Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Baada ya kutangazwa kwa matokeo ya urais, Prof. Lipumba kwaniaba ya wagombea wenzake alipewa fursa ya kutoa neno; katika nasaha zake, alianza kwa kumpongeza JK kwa kutangazwa kuwa mshindi na akamalizia kwa kumkabidhi ilani ya uchaguzi ya chama chake. Kwa wadadisi wa mambo, kitenda cha kusema kuwa alikuwa anampongeza rais mteule kwa kutangazwa kuwa mshindi, na wala siyo kwa kuchaguliwa kuwa rais, kilikuwa kinarejelea ujumbe ule ule uliotolewa na Maalim Seif huko Zenj, wakati aliposema ya kuwa, kati yake na Shein apakuwepo mshindi. Kwa maneno mengine, viongozi wote wawili wa CUF walikuwa wanatoa ujumbe ya kwamba ushindi iliupata CCM katika chaguzi zote mbili ulikuwa ni wa mezani na wala siyo wa wapiga kura, na hivyo chama hicho hakina uhalali wowote wa kwenda kifua mbele.