kwa muonekano wake nikajua ataninyoa kawaida, ila kulikuwa hakuna kioo.
Eeeh, kamaliza ndo kanipa kiooo nijicheki, Yesu Maria na Yosefu!! yani kichwa kimegeuka kuwa kama kitunguu, kaninyoa kiduku kile cha vibaka !! na hapo ikumbukwe nina mke, watoto, ninafanya kazi serikalini,
yani tulizinguana sana sio kidogo, ilibaki kidogo nimpige ngumi ya uso maana nilikasirika sana.
ilibidi tu nisepe hapo nikavaa kofia mpaka nlipofika kwa vinyozi wanaojielewa nikapigwa upara maana style aliyoninyoa yule bwanza huku pembeni alipiga upara kabisa juu akaziacha.
Kuanzia siku hio kila nikienda kwa kinyozi lazima niwaambie wanyoe vipi
Kinyozi alikuwa kavaa kiheshima na yeye kanyoa kiheshima nywele zake, hakuuliza ninyoe vipi ila kwa muonekano wake nikajua ataninyoa kawaida, ila kulikuwa hakuna kioo.
Eeeh, kamaliza ndo kanipa kiooo nijicheki, Yesu Maria na Yosefu!! yani kichwa kimegeuka kuwa kama kitunguu, kaninyoa kiduku kile cha vibaka !! na hapo ikumbukwe nina mke, watoto, ninafanya kazi serikalini,
yani tulizinguana sana sio kidogo, ilibaki kidogo nimpige ngumi ya uso maana nilikasirika sana.
ilibidi tu nisepe hapo nikavaa kofia mpaka nlipofika kwa vinyozi wanaojielewa nikapigwa upara maana style aliyoninyoa yule bwanza huku pembeni alipiga upara kabisa juu akaziacha.
Kuanzia siku hio kila nikienda kwa kinyozi lazima niwaambie wanyoe vipi