kinetiq01
Member
- Aug 25, 2006
- 49
- 0
Huenda si hoja mpya, lakini najiuliza endapo tunajua kwamba Kenya inanufaika zaidi na Kiswahili licha ya kuwa na wazungumzaji wachache kuliko Tanzania?
Nasema hayo kwasababu kibiashara au kiteknolojia inaonyesha Kenya inapata miradi mingi na mikubwa zaidi kuliko Tanzania kwa kigezo cha lugha ya Kiswahili.Nitatoa mfano:-
1. Jumapili ijayo Facebook watafanya sherehe Nairobi ya kuzindua mradi wa Facebook kwa lugha ya Kiswahili. CEO na founder Mark Zuckerberg ndiye atakuwa mgeni rasmi.
2. Microsoft wamekuwa na ofisi kubwa Nairobi kwa muda mrefu, ambapo project yao ya OS localisation imepata mafanikio makubwa.
3. Google wana ofisi ya kanda Nairobi, wanafanya shughuli mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuunda translation tool ya Kiswahili.
Mashirika yote haya yanaajiri wataalam wa Kiswahili ambapo kwa asilimia kubwa ni wakenya. Sisi wa kwetu wanaishia kulalamika kuwa Kiswahili kinachotumika siyo fasaha, lakini hawachukui hatua kuwavutia hao wenye miradi kuiendeleza ndani ya Tanzania.
Nimetoa mifano hiyo michache, lakini yako mambo mengi ambayo naona hatuyachangamkii. Kama kuna kitu watanzania tungeweza kufanikiwa kwa urahisi ni ku-export Kiswahili kama product, hakuna wa kutubabaisha. Lakini wapi bwana. Najiuliza tatizo ni nini? Zifuatazo zaweza kuwa baadhi ya sababu.
- Hatuna sera ya kitaifa kujenga na kutumia Kiswahili kama biashara
- Huenda ikawa sisi hatujui kutumia fursa zinazojitokeza.
- Huenda jamaa wakiwasilisha mawazo ya kufanya kazi zao kwetu hawapati ushirikiano.
- Huenda mawasiliano duni ya teknolojia yanawakatisha tamaa
- Hatuna wataalam wa Kiswahili ingawa tuna wazungumzaji wa Kiswahili
Nasema hayo kwasababu kibiashara au kiteknolojia inaonyesha Kenya inapata miradi mingi na mikubwa zaidi kuliko Tanzania kwa kigezo cha lugha ya Kiswahili.Nitatoa mfano:-
1. Jumapili ijayo Facebook watafanya sherehe Nairobi ya kuzindua mradi wa Facebook kwa lugha ya Kiswahili. CEO na founder Mark Zuckerberg ndiye atakuwa mgeni rasmi.
2. Microsoft wamekuwa na ofisi kubwa Nairobi kwa muda mrefu, ambapo project yao ya OS localisation imepata mafanikio makubwa.
3. Google wana ofisi ya kanda Nairobi, wanafanya shughuli mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuunda translation tool ya Kiswahili.
Mashirika yote haya yanaajiri wataalam wa Kiswahili ambapo kwa asilimia kubwa ni wakenya. Sisi wa kwetu wanaishia kulalamika kuwa Kiswahili kinachotumika siyo fasaha, lakini hawachukui hatua kuwavutia hao wenye miradi kuiendeleza ndani ya Tanzania.
Nimetoa mifano hiyo michache, lakini yako mambo mengi ambayo naona hatuyachangamkii. Kama kuna kitu watanzania tungeweza kufanikiwa kwa urahisi ni ku-export Kiswahili kama product, hakuna wa kutubabaisha. Lakini wapi bwana. Najiuliza tatizo ni nini? Zifuatazo zaweza kuwa baadhi ya sababu.
- Hatuna sera ya kitaifa kujenga na kutumia Kiswahili kama biashara
- Huenda ikawa sisi hatujui kutumia fursa zinazojitokeza.
- Huenda jamaa wakiwasilisha mawazo ya kufanya kazi zao kwetu hawapati ushirikiano.
- Huenda mawasiliano duni ya teknolojia yanawakatisha tamaa
- Hatuna wataalam wa Kiswahili ingawa tuna wazungumzaji wa Kiswahili