EJM_
JF-Expert Member
- Jul 8, 2011
- 3,836
- 2,090
Juzi Rais Magufuli ametoa hotuba iliyoonyesha dhamira ya Serikali kutokuwa tayari kufunga baadhi ya mikoa (lockdown) yenye maambukizi makubwa ya Covid19 hapa nchini. Sababu kubwa ya raisi ni kwamba mikoa hii (hasa Dar es salaam) ndio source kubwa ya mapato yabserikali kwahiyo kuilockdown ni kulockdown pia mapato ya serikali.
Mimi sitaangalia sana kibinadamu kwa maana ya mapato vs uhai kwasababu hili limeongelewa sana. Nitaangalia kwa muktadha rahisi kabisa wa kiuchumi.
Kwa sasa serikali imeacha mipaka yetu wazi ili kutofunga njia za kiuchumi (kasoro uwanja wa ndege pekee) hii imeelezwa pia na rais kuwa kama tukifunga mipaka kuna hatari ya nchi nyingine 8 kuathirika kama tutafunga mipaka yetu (ingawa nyingi ya hizo nchi wamefunga mipaka yao kwahiyo tunawahurumia watu ambao hawatuhurumii bali wanajihurumia wao)
Sasa hofu yangu iko hapa
Baada ya muda janga hili litakwisha na tutarudi kwenye maisha ya kawaida. Hata hivyo effect zake zitakaa kwa muda mrefu kidogo na ndio hizo ninazozohofia kuwa zinaweza kuja kuwa na athari hasi kubwa kwenye uchumi wetu.
Mfano baada ya janga hili, nchi nyingi zitachukua tahadhari ya watu wanaoingia na kutoka nchini mwao na zile ambazo zilichukua hatua madhubuti za kuzuia ugonjwa huu zitapata ahueni ya kiuchumi haraka kuliko zile zilizobaki kushangaa kutegemea rehema za Mungu.
Mfano tunaweza kujikuta tunazuiliwa kuingia nchi nyingine kwasababu itaonekana kuna possibility yabkuwapelekea Corona na hivyo kujikuta hatuwezi kufanya biashara zetu nje ya nchi yetu. Pia tunaweza kujikuta hata bandari yetu inapoteza biashara kubwa kwankigezo hicho na baadhi ya nchi kuamua kupitishia bidhaa zao bandari za Beira, Mombasa au hata Africa kusini ambako watakuwa na uhakika na afya zao.
Tunajua tunategemea sana utalii ili kuingiza fedha za kigeni. Sasa hao wazungu ambao ndio wanakuja kutalii hapa kwetu wakiambiwa tu kwamba wasije kwetu wasababu tulihandle vibaya Covid19 cases na kuna possibility ya kuwa na wagonjwa huko, hawatakuja na hii itakuwa a big blow for us.
Kwa haya machache tunaweza kuhusi tunaokoa mapato kidogo kwa sasa huku tukiwa tunaua kabisa uchumi hapo baadae.
Tuwe makini
Mimi sitaangalia sana kibinadamu kwa maana ya mapato vs uhai kwasababu hili limeongelewa sana. Nitaangalia kwa muktadha rahisi kabisa wa kiuchumi.
Kwa sasa serikali imeacha mipaka yetu wazi ili kutofunga njia za kiuchumi (kasoro uwanja wa ndege pekee) hii imeelezwa pia na rais kuwa kama tukifunga mipaka kuna hatari ya nchi nyingine 8 kuathirika kama tutafunga mipaka yetu (ingawa nyingi ya hizo nchi wamefunga mipaka yao kwahiyo tunawahurumia watu ambao hawatuhurumii bali wanajihurumia wao)
Sasa hofu yangu iko hapa
Baada ya muda janga hili litakwisha na tutarudi kwenye maisha ya kawaida. Hata hivyo effect zake zitakaa kwa muda mrefu kidogo na ndio hizo ninazozohofia kuwa zinaweza kuja kuwa na athari hasi kubwa kwenye uchumi wetu.
Mfano baada ya janga hili, nchi nyingi zitachukua tahadhari ya watu wanaoingia na kutoka nchini mwao na zile ambazo zilichukua hatua madhubuti za kuzuia ugonjwa huu zitapata ahueni ya kiuchumi haraka kuliko zile zilizobaki kushangaa kutegemea rehema za Mungu.
Mfano tunaweza kujikuta tunazuiliwa kuingia nchi nyingine kwasababu itaonekana kuna possibility yabkuwapelekea Corona na hivyo kujikuta hatuwezi kufanya biashara zetu nje ya nchi yetu. Pia tunaweza kujikuta hata bandari yetu inapoteza biashara kubwa kwankigezo hicho na baadhi ya nchi kuamua kupitishia bidhaa zao bandari za Beira, Mombasa au hata Africa kusini ambako watakuwa na uhakika na afya zao.
Tunajua tunategemea sana utalii ili kuingiza fedha za kigeni. Sasa hao wazungu ambao ndio wanakuja kutalii hapa kwetu wakiambiwa tu kwamba wasije kwetu wasababu tulihandle vibaya Covid19 cases na kuna possibility ya kuwa na wagonjwa huko, hawatakuja na hii itakuwa a big blow for us.
Kwa haya machache tunaweza kuhusi tunaokoa mapato kidogo kwa sasa huku tukiwa tunaua kabisa uchumi hapo baadae.
Tuwe makini