Wadau,
Naomba kujuzwa kama kuna ulazima wa kufanyia inspection magari yanayoingizwa kutoka nchi za nje, na je kama hujafanyia inspection kuna hatua gani zitachukuliwa na mamlaka husika(TRA?)
Inspection ni lazima kutokana na taratibu zilizowekwa kwenye uingizaji wa magari nchini. kwa magari yanayotokea UK inatakiwa ufanye inspection kama kama hilo Gari halina valid MOT,kwa japan na dubai lazima yafanyiwe inspection, iwapo hautafanya inspection au hauna Valid MOT, kitaratibu hautaweza kulitoa bandarini mpaka ulipe faini ambayo ni kubwa ukilinganisha na gharama za ukaguzi pia utakuwa umepoteza muda kulitoa hilo gari bandari kitu ambacho kitakuongezea gharama bandarini. TBS NDIO wanahusika na Inspection na TRA hawawezi kutoa release bila ya TBS kuruhsu..
nadhani litakuwa ni gari lako au umenunua kwa mtu binafsi
maana kama umenunua kwa routine exporters wa Japan au Dubai kwa mfano, wao wanajua hiyo ni standard procedure ya inspection certificate kabla ya ku export.
kwa Japan export inspection certificate ni kama $200 na inakuwa itemized kwenye bili ya gari ikiambatana na (exclusive of) CIF (bei ya gari, uchukuzi na bima).
sasa, kwa gharama za ziada ambazo utaingia kwa ku import gari pembeni ya CIF, hiyo $200 mbona cha mtoto, you got bigger fish to fry
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.